Friday, August 31, 2012

Wahadzabe walikula pundamilia 18 ili kushiriki sensa

 
Vijana wa Kihadzabe wakicheza ngoma.

HIVI karibuni kabila la Wahadzabe lililopo lilizua gumzo baada ya kutoa sharti la kupatiwa nyama ya tumbili ili liweze kushiriki katika Sensa ya Watu na Makazi.

Tofauti na matarajio ya watu kwamba viongozi wa kabila hilo wangekamatwa na Dola kwa kitendo cha kuipa Serikali masharti ambayo ni kinyume na sheria ya sensa, Serikali ilikubali kulipatia kabila hilo nyama ya pundamilia 18 badala ya tumbili jambo lililofanikisha kujenga mazingira rafiki yaliyowezesha Wahadzabe kuhesabiwa.

Ingawa Serikali ingeweza kukataa sharti hilo, viongozi walitumia busara kwa kuzingatia mambo mbalimbali hasa sifa za kipekee za kabila hilo ikiwa ni pamoja na ukosefu wa makazi ya kudumu. Kabila hilo halina utaratibu wa kuhodhi mali kwa kuwa haliwekezi katika mifugo, biashara wala kilimo.

Ni dhahiri kuwa wasingetimiza masharti yao isingekuwa rahisi kuwapata na kuwahesabu kwa kuwa ni wachache na hawana makazi maalumu. Kabila la Wahadzabe ni miongoni mwa makabila madogo yaliyopo katika hatari ya kutoweka kwa kuwa watu wake hawaongezeki kwa kasi ikilinganishwa na makabila mengine.

Hadza au Wahadzabe ni kabila linaloishi Kaskazini ya Kati Tanzania wanoishi kuzunguka Ziwa Eyasi eneo la Karatu, Mkoa wa Manyara, pia wanapatikana Mbulu, Iramba, Meatu na Maswa. Kabila hilo ni jamii pekee nchini Tanzania inayoishi kwa kutumia mfumo wa binadamu wa kale ambapo wanaishi kwa kutegemea uwindaji pamoja na kukusanya mizizi na matunda ya pori kama chakula kikuu.

Tofauti na makabila mengine ambayo yanajihusisha na kilimo, ufugaji, uvuvi, biashara na shughuli mbalimbali za kuingiza kipato, shughuli kubwa ya wanaume wa Kihadzabe huwinda kwa kutumia upinde na mshale. Wanawake wanajihusisha na ukusanyaji wa mboga, mizizi na matunda pori kisha kukusanyika pamoja na kula kisha kukaa kwa ajili ya kusubiri kesho.

Wanawake wa Kihadzabe wakishamaliza kukusanya mizizi na matunda kugonga na kusaga mbegu za ubuyu kisha kutumia unga wake kutengenezea uji. Wakati wanaume hutumia muda wao kutengeneza upinde na mishale.

Kwa kifupi kabila hilo halijui thamani wala karaha ya kukosa fedha kwa sababu linaishi maisha ya kipekee katika maeneo ya nyikani ambapo hakuna matumizi ya kujenga nyumba, samani za ndani, kununua nguo, chakula wala gharama za matibabu.

Mwandishi wa Kitabu cha utamaduni mila na desturi za makabila ya Kaskazini Mashariki ya Tanzania Gervase Mlola anasema mfumo wa maisha ya Wahadzabe unajenga imani kuwa kabila hilo ni masalia ya binadamu wa kwanza ambaye aliishi kwa kula nyama, mizizi na matunda.

Pia utafiti wa kisayansi unaonesha kuwa masalia ya mifupa ya mwanadamu wa kwanza aliyeishi miaka milioni 4 iliyopita yalipatikana katika makazi ya Wahadzabe jambo linalothibitisha kuwa kizazi cha kabila hilo kina uhusiano wa moja kwa moja na binadamu wa kwanza.

Mlola anasema watu wa kabila hilo wana miili midogo, ni weusi na wana chale kwenye mashavu. Hata hivyo watu wa kabila hilo hawatogi masikio, hawavai wala hawaweki chochote masikioni kama ilivyo kwa makabila mengine yanayoishi maeneo ya jirani.

Utafiti uliyofanywa kuhusu kukua kwa jamii za Kiafrika zilizostaarabika unaonesha kuwa Wahadzabe ambao ni maarufu kwa jila na Watindiga waliishi katika ardhi ya Tanzania kwa miaka mingi kabla ya kuingia kwa kizazi cha watu jamii ya Wabantu ambao mfumo wao wa maisha ulikuwa tofauti kwa kuwa walistaarabika zaidi na kutumia zana za kisasa. Lugha ya Wahadzabe inaju

likana kama Khoisan ambayo ni sawa na watu jamii nyingine zinazozungumza lugha Afrika ya Kusini, Wasandawe wanaishi Kondoa katika Mkoa wa Dodoma ndio kabila pekee lenye uhusiano wa karibu na Wahadzabe. Inasemekana kuwa miaka ya nyuma Wasandawe waliishi kwa kuwinda na kukusanya matunda ila hivi sasa wamebadilika kulingana na mabadiliko ya mfumo wa maisha.

Mila na desturi za kabila la Wahadzabe zinarithiwa na kizazi kipya bila kufanya mabadiliko makubwa jambo linalosababisha
kabila kuwa na mfumo wa kizamani ambao ni kikwazo kikubwa kwa maendeleo. Upinde na mshale ni jambo la muhimu na la lazima kurithiwa na vijana wa kiume katika jamii ya Wahadzabe.

Kila mwanamume ana upinde na mishale ya kutosha yenye sumu kwa ajili ya kuwinda wanyama wakubwa na isiyokuwa na sumu kwa ajili ya wanyama wadogo kama digidigi na swala. Wahadzabe wamekuwa wakiishi kwa muda mrefu bila kutawaliwa.

Tofauti na makabila mengine, Wahadzabe hawana utawala unaotegemea kiongozi wa kisiasa, kimila wala mganga wa jadi kwa ajili ya kuita mvua wala kuponya watu. Wanaishi katika makundi ambayo yana msemaji mmoja au wawili. Wasemaji huchaguliwa kutoka rika lolole ila ni lazima awe na uwezo wa kujieleza.

Hata hivyo wakati wa majadiliano kila mtu anapata nafasi sawa na maamuzi yanatolewa kwa kuzingatia kundi kubwa pasipo na kiongozi wa kutoa ushawishi kwa kundi moja kuunga mkono kundi lingine. Ingawa hawana uongozi huishi kwa kuheshimiana na kila mtu anajua wajibu wake pasipo kusukumwa.

Wahadzabe wanaishi katika makambi ya muda mfupi ambapo kambi moja hukaa watu wazima takribani 30. Kambi hupewa jina la mtu maarufu katika kambi husika na mtu huyo huchukuliwa kama kiongozi ingawa hana sauti wala uwezo wa kutoa maamuzi dhidi ya wenzake.

Kabila hilo kutembea kwa makundi ili kuweza kukabiliana na hatari hasa wanyama wakali wakati wa kuwinda. Wakiwinda
wanyama wadogo watamchinja na kuwagawa nyama kwa uwiano sawa kisha kila mtu hupeleka nyama hiyo kwenye familia yake.

Endapo watafanikiwa kuua mnyama mkubwa kama nyati wataitana na kundi nzima litakaa eneo la tukio watu kwa ajili ya kuchinja na kula nyama kwa pamoja. Kwa Mhadzabe hakuna kinachotupwa, baada ya kula nyama hutumia ngozi kutengenezea mavazi pia husaga mifupa na kutoa mafuta na baadhi ya mifupa hutumia kutengeneza ncha za mishale ya kuwindia.

Baadhi ya ncha za mishale hupakazwa sumu kwa ajili ya kuwinda wanyama wakubwa. Utengenezaji wa mishale ya sumu
hufanyika kitaalamu na ujuzi huo unarithiwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine. Utafiti unaonesha kuwa kabila hilo halikuathiriwa na mfumo dume.

Wanawake na wanaume hushiriki katika shughuli za kijamii kisha hugawana chakula pasipo ubaguzi wa kijinsia. Katika jumuiya ya Wahadzabe hakuna anayepatwa na njaa. Wahadzabe wote huwa na tabia ya kuvuta tumbaku. Waume kwa wanawake, wazee kwa vijana, wote wanapokaa katika kikundi huwa na kawaida ya kushirikiana kuvuta mtemba maarufu kama kiko ambacho hutengenezwa kutokana na mawe laini.

Vijana wa kiume ndiyo huwa na jukumu la kuteka maji kisha kwenda kuwinda ndege kwa kutumia mishale. Ndege hao hunyonyolewa manyoya na kuchomwa. Manyoya hutumika kutengenezea mishale na kwa kawaida hakuna kinachotupwa kutokana na ndege au mnyama aliyewindwa.

Kwa kuwa Wahadzabe wanazingatia na kuthamini mfumo wa ikilojia hujenga makazi yao mbali na vyanzo vya maji ili kuepuka
kuharibu vyanzo vya maji, kutisha wanyama pia kujiepusha na wadudu wanaoeneza maradhi hususan malaria. Tofauti na makabila mengine, Wahadzabe hawana tabia ya kujiona wao ni bora kuliko wanyama.

Wao wanaamini katika ikolojia kwamba ardhi, wanyama na mimea ni vitu vinavyotegemeana na hakuna chenye ubora kuliko
kingine. Huishi kwa kushirikiana bila kubadili wala kuharibu mazingira. Kila kitu hutumiwa kwa faida ya wote.

Ingawa wana mila ngumu, vijana huweza kumudu changamoto za maisha bila taabu. Watoto wa Kihadzabe, wenye umri kuanzia miaka nane wanaweza kujitafutia maisha yao na hata familia zao kwa kuwa hujifunza kazi za wakubwa wangali na
umri mdogo.

Uwindaji ni sehemu ya starehe kwa vijana wa Kihadzabe. Pia wana ujuzi wa kutengeneza visu vya vyuma ambavyo vinafanana na zana za kale enzi za mawe. Jioni ni muda wa kupumzika. Vijana huwa na kazi ya kuwasha moto na kuchoma nyama. Wazee huota moto kwa kuuzunguka.

Pia wanapata muda wa kucheza pamoja na kufurahi. Wakati wa kucheza huweka mduara kisha kucheza na kuimba huku wakipiga makofi na kuzunguka duara. Pia wana ngoma ambazo hutumia vifaa mbalimbali vya muziki. Wanapokuwa na tatizo hushikamana na kushirikiana hasa kwa kusali nyakati za usiku ili Mungu aweze kusikia kilio chao na kuwaondolea tatizo.

Ingawa ni jamii iliyopo nyuma kimaendeleo zipo ishara zinazoonesha kuwa walikuwa na ujuzi fulani katika kufanya mawasiliano. Wakati wa kurina asali Wahadzabe wanawasha moto unaotoa moshi mzito ili kuwafukuza nyuki kisha kurina asali pasipo kushambuliwa na nyuki.

Kila wanapomaliza kurina asali hasa kwenye mibuyu walichonga vijiti mithili ya msumari kisha kuvipigilia kwenye mbuyu kama ishara kuwa Mhadzabe aliwahi kurina asali kwenye mti huo. Hadi miaka ya hivi karibuni Wahadzabe wamekuwa wakichora kwenye miamba, kama yanavyofanya makabila mengine yaishiyo jirani.

Ingawa hawana kiongozi wa kiimani, Wahadzabe wanamkusanyiko wa hadithi, zinazoelezea miiko na imani kuhusu maisha
yao. Kwa mujibu wa hadithi hizo kabila hilo linaongozwa na mungu anayefahamika kwa jina la Ishoko. Ishoko amekuwepo tangu mwanzo wa dahari na kusaidia kizazi kimoja kwenda kingine.

Ishoko ambaye ni rafiki wa ambaye amewezesha watu wote kukua vyema na kufahamu mambo mbalimbali hasa mema
na mabaya. Anafundisha watu kujua kazi na wajibu wa kila mtu kulingana na mila na desturi, pia anatunza mazingira kwa kuzingatia uwiano wa ikolojia.

Ishoko anafananishwa na malaika ambaye aliweza kuwatoa Wahadzabe kwenye umbo la awali lililokuwa sawa na la mnyama na kuwaweka katika hali ya ubinadamu. Ishoko aliwawezesha kuondokana na mateso ya kula nyama mbichi kwa kuwapatia moto.

Wanaamini kuwa hata bakuli na mkuki wa kwanza ulitengenezwa na malaika kisha kuwafundisha jinsi ya kutumia kwa lengo la kuboresha maisha. Ni rahisi kuwatambua Wahadzabe kwa mavazi yao. Bado wanavaa nguo zilizotengenezwa kwa vipande vya ngozi zinazotokana na wanyama mbalimbali.

Wanaume wanaokwenda mawindoni huvaa ngozi nene ya baboon. Wahadzabe walioendelea wanavaa kaptula na wanawake wanajifunga vipande vya khanga na vitenge. Ila wengi wao wanavaa vipande vya ngozi vilivyolainishwa vizuri kisha kunakishiwa na shanga za njano, nyeupe na bluu bahari.

Ingawa wana mila ngumu mabadiliko ya mfumo wa maisha hasa mpango wa Serikali wa kuendeleza watu wake unaathiri
mfumo, mila na desturi za maisha ya Wahadzabe. Athari hizo zinaonekana kupitia programu za elimu ambapo hivi sasa watoto wengi wanaandikishwa shule. Jambo hilo linasababisha wazazi wao kujihusisha na shughuli za kuwaingizia kipato ili waweze kununua sare na kulipa ada za shule. Vijana wachache wa Kihadzabe wanapopata elimu wanahama katika makazi duni na kuishi maeneo mengine yenye maendeleo kisha kuhawahamisha wazazi wao ili nao waweze kujionea dunia katika taswira tofauti na maisha ya kula nyama na mizizi.

Wahadzabe walikula pundamilia 18 ili kushiriki sensa

 
Vijana wa Kihadzabe wakicheza ngoma.

HIVI karibuni kabila la Wahadzabe lililopo lilizua gumzo baada ya kutoa sharti la kupatiwa nyama ya tumbili ili liweze kushiriki katika Sensa ya Watu na Makazi.

Tofauti na matarajio ya watu kwamba viongozi wa kabila hilo wangekamatwa na Dola kwa kitendo cha kuipa Serikali masharti ambayo ni kinyume na sheria ya sensa, Serikali ilikubali kulipatia kabila hilo nyama ya pundamilia 18 badala ya tumbili jambo lililofanikisha kujenga mazingira rafiki yaliyowezesha Wahadzabe kuhesabiwa.

Ingawa Serikali ingeweza kukataa sharti hilo, viongozi walitumia busara kwa kuzingatia mambo mbalimbali hasa sifa za kipekee za kabila hilo ikiwa ni pamoja na ukosefu wa makazi ya kudumu. Kabila hilo halina utaratibu wa kuhodhi mali kwa kuwa haliwekezi katika mifugo, biashara wala kilimo.

Ni dhahiri kuwa wasingetimiza masharti yao isingekuwa rahisi kuwapata na kuwahesabu kwa kuwa ni wachache na hawana makazi maalumu. Kabila la Wahadzabe ni miongoni mwa makabila madogo yaliyopo katika hatari ya kutoweka kwa kuwa watu wake hawaongezeki kwa kasi ikilinganishwa na makabila mengine.

Hadza au Wahadzabe ni kabila linaloishi Kaskazini ya Kati Tanzania wanoishi kuzunguka Ziwa Eyasi eneo la Karatu, Mkoa wa Manyara, pia wanapatikana Mbulu, Iramba, Meatu na Maswa. Kabila hilo ni jamii pekee nchini Tanzania inayoishi kwa kutumia mfumo wa binadamu wa kale ambapo wanaishi kwa kutegemea uwindaji pamoja na kukusanya mizizi na matunda ya pori kama chakula kikuu.

Tofauti na makabila mengine ambayo yanajihusisha na kilimo, ufugaji, uvuvi, biashara na shughuli mbalimbali za kuingiza kipato, shughuli kubwa ya wanaume wa Kihadzabe huwinda kwa kutumia upinde na mshale. Wanawake wanajihusisha na ukusanyaji wa mboga, mizizi na matunda pori kisha kukusanyika pamoja na kula kisha kukaa kwa ajili ya kusubiri kesho.

Wanawake wa Kihadzabe wakishamaliza kukusanya mizizi na matunda kugonga na kusaga mbegu za ubuyu kisha kutumia unga wake kutengenezea uji. Wakati wanaume hutumia muda wao kutengeneza upinde na mishale.

Kwa kifupi kabila hilo halijui thamani wala karaha ya kukosa fedha kwa sababu linaishi maisha ya kipekee katika maeneo ya nyikani ambapo hakuna matumizi ya kujenga nyumba, samani za ndani, kununua nguo, chakula wala gharama za matibabu.

Mwandishi wa Kitabu cha utamaduni mila na desturi za makabila ya Kaskazini Mashariki ya Tanzania Gervase Mlola anasema mfumo wa maisha ya Wahadzabe unajenga imani kuwa kabila hilo ni masalia ya binadamu wa kwanza ambaye aliishi kwa kula nyama, mizizi na matunda.

Pia utafiti wa kisayansi unaonesha kuwa masalia ya mifupa ya mwanadamu wa kwanza aliyeishi miaka milioni 4 iliyopita yalipatikana katika makazi ya Wahadzabe jambo linalothibitisha kuwa kizazi cha kabila hilo kina uhusiano wa moja kwa moja na binadamu wa kwanza.

Mlola anasema watu wa kabila hilo wana miili midogo, ni weusi na wana chale kwenye mashavu. Hata hivyo watu wa kabila hilo hawatogi masikio, hawavai wala hawaweki chochote masikioni kama ilivyo kwa makabila mengine yanayoishi maeneo ya jirani.

Utafiti uliyofanywa kuhusu kukua kwa jamii za Kiafrika zilizostaarabika unaonesha kuwa Wahadzabe ambao ni maarufu kwa jila na Watindiga waliishi katika ardhi ya Tanzania kwa miaka mingi kabla ya kuingia kwa kizazi cha watu jamii ya Wabantu ambao mfumo wao wa maisha ulikuwa tofauti kwa kuwa walistaarabika zaidi na kutumia zana za kisasa. Lugha ya Wahadzabe inaju

likana kama Khoisan ambayo ni sawa na watu jamii nyingine zinazozungumza lugha Afrika ya Kusini, Wasandawe wanaishi Kondoa katika Mkoa wa Dodoma ndio kabila pekee lenye uhusiano wa karibu na Wahadzabe. Inasemekana kuwa miaka ya nyuma Wasandawe waliishi kwa kuwinda na kukusanya matunda ila hivi sasa wamebadilika kulingana na mabadiliko ya mfumo wa maisha.

Mila na desturi za kabila la Wahadzabe zinarithiwa na kizazi kipya bila kufanya mabadiliko makubwa jambo linalosababisha
kabila kuwa na mfumo wa kizamani ambao ni kikwazo kikubwa kwa maendeleo. Upinde na mshale ni jambo la muhimu na la lazima kurithiwa na vijana wa kiume katika jamii ya Wahadzabe.

Kila mwanamume ana upinde na mishale ya kutosha yenye sumu kwa ajili ya kuwinda wanyama wakubwa na isiyokuwa na sumu kwa ajili ya wanyama wadogo kama digidigi na swala. Wahadzabe wamekuwa wakiishi kwa muda mrefu bila kutawaliwa.

Tofauti na makabila mengine, Wahadzabe hawana utawala unaotegemea kiongozi wa kisiasa, kimila wala mganga wa jadi kwa ajili ya kuita mvua wala kuponya watu. Wanaishi katika makundi ambayo yana msemaji mmoja au wawili. Wasemaji huchaguliwa kutoka rika lolole ila ni lazima awe na uwezo wa kujieleza.

Hata hivyo wakati wa majadiliano kila mtu anapata nafasi sawa na maamuzi yanatolewa kwa kuzingatia kundi kubwa pasipo na kiongozi wa kutoa ushawishi kwa kundi moja kuunga mkono kundi lingine. Ingawa hawana uongozi huishi kwa kuheshimiana na kila mtu anajua wajibu wake pasipo kusukumwa.

Wahadzabe wanaishi katika makambi ya muda mfupi ambapo kambi moja hukaa watu wazima takribani 30. Kambi hupewa jina la mtu maarufu katika kambi husika na mtu huyo huchukuliwa kama kiongozi ingawa hana sauti wala uwezo wa kutoa maamuzi dhidi ya wenzake.

Kabila hilo kutembea kwa makundi ili kuweza kukabiliana na hatari hasa wanyama wakali wakati wa kuwinda. Wakiwinda
wanyama wadogo watamchinja na kuwagawa nyama kwa uwiano sawa kisha kila mtu hupeleka nyama hiyo kwenye familia yake.

Endapo watafanikiwa kuua mnyama mkubwa kama nyati wataitana na kundi nzima litakaa eneo la tukio watu kwa ajili ya kuchinja na kula nyama kwa pamoja. Kwa Mhadzabe hakuna kinachotupwa, baada ya kula nyama hutumia ngozi kutengenezea mavazi pia husaga mifupa na kutoa mafuta na baadhi ya mifupa hutumia kutengeneza ncha za mishale ya kuwindia.

Baadhi ya ncha za mishale hupakazwa sumu kwa ajili ya kuwinda wanyama wakubwa. Utengenezaji wa mishale ya sumu
hufanyika kitaalamu na ujuzi huo unarithiwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine. Utafiti unaonesha kuwa kabila hilo halikuathiriwa na mfumo dume.

Wanawake na wanaume hushiriki katika shughuli za kijamii kisha hugawana chakula pasipo ubaguzi wa kijinsia. Katika jumuiya ya Wahadzabe hakuna anayepatwa na njaa. Wahadzabe wote huwa na tabia ya kuvuta tumbaku. Waume kwa wanawake, wazee kwa vijana, wote wanapokaa katika kikundi huwa na kawaida ya kushirikiana kuvuta mtemba maarufu kama kiko ambacho hutengenezwa kutokana na mawe laini.

Vijana wa kiume ndiyo huwa na jukumu la kuteka maji kisha kwenda kuwinda ndege kwa kutumia mishale. Ndege hao hunyonyolewa manyoya na kuchomwa. Manyoya hutumika kutengenezea mishale na kwa kawaida hakuna kinachotupwa kutokana na ndege au mnyama aliyewindwa.

Kwa kuwa Wahadzabe wanazingatia na kuthamini mfumo wa ikilojia hujenga makazi yao mbali na vyanzo vya maji ili kuepuka
kuharibu vyanzo vya maji, kutisha wanyama pia kujiepusha na wadudu wanaoeneza maradhi hususan malaria. Tofauti na makabila mengine, Wahadzabe hawana tabia ya kujiona wao ni bora kuliko wanyama.

Wao wanaamini katika ikolojia kwamba ardhi, wanyama na mimea ni vitu vinavyotegemeana na hakuna chenye ubora kuliko
kingine. Huishi kwa kushirikiana bila kubadili wala kuharibu mazingira. Kila kitu hutumiwa kwa faida ya wote.

Ingawa wana mila ngumu, vijana huweza kumudu changamoto za maisha bila taabu. Watoto wa Kihadzabe, wenye umri kuanzia miaka nane wanaweza kujitafutia maisha yao na hata familia zao kwa kuwa hujifunza kazi za wakubwa wangali na
umri mdogo.

Uwindaji ni sehemu ya starehe kwa vijana wa Kihadzabe. Pia wana ujuzi wa kutengeneza visu vya vyuma ambavyo vinafanana na zana za kale enzi za mawe. Jioni ni muda wa kupumzika. Vijana huwa na kazi ya kuwasha moto na kuchoma nyama. Wazee huota moto kwa kuuzunguka.

Pia wanapata muda wa kucheza pamoja na kufurahi. Wakati wa kucheza huweka mduara kisha kucheza na kuimba huku wakipiga makofi na kuzunguka duara. Pia wana ngoma ambazo hutumia vifaa mbalimbali vya muziki. Wanapokuwa na tatizo hushikamana na kushirikiana hasa kwa kusali nyakati za usiku ili Mungu aweze kusikia kilio chao na kuwaondolea tatizo.

Ingawa ni jamii iliyopo nyuma kimaendeleo zipo ishara zinazoonesha kuwa walikuwa na ujuzi fulani katika kufanya mawasiliano. Wakati wa kurina asali Wahadzabe wanawasha moto unaotoa moshi mzito ili kuwafukuza nyuki kisha kurina asali pasipo kushambuliwa na nyuki.

Kila wanapomaliza kurina asali hasa kwenye mibuyu walichonga vijiti mithili ya msumari kisha kuvipigilia kwenye mbuyu kama ishara kuwa Mhadzabe aliwahi kurina asali kwenye mti huo. Hadi miaka ya hivi karibuni Wahadzabe wamekuwa wakichora kwenye miamba, kama yanavyofanya makabila mengine yaishiyo jirani.

Ingawa hawana kiongozi wa kiimani, Wahadzabe wanamkusanyiko wa hadithi, zinazoelezea miiko na imani kuhusu maisha
yao. Kwa mujibu wa hadithi hizo kabila hilo linaongozwa na mungu anayefahamika kwa jina la Ishoko. Ishoko amekuwepo tangu mwanzo wa dahari na kusaidia kizazi kimoja kwenda kingine.

Ishoko ambaye ni rafiki wa ambaye amewezesha watu wote kukua vyema na kufahamu mambo mbalimbali hasa mema
na mabaya. Anafundisha watu kujua kazi na wajibu wa kila mtu kulingana na mila na desturi, pia anatunza mazingira kwa kuzingatia uwiano wa ikolojia.

Ishoko anafananishwa na malaika ambaye aliweza kuwatoa Wahadzabe kwenye umbo la awali lililokuwa sawa na la mnyama na kuwaweka katika hali ya ubinadamu. Ishoko aliwawezesha kuondokana na mateso ya kula nyama mbichi kwa kuwapatia moto.

Wanaamini kuwa hata bakuli na mkuki wa kwanza ulitengenezwa na malaika kisha kuwafundisha jinsi ya kutumia kwa lengo la kuboresha maisha. Ni rahisi kuwatambua Wahadzabe kwa mavazi yao. Bado wanavaa nguo zilizotengenezwa kwa vipande vya ngozi zinazotokana na wanyama mbalimbali.

Wanaume wanaokwenda mawindoni huvaa ngozi nene ya baboon. Wahadzabe walioendelea wanavaa kaptula na wanawake wanajifunga vipande vya khanga na vitenge. Ila wengi wao wanavaa vipande vya ngozi vilivyolainishwa vizuri kisha kunakishiwa na shanga za njano, nyeupe na bluu bahari.

Ingawa wana mila ngumu mabadiliko ya mfumo wa maisha hasa mpango wa Serikali wa kuendeleza watu wake unaathiri
mfumo, mila na desturi za maisha ya Wahadzabe. Athari hizo zinaonekana kupitia programu za elimu ambapo hivi sasa watoto wengi wanaandikishwa shule. Jambo hilo linasababisha wazazi wao kujihusisha na shughuli za kuwaingizia kipato ili waweze kununua sare na kulipa ada za shule. Vijana wachache wa Kihadzabe wanapopata elimu wanahama katika makazi duni na kuishi maeneo mengine yenye maendeleo kisha kuhawahamisha wazazi wao ili nao waweze kujionea dunia katika taswira tofauti na maisha ya kula nyama na mizizi.

Vituo vya ‘kuchimba dawa kwa abiria wa mabasi vyatangazwa



ABIRIA wa mabasi yaendayo mikoani kuanzia kesho watalazimika kuwa na fedha za ziada mifukoni kwa ajili ya kulipia huduma ya choo.

Fedha hizo zitatumiwa kulipia huduma hiyo baada ya Serikali kupitia Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini(Sumatra), kutangaza rasmi kwamba utaratibu wa abiria kushuka maporini na kujisaidia imepigwa marufuku.

Katika Mkutano wa Nane wa Bunge la Jamhuri uliomalizika hivi karibuni Dodoma, Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe alitangaza kukataza ‘uchimbaji dawa’ porini ifikapo leo.

Baada ya agizo hilo, Mamlaka hiyo ilifanya kikao na wasafirishaji ili kuweka mikakati kwa pamoja juu ya utekelezaji wake ambapo maeneo ya kujisaidia yalibainishwa ili abiria wajulishwe.

Hivyo kwa mujibu wa tangazo la Sumatra kwenye vyombo vya habari jana, vituo kadhaa viliainishwa katika barabara tano kuu ambazo kwa upande wa barabara ya Dar es Salaam – Mbeya, vituo vilivyoainishwa ni vya mikoa ya Pwani, Morogoro, Iringa na Njombe.

Vituo hivyo ni Ruvu iliko hoteli inayotoa huduma hiyo bure, Chalinze kuna hoteli inahudumia kwa Sh 200; stendi kuu ya mabasi ya Msamvu huduma inatolewa kwa Sh 200 na Ruaha Mbuyuni Hoteli ya Al Jazeera inatoa huduma bure.

Kitonga, Hoteli ya Confort inahudumia bure, stendi ya Ipogoro malipo ni kati ya Sh 100 na 200, Mafinga abiria watalazimika kulipia kiasi kama hicho na Makambako malipo yatakuwa kati ya Sh 200 na 300.

Katika njia ya Dar es Salaam - Mwanza; ambapo magari yanapitia mikoa ya Pwani, Morogoro, Dodoma, Singida,Tabora na Shinyanga, ‘dawa itachimbwa’ Msamvu, Gairo kuna hoteli ambayo inahudumia bure, Badueli umbali wa kilometa tatu kutoka Dodoma mjini pia huduma ni ya bure.

Singida mjini iliko stendi ya mabasi huduma hiyo pia itapatikana kwa malipo ya Sh 200, kituo cha mabasi Nzega mjini huduma italipiwa Sh 200 na katika stendi kuu mjini Tabora malipo ni Sh 200 pia.

Katika stendi kuu ya mabasi Shinyanga mjini, huduma hiyo italipiwa Sh 200 na kwa waendao Kagera kupitia Kahama huduma itapatikana stendi kuu ya mabasi kwa kati ya Sh 200 na 300 huku Mwanza mjini katika stendi kuu ya mabasi pia huduma italipiwa Sh 200.

Kwa waendao Kagera baada ya kutoka Kahama, huduma zitapatikana Ushirombo kwa Sh 100 na Sh 500 ambapo pia watapata fursa ya kuoga, Chato Sh 200, Muleba Sh 200 na Bukoba Sh 200.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, kwa abiria watokao Kigoma kabla ya kufika Kahama watahudumiwa Kasulu kwa Sh 200, Kibondo kwa Sh 200 na Runzewe kwa Sh 200 pia.

Upande wa njia ya Dar es Salaam -Tanga, abiria watahudumiwa katika kituo cha mizani Msata bila gharama yoyote sawa na Segera.

Kwa njia ya Dar es Salaam - Moshi, Arusha na Manyara, huduma zitapatikana Korogwe katika hoteli mbili bila malipo na Mombo ambako pia kuna hoteli isiyotoza malipo. Lakini Same, Mwanga, Himo, Moshi Mjini na Boma Ng’ombe, huduma itatolewa kwa Sh 200 na Arusha huduma itapatikana stendi kuu kwa Sh 200 sawa na ilivyo kwa Manyara.

Njia ya Dar es Salaam-Lindi-Mtwara, eneo la Nangurukuru kuna hoteli iitwayo StarCom ambayo itatoa huduma bila malipo, ambapo Lindi huduma hiyo haitalipiwa huku Mtwara ikilipiwa Sh 200 ingawa haitoshelezi mahitaji.

Hata hivyo, taarifa hiyo haikusema lolote kuhusu watoto na wale ambao wana matatizo ya kupata haja ndogo kila baada ya muda mfupi.

Vituo vya ‘kuchimba dawa kwa abiria wa mabasi vyatangazwa



ABIRIA wa mabasi yaendayo mikoani kuanzia kesho watalazimika kuwa na fedha za ziada mifukoni kwa ajili ya kulipia huduma ya choo.

Fedha hizo zitatumiwa kulipia huduma hiyo baada ya Serikali kupitia Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini(Sumatra), kutangaza rasmi kwamba utaratibu wa abiria kushuka maporini na kujisaidia imepigwa marufuku.

Katika Mkutano wa Nane wa Bunge la Jamhuri uliomalizika hivi karibuni Dodoma, Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe alitangaza kukataza ‘uchimbaji dawa’ porini ifikapo leo.

Baada ya agizo hilo, Mamlaka hiyo ilifanya kikao na wasafirishaji ili kuweka mikakati kwa pamoja juu ya utekelezaji wake ambapo maeneo ya kujisaidia yalibainishwa ili abiria wajulishwe.

Hivyo kwa mujibu wa tangazo la Sumatra kwenye vyombo vya habari jana, vituo kadhaa viliainishwa katika barabara tano kuu ambazo kwa upande wa barabara ya Dar es Salaam – Mbeya, vituo vilivyoainishwa ni vya mikoa ya Pwani, Morogoro, Iringa na Njombe.

Vituo hivyo ni Ruvu iliko hoteli inayotoa huduma hiyo bure, Chalinze kuna hoteli inahudumia kwa Sh 200; stendi kuu ya mabasi ya Msamvu huduma inatolewa kwa Sh 200 na Ruaha Mbuyuni Hoteli ya Al Jazeera inatoa huduma bure.

Kitonga, Hoteli ya Confort inahudumia bure, stendi ya Ipogoro malipo ni kati ya Sh 100 na 200, Mafinga abiria watalazimika kulipia kiasi kama hicho na Makambako malipo yatakuwa kati ya Sh 200 na 300.

Katika njia ya Dar es Salaam - Mwanza; ambapo magari yanapitia mikoa ya Pwani, Morogoro, Dodoma, Singida,Tabora na Shinyanga, ‘dawa itachimbwa’ Msamvu, Gairo kuna hoteli ambayo inahudumia bure, Badueli umbali wa kilometa tatu kutoka Dodoma mjini pia huduma ni ya bure.

Singida mjini iliko stendi ya mabasi huduma hiyo pia itapatikana kwa malipo ya Sh 200, kituo cha mabasi Nzega mjini huduma italipiwa Sh 200 na katika stendi kuu mjini Tabora malipo ni Sh 200 pia.

Katika stendi kuu ya mabasi Shinyanga mjini, huduma hiyo italipiwa Sh 200 na kwa waendao Kagera kupitia Kahama huduma itapatikana stendi kuu ya mabasi kwa kati ya Sh 200 na 300 huku Mwanza mjini katika stendi kuu ya mabasi pia huduma italipiwa Sh 200.

Kwa waendao Kagera baada ya kutoka Kahama, huduma zitapatikana Ushirombo kwa Sh 100 na Sh 500 ambapo pia watapata fursa ya kuoga, Chato Sh 200, Muleba Sh 200 na Bukoba Sh 200.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, kwa abiria watokao Kigoma kabla ya kufika Kahama watahudumiwa Kasulu kwa Sh 200, Kibondo kwa Sh 200 na Runzewe kwa Sh 200 pia.

Upande wa njia ya Dar es Salaam -Tanga, abiria watahudumiwa katika kituo cha mizani Msata bila gharama yoyote sawa na Segera.

Kwa njia ya Dar es Salaam - Moshi, Arusha na Manyara, huduma zitapatikana Korogwe katika hoteli mbili bila malipo na Mombo ambako pia kuna hoteli isiyotoza malipo. Lakini Same, Mwanga, Himo, Moshi Mjini na Boma Ng’ombe, huduma itatolewa kwa Sh 200 na Arusha huduma itapatikana stendi kuu kwa Sh 200 sawa na ilivyo kwa Manyara.

Njia ya Dar es Salaam-Lindi-Mtwara, eneo la Nangurukuru kuna hoteli iitwayo StarCom ambayo itatoa huduma bila malipo, ambapo Lindi huduma hiyo haitalipiwa huku Mtwara ikilipiwa Sh 200 ingawa haitoshelezi mahitaji.

Hata hivyo, taarifa hiyo haikusema lolote kuhusu watoto na wale ambao wana matatizo ya kupata haja ndogo kila baada ya muda mfupi.

Hawa Ngulume afariki dunia



ALIYEKUWA Mkuu wa Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya, Hawa Ngulume amefariki dunia jana asubuhi katika Hospitali Kuu ya Jeshi Lugalo jijini Dar es Salaam, kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa saratani ya mapafu kwa muda mrefu.

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Jordan Rugimbana, alithibitisha kutokea kwa msiba huo, na kufafanua kuwa msiba uko nyumbani kwa marehemu Goba jijini Dar es Salaam.

“Ni kweli tumepokea kwa masikitiko taarifa ya msiba wa Mheshimiwa Ngulume, ila bado hatujajua sababu ya kifo hicho, tunasubiri taarifa ya madaktari wa Lugalo ambako alilazwa kwa muda wa wiki nzima,” alisema DC Rugimbana.

Hata hivyo, kwa mujibu wa Msemaji wa familia hiyo, Alhaji Mwenza, Ngulume alifariki jana saa 4.25 asubuhi ambako alikuwa akitibiwa ugonjwa wa saratani ya mapafu.

Alisema kwa mujibu wa taarifa za awali alizokuwa nazo marehemu, ilikuwa azikwe leo saa saba mara baada ya sala ya Ijumaa nyumbani kwake Goba, lakini baadaye ratiba ilibadilika na leo anatarajiwa kusafirishwa kijijini kwao Kintiko mkoani Singida.

“Kwa mujibu wa watoto wake, kesho (leo) atasafirishwa kupelekwa Singida katika Tarafa ya Kintiko ambako anatarajiwa kuzikwa keshokutwa (kesho) kama mambo yote yataenda sawa,” alisema Mwenza.

Ngulume wakati wa uhai wake aliwahi kushika nyadhifa mbalimbali ikiwamo ukuu wa wilaya katika wilaya za Kinondoni, Singida, Bagamoyo na Mbarali alikostaafu wadhifa huo Mei mwaka huu.

Ameacha watoto wawili na wajukuu watano. Katika hatua nyingine, Rais Jakaya Kikwete ametuma salamu za rambirambi kwa familia ya Ngulume.

Alisema jana kuwa Ngulume, enzi za uhai wake, alikuwa kiongozi shupavu aliyesimamia uamuzi wake katika majukumu muhimu ya kitaifa kwa lengo la kuletea wananchi maendeleo sehemu zote alizotumikia.

“Nilimfahamu marehemu, enzi za uhai wake, akiwa kiongozi mwanamke shupavu aliyesimamia kikamilifu uamuzi wake na hivyo kuthibitisha ukweli, kwamba wanawake wakipewa fursa wanaweza,” alisema Rais Kikwete.

“Kutokana na msiba huo mkubwa, natuma salamu za rambirambi kutoka dhati ya moyo wangu kwa familia ya marehemu, Hawa Ngulume kwa kuondokewa na mhimili muhimu na kiongozi wa familia.

“Natambua machungu mliyonayo hivi sasa kwa kumpoteza mama wa familia, lakini nawahakikishieni kuwa niko pamoja nanyi katika kuomboleza msiba huu mkubwa,” aliongeza Rais Kikwete.

Hawa Ngulume afariki dunia



ALIYEKUWA Mkuu wa Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya, Hawa Ngulume amefariki dunia jana asubuhi katika Hospitali Kuu ya Jeshi Lugalo jijini Dar es Salaam, kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa saratani ya mapafu kwa muda mrefu.

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Jordan Rugimbana, alithibitisha kutokea kwa msiba huo, na kufafanua kuwa msiba uko nyumbani kwa marehemu Goba jijini Dar es Salaam.

“Ni kweli tumepokea kwa masikitiko taarifa ya msiba wa Mheshimiwa Ngulume, ila bado hatujajua sababu ya kifo hicho, tunasubiri taarifa ya madaktari wa Lugalo ambako alilazwa kwa muda wa wiki nzima,” alisema DC Rugimbana.

Hata hivyo, kwa mujibu wa Msemaji wa familia hiyo, Alhaji Mwenza, Ngulume alifariki jana saa 4.25 asubuhi ambako alikuwa akitibiwa ugonjwa wa saratani ya mapafu.

Alisema kwa mujibu wa taarifa za awali alizokuwa nazo marehemu, ilikuwa azikwe leo saa saba mara baada ya sala ya Ijumaa nyumbani kwake Goba, lakini baadaye ratiba ilibadilika na leo anatarajiwa kusafirishwa kijijini kwao Kintiko mkoani Singida.

“Kwa mujibu wa watoto wake, kesho (leo) atasafirishwa kupelekwa Singida katika Tarafa ya Kintiko ambako anatarajiwa kuzikwa keshokutwa (kesho) kama mambo yote yataenda sawa,” alisema Mwenza.

Ngulume wakati wa uhai wake aliwahi kushika nyadhifa mbalimbali ikiwamo ukuu wa wilaya katika wilaya za Kinondoni, Singida, Bagamoyo na Mbarali alikostaafu wadhifa huo Mei mwaka huu.

Ameacha watoto wawili na wajukuu watano. Katika hatua nyingine, Rais Jakaya Kikwete ametuma salamu za rambirambi kwa familia ya Ngulume.

Alisema jana kuwa Ngulume, enzi za uhai wake, alikuwa kiongozi shupavu aliyesimamia uamuzi wake katika majukumu muhimu ya kitaifa kwa lengo la kuletea wananchi maendeleo sehemu zote alizotumikia.

“Nilimfahamu marehemu, enzi za uhai wake, akiwa kiongozi mwanamke shupavu aliyesimamia kikamilifu uamuzi wake na hivyo kuthibitisha ukweli, kwamba wanawake wakipewa fursa wanaweza,” alisema Rais Kikwete.

“Kutokana na msiba huo mkubwa, natuma salamu za rambirambi kutoka dhati ya moyo wangu kwa familia ya marehemu, Hawa Ngulume kwa kuondokewa na mhimili muhimu na kiongozi wa familia.

“Natambua machungu mliyonayo hivi sasa kwa kumpoteza mama wa familia, lakini nawahakikishieni kuwa niko pamoja nanyi katika kuomboleza msiba huu mkubwa,” aliongeza Rais Kikwete.

Bashe, Kigwangallah katika vita ya bastola

BASHE AMTUHUMU KIGWANGALLAH KUMTISHA KWA SILAHA,NAYE AENDA POLISI KUWATUHUMU WAFUASI WA BASHE KUMTISHA

VITA ya mahasimu wa siku nyingi katika siasa wilayani Nzega, Hussein Bashe na Dk Hamis Kigwangallah imechukua sura mpya, baada ya makada hao wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kufikia hatua ya kutishiana kwa bastola hadharani.Hata hivyo, pamoja na taarifa hizo kuthibitishwa na viongozi wa CCM wilayani humo na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Bashe na Kigwangallah kwa nyakati tofauti kila mmoja amekanusha madai hayo akimtuhumu mwenzake kuwa ndiye aliyekuwa na silaha.

Wakati Bashe akisema Dk Kigwangallah ambaye pia ni mbunge wa Nzega ndiye aliyetoa bastola kumstishia wakiwa ndani ya ofisi ya ya CCM Wilaya, Dk Kigwangallah anaeleza kuwa walinzi wa Bashe ndio waliomtishia yeye bastola na kwamba tayari amelifikisha suala hilo polisi ambao wanalifanyia kazi.

Habari zilizolifikia gazeti hili zilieleza kuwa, Dk Kigwangallah na Bashe walizua tafrani hiyo juzi wakati wakirejesha fomu za kuwania nafasi ya ujumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (Nec) kupitia Wilaya ya Nzega.

Upinzani baina ya wanasiasa hao vijana, ulianza 2010 baada ya Kigwangallah kupitishwa na CCM kugombea ubunge katika jimbo hilo licha ya kushika nafasi ya tatu katika kura za maoni, ndani ya chama hicho.

Bashe ambaye aliibuka kidedea katika mchakato huo wa kura za maoni alitoswa na chama hicho kwa maelezo kuwa hakuwa raia wa Tanzania, huku aliyeshika nafasi ya pili, Lucas Selelii ambaye alikuwa kinara wa kupambana na mafisadi wa chama hicho naye akitoswa. Baadaye Waziri wa Mambo ya Ndani wa wakati huo, Lawrence Masha alisema Bashe alikuwa raia halali wa Tanzania.

Vita hiyo ilionekana kuendelea juzi baada ya kudaiwa kutishiana bastola huku kila mmoja akitoa maelezo ya kumrushia lawama mwenzake.

Ilivyokuwa
Katibu wa CCM Wilaya ya Nzega, Kajoro Vyehoroka alisema Bashe alifika ofisini hapo kurejesha fomu saa 09:50 alasiri, muda mfupi baada ya Dk Kigwangallah ambaye alifika saa 09:48.

“Kigwangala alifika na kuingia ofisi ya Mwenyekiti wa CCM Wilaya, Fransis Shija, ambako alikaa na kujaza fomu yake. Bashe naye alifika akaingia ofisini kwangu, akakaa na kuandika," alisema.

Katibu huyo aliendelea kueleza kuwa ilipofika saa 9:55, Dk Kigwangallah alikwenda kwa katibu muhutasi kurejesha fomu yake na kukaa hapo.

"Bashe alipofika hapo naye alisimama akingoja Kigwangallah amalize, lakini Kigwangallah alimueleza kuwa muda wa kurejesha fomu umemalizika, hivyo kumzuia kurudisha fomu, hali iliyozua mvutano na vurugu" alieleza katibu huyo.

Katibu wa Vijana wa CCM Wilayani Nzega, Salome Nyombi, alisema baada ya vurugu hizo kuzuiliwa ndani ya ofisi ya katibu, Bashe alitolewa nje ambako alianza kuwasimulia rafiki zake kilichotokea ndani.

Alisema baadaye Kigwangallah naye alifa eneo hilo na kuanza kurusha maneno, hali iliyozua mtafaruku mwingine katika eneo hilo.

"Alipozuiliwa kufanya vurugu, aliendelea kutukana na kisha kutoa bastola akiwatishia watu waliokuwa wakizungumza na Bashe kwa madai kuwa ni vibaraka wake," alisema na kuongeza:

“Hali ilikuwa mbaya kiasi cha baadhi yetu kulazimika kukimbia, na wengine tulilala kwenye viti, lakini kijana mmoja anayeitwa Sango, alimzuia (Kigwangallah) kwa kujaribu kumpiga kwa kiti, ndipo watu walipomtoa Bashe na kumpeleka eneo lingine.”

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake wilayani Nzega, Mary Igogo, alisema amesikitishwa na vurugu hizo na kusema iwapo wasingemzuia Bashe, kungezuka ugomvi mkubwa.

Katibu CCM mkoa
Katibu CCM Mkoa wa Tabora, Iddi Ame akizungumuza kwa simu, alisema ndani ya CCM ni ajabu kwa wanachama kutishina kwa silaha.

Ame alisema kuwa kitendo hicho ni aibu kubwa kwa CCM huku akiuagiza uongozi wa Wilaya ya Nzega kutoa maamuzi mapema juu ya vurugu za makada hao.

“CCM hatuna historia ya kutishana kwa bastola na kamwe jambo hilo haliwezi kuwa siasa kwa kuwa linaleta sura mbaya ndani ya chama chetu, nawaagiza uongozi wa wilaya watoe tamko au maamuzi ya jambo hili mapema,”Ame.

Shuhuda
Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo ambaye jina lake halikufahamika mara moja, alisema vurugu zilikuwa kubwa zaidi nje ya ofisi za CCM baada ya mahasimu hao kutolewa ndani ya ofisi hizo baada ya kuanza kulumbana.

Taarifa kutoka Jeshi la Polisi zilieleza kuwa Kigwangallah alifika katika kituo cha polisi na kufungua malalamiko ya kutishiwa maisha na Sango Issaya, Hussein Bashe pamoja na Majaliwa Bilali.

Taarifa hizo zilifafanua kwamba kwa nyakati tofauti mahasimu hao walitoa maelezo yao polisi na wapo nje kwa dhamana mpaka pale upelelezi wa tuhuma walizopeana utakapokamilika.

"Tumepokea taarifa za hawa watu na tunaendelea na upelelezi wetu mpaka hapo tutakapojiridhisha na ushahidi ndipo tutawapeleka mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili,”alisema ofisa mmoja wa polisi wa ngazi za juu wilaya.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Antony Rutta, aliliambia gazeti hili kuwa taarifa za tukio hilo alizipata, lakini anaendelea kuzifuatilia kujua chanzo chake.

“Ni kweli nimepata taarifa za Bashe na Kigwangallah wamedaiwa kutishiana bastola…mimi nilisikia hayo nikiwa njiani kutoka huko Nzega kurudi Tabora….nitafuatilia,”alisema.

Kauli za Bashe, Kigwangallah
Bashe alikiri kutokea vurugu hizo, lakini akakanusha kumtishia bastola Dk Kigwangallah akidai kuwa mwenzake huyo ndiye aliyemtishia yeye kwa bastola akitaka fomu yake isipokelewe kwa kile alichoeleza kuwa imechelewa kurejeshwa.

“Huyu ndugu yangu ana visa na chuki dhidi yangu, ni kweli alinichomolea bastola, lakini wanachama walituamulia," alisema

Hata hivyo, Bashe alieleza kuwa pamoja na hila hizo, Dk Kigwangallah hamuwezi kisiasa kwani katika chaguzi zote zilizowahi kufanyika zikiwahusisha wao, amekuwa akimshinda kwa kishindo.

"Kigwangallah pia aliwahi kuvamia mkutano wangu, lakini niliwaambia watu wangu wamwache. Anachotafuta ni confrontation (msuguano) na mimi ili kutokee tatizo nienguliwe kwenye uchaguzi baada ya kuona haniwezi," alisema.

Bashe alisema kwamba amegundua Kigwangallah anatumia mbinu ili majina yao yakatwe yote kwa kuwa ameshaona hawezi kumshinda. “Jamani Kigwangallah hawezi kunishinda, amenitishia na bastola nikakaa kimya, sikupenda kabisa kumjibu maana najua anachotafuta,” alisema

Kwa upande wake, Dk Kigwangallah alisema aliomba Bashe azuiwe kurejesha fomu yake kwa kuwa aliirudisha nje ya muda, lakini alishangaa kuona anafanyiwa vurugu na wafuasi wake.

Alisema alitishiwa maisha na watu watatu ambao aliwataja akiwamo Bashe na kueleza kuwa tayari malalamiko hayo ameyafikisha polisi.

"Walinzi wa Bashe ndio walionitishia bastola na baada ya tukio hilo nikaenda kuripoti polisi na tayari polisi wamechukua hatua ikiwamo kuwafikisha mahakamani Bashe na wapambe wake hao," alisema Dk Kigwangallah na kuongeza;

“Huyu ndugu yangu (Bashe) ni mzushi anataka kuyakuza mambo tu. Katika hilo Katibu amembeba kwani muda wa kurejesha fomu ulikuwa umeisha".
Alisema Bashe amekuwa akijaribu kumfanyia faulo ya kumtishia huku akitembea na jopo la waandishi wa habari ili wamchafue.

’’Nimeamua kuja kutoa taarifa kwani nimetishiwa maisha yangu na kijana huyu pamoja na Bashe lazima nitoe taarifa hizi, maana nimeonewa,’’alisema Kigwangallah.

Alipoulizwa kana anamiliki bastola, Kigwangallah alisema kuwa kwa muda mrefu amekuwa akimiliki silaha hiyo.

“Kama ningeamua kuua ningeweza kufanya hivyo ila naelewa maana ya kuwa na silaha ya moto, ndio maana nimekuja hapa kutoa taarifa kwa sababu lolote linaweza kutokea” alisema mbunge huyo wakati akiwa Kituo cha Polisi Nzega.

Zungu amkacha Mkono
Katika hatua nyingine mbunge wa Ilala, Mussa Azzan Zungu ameshindwa kurudisha fomu ya kuwania nafasi ya uenyekiti wa Wazazi Taifa.

Siku ya mwisho ya kurejesha fomu ilikuwa juzi, lakini mbunge huyo ambaye pia ni mwenyekiti wa Bunge alishindwa kuirejesha kama walivyofanya wagombea wengine 16 akiwemo Mbunge wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono.

Bashe, Kigwangallah katika vita ya bastola

BASHE AMTUHUMU KIGWANGALLAH KUMTISHA KWA SILAHA,NAYE AENDA POLISI KUWATUHUMU WAFUASI WA BASHE KUMTISHA

VITA ya mahasimu wa siku nyingi katika siasa wilayani Nzega, Hussein Bashe na Dk Hamis Kigwangallah imechukua sura mpya, baada ya makada hao wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kufikia hatua ya kutishiana kwa bastola hadharani.Hata hivyo, pamoja na taarifa hizo kuthibitishwa na viongozi wa CCM wilayani humo na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Bashe na Kigwangallah kwa nyakati tofauti kila mmoja amekanusha madai hayo akimtuhumu mwenzake kuwa ndiye aliyekuwa na silaha.

Wakati Bashe akisema Dk Kigwangallah ambaye pia ni mbunge wa Nzega ndiye aliyetoa bastola kumstishia wakiwa ndani ya ofisi ya ya CCM Wilaya, Dk Kigwangallah anaeleza kuwa walinzi wa Bashe ndio waliomtishia yeye bastola na kwamba tayari amelifikisha suala hilo polisi ambao wanalifanyia kazi.

Habari zilizolifikia gazeti hili zilieleza kuwa, Dk Kigwangallah na Bashe walizua tafrani hiyo juzi wakati wakirejesha fomu za kuwania nafasi ya ujumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (Nec) kupitia Wilaya ya Nzega.

Upinzani baina ya wanasiasa hao vijana, ulianza 2010 baada ya Kigwangallah kupitishwa na CCM kugombea ubunge katika jimbo hilo licha ya kushika nafasi ya tatu katika kura za maoni, ndani ya chama hicho.

Bashe ambaye aliibuka kidedea katika mchakato huo wa kura za maoni alitoswa na chama hicho kwa maelezo kuwa hakuwa raia wa Tanzania, huku aliyeshika nafasi ya pili, Lucas Selelii ambaye alikuwa kinara wa kupambana na mafisadi wa chama hicho naye akitoswa. Baadaye Waziri wa Mambo ya Ndani wa wakati huo, Lawrence Masha alisema Bashe alikuwa raia halali wa Tanzania.

Vita hiyo ilionekana kuendelea juzi baada ya kudaiwa kutishiana bastola huku kila mmoja akitoa maelezo ya kumrushia lawama mwenzake.

Ilivyokuwa
Katibu wa CCM Wilaya ya Nzega, Kajoro Vyehoroka alisema Bashe alifika ofisini hapo kurejesha fomu saa 09:50 alasiri, muda mfupi baada ya Dk Kigwangallah ambaye alifika saa 09:48.

“Kigwangala alifika na kuingia ofisi ya Mwenyekiti wa CCM Wilaya, Fransis Shija, ambako alikaa na kujaza fomu yake. Bashe naye alifika akaingia ofisini kwangu, akakaa na kuandika," alisema.

Katibu huyo aliendelea kueleza kuwa ilipofika saa 9:55, Dk Kigwangallah alikwenda kwa katibu muhutasi kurejesha fomu yake na kukaa hapo.

"Bashe alipofika hapo naye alisimama akingoja Kigwangallah amalize, lakini Kigwangallah alimueleza kuwa muda wa kurejesha fomu umemalizika, hivyo kumzuia kurudisha fomu, hali iliyozua mvutano na vurugu" alieleza katibu huyo.

Katibu wa Vijana wa CCM Wilayani Nzega, Salome Nyombi, alisema baada ya vurugu hizo kuzuiliwa ndani ya ofisi ya katibu, Bashe alitolewa nje ambako alianza kuwasimulia rafiki zake kilichotokea ndani.

Alisema baadaye Kigwangallah naye alifa eneo hilo na kuanza kurusha maneno, hali iliyozua mtafaruku mwingine katika eneo hilo.

"Alipozuiliwa kufanya vurugu, aliendelea kutukana na kisha kutoa bastola akiwatishia watu waliokuwa wakizungumza na Bashe kwa madai kuwa ni vibaraka wake," alisema na kuongeza:

“Hali ilikuwa mbaya kiasi cha baadhi yetu kulazimika kukimbia, na wengine tulilala kwenye viti, lakini kijana mmoja anayeitwa Sango, alimzuia (Kigwangallah) kwa kujaribu kumpiga kwa kiti, ndipo watu walipomtoa Bashe na kumpeleka eneo lingine.”

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake wilayani Nzega, Mary Igogo, alisema amesikitishwa na vurugu hizo na kusema iwapo wasingemzuia Bashe, kungezuka ugomvi mkubwa.

Katibu CCM mkoa
Katibu CCM Mkoa wa Tabora, Iddi Ame akizungumuza kwa simu, alisema ndani ya CCM ni ajabu kwa wanachama kutishina kwa silaha.

Ame alisema kuwa kitendo hicho ni aibu kubwa kwa CCM huku akiuagiza uongozi wa Wilaya ya Nzega kutoa maamuzi mapema juu ya vurugu za makada hao.

“CCM hatuna historia ya kutishana kwa bastola na kamwe jambo hilo haliwezi kuwa siasa kwa kuwa linaleta sura mbaya ndani ya chama chetu, nawaagiza uongozi wa wilaya watoe tamko au maamuzi ya jambo hili mapema,”Ame.

Shuhuda
Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo ambaye jina lake halikufahamika mara moja, alisema vurugu zilikuwa kubwa zaidi nje ya ofisi za CCM baada ya mahasimu hao kutolewa ndani ya ofisi hizo baada ya kuanza kulumbana.

Taarifa kutoka Jeshi la Polisi zilieleza kuwa Kigwangallah alifika katika kituo cha polisi na kufungua malalamiko ya kutishiwa maisha na Sango Issaya, Hussein Bashe pamoja na Majaliwa Bilali.

Taarifa hizo zilifafanua kwamba kwa nyakati tofauti mahasimu hao walitoa maelezo yao polisi na wapo nje kwa dhamana mpaka pale upelelezi wa tuhuma walizopeana utakapokamilika.

"Tumepokea taarifa za hawa watu na tunaendelea na upelelezi wetu mpaka hapo tutakapojiridhisha na ushahidi ndipo tutawapeleka mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili,”alisema ofisa mmoja wa polisi wa ngazi za juu wilaya.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Antony Rutta, aliliambia gazeti hili kuwa taarifa za tukio hilo alizipata, lakini anaendelea kuzifuatilia kujua chanzo chake.

“Ni kweli nimepata taarifa za Bashe na Kigwangallah wamedaiwa kutishiana bastola…mimi nilisikia hayo nikiwa njiani kutoka huko Nzega kurudi Tabora….nitafuatilia,”alisema.

Kauli za Bashe, Kigwangallah
Bashe alikiri kutokea vurugu hizo, lakini akakanusha kumtishia bastola Dk Kigwangallah akidai kuwa mwenzake huyo ndiye aliyemtishia yeye kwa bastola akitaka fomu yake isipokelewe kwa kile alichoeleza kuwa imechelewa kurejeshwa.

“Huyu ndugu yangu ana visa na chuki dhidi yangu, ni kweli alinichomolea bastola, lakini wanachama walituamulia," alisema

Hata hivyo, Bashe alieleza kuwa pamoja na hila hizo, Dk Kigwangallah hamuwezi kisiasa kwani katika chaguzi zote zilizowahi kufanyika zikiwahusisha wao, amekuwa akimshinda kwa kishindo.

"Kigwangallah pia aliwahi kuvamia mkutano wangu, lakini niliwaambia watu wangu wamwache. Anachotafuta ni confrontation (msuguano) na mimi ili kutokee tatizo nienguliwe kwenye uchaguzi baada ya kuona haniwezi," alisema.

Bashe alisema kwamba amegundua Kigwangallah anatumia mbinu ili majina yao yakatwe yote kwa kuwa ameshaona hawezi kumshinda. “Jamani Kigwangallah hawezi kunishinda, amenitishia na bastola nikakaa kimya, sikupenda kabisa kumjibu maana najua anachotafuta,” alisema

Kwa upande wake, Dk Kigwangallah alisema aliomba Bashe azuiwe kurejesha fomu yake kwa kuwa aliirudisha nje ya muda, lakini alishangaa kuona anafanyiwa vurugu na wafuasi wake.

Alisema alitishiwa maisha na watu watatu ambao aliwataja akiwamo Bashe na kueleza kuwa tayari malalamiko hayo ameyafikisha polisi.

"Walinzi wa Bashe ndio walionitishia bastola na baada ya tukio hilo nikaenda kuripoti polisi na tayari polisi wamechukua hatua ikiwamo kuwafikisha mahakamani Bashe na wapambe wake hao," alisema Dk Kigwangallah na kuongeza;

“Huyu ndugu yangu (Bashe) ni mzushi anataka kuyakuza mambo tu. Katika hilo Katibu amembeba kwani muda wa kurejesha fomu ulikuwa umeisha".
Alisema Bashe amekuwa akijaribu kumfanyia faulo ya kumtishia huku akitembea na jopo la waandishi wa habari ili wamchafue.

’’Nimeamua kuja kutoa taarifa kwani nimetishiwa maisha yangu na kijana huyu pamoja na Bashe lazima nitoe taarifa hizi, maana nimeonewa,’’alisema Kigwangallah.

Alipoulizwa kana anamiliki bastola, Kigwangallah alisema kuwa kwa muda mrefu amekuwa akimiliki silaha hiyo.

“Kama ningeamua kuua ningeweza kufanya hivyo ila naelewa maana ya kuwa na silaha ya moto, ndio maana nimekuja hapa kutoa taarifa kwa sababu lolote linaweza kutokea” alisema mbunge huyo wakati akiwa Kituo cha Polisi Nzega.

Zungu amkacha Mkono
Katika hatua nyingine mbunge wa Ilala, Mussa Azzan Zungu ameshindwa kurudisha fomu ya kuwania nafasi ya uenyekiti wa Wazazi Taifa.

Siku ya mwisho ya kurejesha fomu ilikuwa juzi, lakini mbunge huyo ambaye pia ni mwenyekiti wa Bunge alishindwa kuirejesha kama walivyofanya wagombea wengine 16 akiwemo Mbunge wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono.

Dk. Slaa amvutia pumzi Sitta


KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, amesema anamvutia pumzi Spika mstaafu wa Bunge, Samuel Sitta, juu ya kauli yake kuwa chama hicho hakina viongozi wa kutosha kufanya kazi ya serikali.

Sitta ambaye pia ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki na mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, alitoa kauli hiyo juzi wilayani Karagwe, Mkoa wa Kagera, alipotembelea ofisi za chama chake, akisema CHADEMA haina kiongozi zaidi ya Dk. Slaa.

Sitta alikwenda mbali zaidi akisema kuwa CHADEMA ina viongozi wenye uzoefu wa kuongoza kumbi za muziki na kwamba Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, ni mjuzi wa disko za usiku.

Akizungumza na Tanzania Daima mjini Iringa jana, akiwa katika mwendelezo wa Operesheni ya Vuguvugu la Mabadiliko (M4C), Dk. Slaa, alisema tuhuma hizo ni nzito na lazima azipitie kwa umakini ili aweze kuzitolea maelezo.

“Nimesoma juu ya hizo taarifa na kama Sitta ninayemheshimu, amefikia kumuita mwenyekiti wetu mtaalamu wa kuongoza disko, si kauli nyepesi, hiyo ngoja tuichambue na leo au kesho tutatoa tamko zito juu ya hilo,” alisema Dk. Slaa.

Aliongeza kuwa Sitta ambaye ni Mbunge wa Urambo Mashariki alitoa kauli hiyo akiwa katika jukwaa la siasa, hivyo naye anatafakari kama amjibu akiwa jukwaani au aitishe mkutano na waandishi wa habari.

Polisi waikaribisha M4C

Katika hatua nyingine, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Kamishna Mwandamizi Msaidizi wa Polisi (SACP), Michael Kamuhanda, amesema hawatakuwa na sababu ya kuzuia mikutano ya CHADEMA baada ya shughuli za sensa kumalizika.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamuhanda alisema tangu siku ya kwanza CHADEMA walipoingia mkoani humo hali ya utulivu ilikuwa ni nzuri na hakukuwa na matatizo yoyote mabaya waliyosababisha.

“Tunajua watafanya mkutano wao Septemba 2, mwaka huu, wilayani Mufindi, hatuna sababu ya kuzuia hilo labda ijitokeza sababu ya kiusalama, kwa kuwa hata Dk. Slaa nimezungumza naye na akaniambia wako salama na amefurahia walivyopokewa kifalme katika mkoa huu,” alisema Kamuhanda.

Akizungumzia sababu ya kuimarisha ulinzi, Kamanda Kamuhanda alisema hatua hiyo inatokana na hali halisi ya kisiasa kwa sasa na kwamba polisi wana wajibu wa kuchukua tahadhari kuhakikisha usalama unakuwepo.

Alipoulizwa kama jeshi hilo linatumiwa na viongozi wa CCM katika kuhakikisha mikutano ya CHADEMA haifanikiwi, Kamuhanda alisema si kweli kwani hata baadhi ya viongozi wa CCM wakiwamo wabunge wa mkoa huo hajawahi kukutana nao.

Tangu kuingia kwa viongozi kadhaa wa CHADEMA mkoani Iringa, jeshi hilo limekuwa katika tahadhari kubwa kwa hofu kuwa wanaweza kufanya mikutano kabla ya sensa ya watu na makazi kumalizika.

 



Dk. Slaa amvutia pumzi Sitta


KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, amesema anamvutia pumzi Spika mstaafu wa Bunge, Samuel Sitta, juu ya kauli yake kuwa chama hicho hakina viongozi wa kutosha kufanya kazi ya serikali.

Sitta ambaye pia ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki na mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, alitoa kauli hiyo juzi wilayani Karagwe, Mkoa wa Kagera, alipotembelea ofisi za chama chake, akisema CHADEMA haina kiongozi zaidi ya Dk. Slaa.

Sitta alikwenda mbali zaidi akisema kuwa CHADEMA ina viongozi wenye uzoefu wa kuongoza kumbi za muziki na kwamba Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, ni mjuzi wa disko za usiku.

Akizungumza na Tanzania Daima mjini Iringa jana, akiwa katika mwendelezo wa Operesheni ya Vuguvugu la Mabadiliko (M4C), Dk. Slaa, alisema tuhuma hizo ni nzito na lazima azipitie kwa umakini ili aweze kuzitolea maelezo.

“Nimesoma juu ya hizo taarifa na kama Sitta ninayemheshimu, amefikia kumuita mwenyekiti wetu mtaalamu wa kuongoza disko, si kauli nyepesi, hiyo ngoja tuichambue na leo au kesho tutatoa tamko zito juu ya hilo,” alisema Dk. Slaa.

Aliongeza kuwa Sitta ambaye ni Mbunge wa Urambo Mashariki alitoa kauli hiyo akiwa katika jukwaa la siasa, hivyo naye anatafakari kama amjibu akiwa jukwaani au aitishe mkutano na waandishi wa habari.

Polisi waikaribisha M4C

Katika hatua nyingine, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Kamishna Mwandamizi Msaidizi wa Polisi (SACP), Michael Kamuhanda, amesema hawatakuwa na sababu ya kuzuia mikutano ya CHADEMA baada ya shughuli za sensa kumalizika.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamuhanda alisema tangu siku ya kwanza CHADEMA walipoingia mkoani humo hali ya utulivu ilikuwa ni nzuri na hakukuwa na matatizo yoyote mabaya waliyosababisha.

“Tunajua watafanya mkutano wao Septemba 2, mwaka huu, wilayani Mufindi, hatuna sababu ya kuzuia hilo labda ijitokeza sababu ya kiusalama, kwa kuwa hata Dk. Slaa nimezungumza naye na akaniambia wako salama na amefurahia walivyopokewa kifalme katika mkoa huu,” alisema Kamuhanda.

Akizungumzia sababu ya kuimarisha ulinzi, Kamanda Kamuhanda alisema hatua hiyo inatokana na hali halisi ya kisiasa kwa sasa na kwamba polisi wana wajibu wa kuchukua tahadhari kuhakikisha usalama unakuwepo.

Alipoulizwa kama jeshi hilo linatumiwa na viongozi wa CCM katika kuhakikisha mikutano ya CHADEMA haifanikiwi, Kamuhanda alisema si kweli kwani hata baadhi ya viongozi wa CCM wakiwamo wabunge wa mkoa huo hajawahi kukutana nao.

Tangu kuingia kwa viongozi kadhaa wa CHADEMA mkoani Iringa, jeshi hilo limekuwa katika tahadhari kubwa kwa hofu kuwa wanaweza kufanya mikutano kabla ya sensa ya watu na makazi kumalizika.

 



Thursday, August 30, 2012

WAANDISHI WA HABARI SINGIDA WATAKIWA KUTOINGIZA USHABIKI KATIKA UTENDAJI WA KAZI.


Mwenyekiti wa Klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Singida (Singpress) Seif Takaza akizungumza muda mfupi kabla hajamkaribisha mkuu wa wilaya ya Iramba kufungua mkutano maalum wa klabu hiyo kwa ajili ya kurekebisha katiba yao. Kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Iramba Yahaya Nawanda.



Mkuu wa wilaya ya Iramba mkoa wa Singida Yahaya Nawanda akifungua mkutano maalum wa klabu ya waandishi wa habari (Singpress) mkoa wa Singida kwa ajili ya kuifanyia marekebisho katiba yao. Wa kwanza kulia ni makamu mwenyekiti wa Singpress Jumbe Ismael na anayefuatia ni mwenyekiti wa Singpress Seif Takaza.

Baadhi ya wanachama wa klabu ya waandishi wa habari waliohudhuria mkutano maalum wa klabu hiyo kufanya marekebisho ya katiba. Mkutano huo ulifanykia kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya wilaya ya Iramba mjini New Kiomboi.




Mkuu wa wilaya ya Iramba Yahaya Nawanda (wa pili kulia – mwenye miwani) akiwa kwenye picha ya pamoja na wananchama wa Singpress.

Mkuu wa wilaya ya Iramba mkoani Singida Yahaya Nawanda amewataka waandishi wa habari kuzingatia na kutii katiba zao kikamilifu, ili pamoja na mambo mengine, kuondoa uwezekano wa kutokea kwa migogoro inayohatarisha ustawi wa tasnia nyeti ya uandishi wa habari.


Nawanda ametoa wito huo wakati akifungua mkutano mkuu maalum wa marekebisho ya katiba ya Klabu ya waandishi wa habari mkoa wa SIngida (Singpress).

Amesema faida za kutii na kuzingatia katiba mahali popote pale, zipo nyingi ikiwemo ya kuimarisha amani na utulivu katika sehemu husika.

Aidha mkuu huyo wa wilaya amewasisitiza wahakikishe hawaendi tofauti na mabadiliko watakayoyafanya, baada ya marekebisho hayo, basi ni muhimu viongozi na wajumbe wote, mfuate kwa dhati na kuheshimu katiba yenu.

Akisisitiza zaidi, Nawanda amewataka waandishi hao wa habari, wasiingize ushabiki wa aina yo yote katika utendaji wao wa kazi za kila siku.

Nawanda amesema kazi ya uandishi wa habari sio kazi ambayo kila mtu anaweza kuifanya, ni lazima isomewe na mhusika awe na maadili.

WAANDISHI WA HABARI SINGIDA WATAKIWA KUTOINGIZA USHABIKI KATIKA UTENDAJI WA KAZI.


Mwenyekiti wa Klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Singida (Singpress) Seif Takaza akizungumza muda mfupi kabla hajamkaribisha mkuu wa wilaya ya Iramba kufungua mkutano maalum wa klabu hiyo kwa ajili ya kurekebisha katiba yao. Kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Iramba Yahaya Nawanda.



Mkuu wa wilaya ya Iramba mkoa wa Singida Yahaya Nawanda akifungua mkutano maalum wa klabu ya waandishi wa habari (Singpress) mkoa wa Singida kwa ajili ya kuifanyia marekebisho katiba yao. Wa kwanza kulia ni makamu mwenyekiti wa Singpress Jumbe Ismael na anayefuatia ni mwenyekiti wa Singpress Seif Takaza.

Baadhi ya wanachama wa klabu ya waandishi wa habari waliohudhuria mkutano maalum wa klabu hiyo kufanya marekebisho ya katiba. Mkutano huo ulifanykia kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya wilaya ya Iramba mjini New Kiomboi.




Mkuu wa wilaya ya Iramba Yahaya Nawanda (wa pili kulia – mwenye miwani) akiwa kwenye picha ya pamoja na wananchama wa Singpress.

Mkuu wa wilaya ya Iramba mkoani Singida Yahaya Nawanda amewataka waandishi wa habari kuzingatia na kutii katiba zao kikamilifu, ili pamoja na mambo mengine, kuondoa uwezekano wa kutokea kwa migogoro inayohatarisha ustawi wa tasnia nyeti ya uandishi wa habari.


Nawanda ametoa wito huo wakati akifungua mkutano mkuu maalum wa marekebisho ya katiba ya Klabu ya waandishi wa habari mkoa wa SIngida (Singpress).

Amesema faida za kutii na kuzingatia katiba mahali popote pale, zipo nyingi ikiwemo ya kuimarisha amani na utulivu katika sehemu husika.

Aidha mkuu huyo wa wilaya amewasisitiza wahakikishe hawaendi tofauti na mabadiliko watakayoyafanya, baada ya marekebisho hayo, basi ni muhimu viongozi na wajumbe wote, mfuate kwa dhati na kuheshimu katiba yenu.

Akisisitiza zaidi, Nawanda amewataka waandishi hao wa habari, wasiingize ushabiki wa aina yo yote katika utendaji wao wa kazi za kila siku.

Nawanda amesema kazi ya uandishi wa habari sio kazi ambayo kila mtu anaweza kuifanya, ni lazima isomewe na mhusika awe na maadili.

Mwisho wa kuhesabiwa sensa leo


OFISI ya Takwimu ya Taifa (NBS) imesema watu ambao watakuwa hawajahesabiwa hadi leo, wawasiliane na viongozi wao wa mitaa, vitongoji na vijiji.

Akizungumza na gazeti hili jana, Ofisa Mawasiliano na Uhamasishaji wa NBS, Said Ameir alisema ofisi yake imetenga siku tano ili watu wote wawe wamehesabiwa.

Alifafanua, kama itatokea kuna watu hawajahesabiwa, watumie siku tatu zilizobaki kuanzia leo kuhakikisha wanafanya hivyo.

Alitaka waishio mijini wawasiliane na wenyekiti wa serikali za mitaa na wanaoishi vijijini wawasiliane na wenyeviti wa vitongoji na vijiji kwa msaada zaidi.

Ameir alifafanua kuwa pamoja na kuwa makarani wa sensa watapita, swali lao litabaki lile lile kuwa ni watu wangapi walilala ndani ya kaya hiyo usiku wa kuamkia Agosti 26.

Alikumbusha wananchi wahakikishe ambao hawakulala katika nyumba hizo usiku huo, hawahesabiwi kwani watakuwa wamehesabiwa walikotoka. Kuhusu matumizi ya dodoso fupi na dodoso refu, Ameir alisema katika kaya moja ni dodoso moja tu linatumika.

“Katika kaya ambako makarani wenye dodoso fupi wamepita, mwenye refu haruhusiwi kupita na pale alipopita mwenye refu mwenye fupi haruhusiwi kupita,” alifafanua. Alisema dodoso fupi linatumika kwa asilimia 70 ya kaya zinazohesabiwa wakati refu linatumika kwa asilimia 30 tu katika eneo moja.

Aliongeza kuwa fupi lina maswali 32 wakati refu lina maswali 62. Kuhusu taarifa za upungufu wa vifaa katika baadhi ya mikoa, Ameir alisema amesikia habari hizo lakini vifaa zaidi kwenye sensa ni madodoso ambayo alisema ofisi yake imehakikisha yapo mengi katika mikoa yote ili kusiwepo na tatizo hilo.

“Sisi unaposema vifaa ina maana ni madodoso, ukiacha sare za makarani, kwa hiyo tumejiimarisha kuhakikisha hakuna upungufu wowote,” alisema ofisa huyo. Ameir alitoa mwito kwa wananchi ambao hawajahesabiwa kuvuta subira kwani nia ya Serikali ni kuhakikisha kila Mtanzania anahesabiwa. Upungufu Dodoma Hata hivyo, Dodoma, makarani wa sensa walilazimika kudurufu madodoso ili kuendelea na kazi baada ya kuishiwa. Hali hiyo ya upungufu wa vifaa ilijitokeza mapema katika maeneo ya Uwanja wa Ndege na Majengo, ambako makarani walilazimika kusitisha kazi kwa muda.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk Rehema Nchimbi alikiri upungufu huo na kusema tatizo hilo limetatuliwa kutokana na vifaa hivyo kuwasili kutoka Dar es Salaam na vilitarajiwa kusambazwa katika maeneo yenye upungufu. Alisema wilaya ya Kondoa ilikuwa na upungufu mkubwa.

Wakimbia nyumba Mkoani Dar es Salaam katika wilaya ya Kinondoni, licha ya kwamba kazi ya sensa ilifanyika vizuri kwa kiwango kikubwa, lakini zipo nyumba mbili ambazo hazijahesabiwa kutokana na wahusika kukimbia.

Mkuu wa Wilaya hiyo, Jordan Rugimbana alisema hayo alipozungumza na gazeti hili kuhusu mwenendo wa sensa katika wilaya hiyo na kuzitaja nyumba hizo kuwa zipo maeneo ya Ununio na Mtambani.

Alisema katika nyumba hizo, makarani walipofika hawakukuta wahusika na kulazimika kushirikiana na wenyeviti wa mtaa, kujua ni nani waliokuwa wakiishi katika nyumba hizo.

Rugimbana alisema kwa ujumla kazi ya sensa katika wilaya hiyo ilikwenda vizuri ingawa mwanzoni kulikuwepo na upungufu wa vifaa ambapo NBS ilipoelezwa, ilishughulikia na sasa hakuna tena upungufu.

“Asilimia 80 ya makarani wamemaliza kushughulikia kaya kwa kaya sasa wanafanya majumuisho tu kujua ni wapi walikoacha kuhesabu,” alisema Rugimbana.

Aidha, alisema yapo matukio kadhaa yaliyowafikia, kwamba kuna baadhi ya watu wanakataa kuhesabiwa kwa kigezo cha dini, lakini alimshukuru Rais Jakaya Kikwete kwani hotuba yake ilileta mwelekeo mzuri wa kuelewa na kujiunga na sensa.

“Ipo baadhi ya misikiti ambayo waumini wao walikuwa wakiambiwa wasishiriki lakini wameshiriki,” alisema Rugimbana bila kuitaja.

Kadhalika, alisema zilikuwapo kaya 12 zilizoripotiwa katika maeneo ya Sinza, Mtambani na Mivumoni, ambazo hazikutaka kuhesabiwa, lakini polisi walipofika, kaya 10 walikubali kuhesabiwa huku mbili wakikosekana katika makazi yao. Imeandikwa na Shadrack Sagati na Lucy Lyatuu Dar na Sifa Lubasi, Dodoma.

Mwisho wa kuhesabiwa sensa leo


OFISI ya Takwimu ya Taifa (NBS) imesema watu ambao watakuwa hawajahesabiwa hadi leo, wawasiliane na viongozi wao wa mitaa, vitongoji na vijiji.

Akizungumza na gazeti hili jana, Ofisa Mawasiliano na Uhamasishaji wa NBS, Said Ameir alisema ofisi yake imetenga siku tano ili watu wote wawe wamehesabiwa.

Alifafanua, kama itatokea kuna watu hawajahesabiwa, watumie siku tatu zilizobaki kuanzia leo kuhakikisha wanafanya hivyo.

Alitaka waishio mijini wawasiliane na wenyekiti wa serikali za mitaa na wanaoishi vijijini wawasiliane na wenyeviti wa vitongoji na vijiji kwa msaada zaidi.

Ameir alifafanua kuwa pamoja na kuwa makarani wa sensa watapita, swali lao litabaki lile lile kuwa ni watu wangapi walilala ndani ya kaya hiyo usiku wa kuamkia Agosti 26.

Alikumbusha wananchi wahakikishe ambao hawakulala katika nyumba hizo usiku huo, hawahesabiwi kwani watakuwa wamehesabiwa walikotoka. Kuhusu matumizi ya dodoso fupi na dodoso refu, Ameir alisema katika kaya moja ni dodoso moja tu linatumika.

“Katika kaya ambako makarani wenye dodoso fupi wamepita, mwenye refu haruhusiwi kupita na pale alipopita mwenye refu mwenye fupi haruhusiwi kupita,” alifafanua. Alisema dodoso fupi linatumika kwa asilimia 70 ya kaya zinazohesabiwa wakati refu linatumika kwa asilimia 30 tu katika eneo moja.

Aliongeza kuwa fupi lina maswali 32 wakati refu lina maswali 62. Kuhusu taarifa za upungufu wa vifaa katika baadhi ya mikoa, Ameir alisema amesikia habari hizo lakini vifaa zaidi kwenye sensa ni madodoso ambayo alisema ofisi yake imehakikisha yapo mengi katika mikoa yote ili kusiwepo na tatizo hilo.

“Sisi unaposema vifaa ina maana ni madodoso, ukiacha sare za makarani, kwa hiyo tumejiimarisha kuhakikisha hakuna upungufu wowote,” alisema ofisa huyo. Ameir alitoa mwito kwa wananchi ambao hawajahesabiwa kuvuta subira kwani nia ya Serikali ni kuhakikisha kila Mtanzania anahesabiwa. Upungufu Dodoma Hata hivyo, Dodoma, makarani wa sensa walilazimika kudurufu madodoso ili kuendelea na kazi baada ya kuishiwa. Hali hiyo ya upungufu wa vifaa ilijitokeza mapema katika maeneo ya Uwanja wa Ndege na Majengo, ambako makarani walilazimika kusitisha kazi kwa muda.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk Rehema Nchimbi alikiri upungufu huo na kusema tatizo hilo limetatuliwa kutokana na vifaa hivyo kuwasili kutoka Dar es Salaam na vilitarajiwa kusambazwa katika maeneo yenye upungufu. Alisema wilaya ya Kondoa ilikuwa na upungufu mkubwa.

Wakimbia nyumba Mkoani Dar es Salaam katika wilaya ya Kinondoni, licha ya kwamba kazi ya sensa ilifanyika vizuri kwa kiwango kikubwa, lakini zipo nyumba mbili ambazo hazijahesabiwa kutokana na wahusika kukimbia.

Mkuu wa Wilaya hiyo, Jordan Rugimbana alisema hayo alipozungumza na gazeti hili kuhusu mwenendo wa sensa katika wilaya hiyo na kuzitaja nyumba hizo kuwa zipo maeneo ya Ununio na Mtambani.

Alisema katika nyumba hizo, makarani walipofika hawakukuta wahusika na kulazimika kushirikiana na wenyeviti wa mtaa, kujua ni nani waliokuwa wakiishi katika nyumba hizo.

Rugimbana alisema kwa ujumla kazi ya sensa katika wilaya hiyo ilikwenda vizuri ingawa mwanzoni kulikuwepo na upungufu wa vifaa ambapo NBS ilipoelezwa, ilishughulikia na sasa hakuna tena upungufu.

“Asilimia 80 ya makarani wamemaliza kushughulikia kaya kwa kaya sasa wanafanya majumuisho tu kujua ni wapi walikoacha kuhesabu,” alisema Rugimbana.

Aidha, alisema yapo matukio kadhaa yaliyowafikia, kwamba kuna baadhi ya watu wanakataa kuhesabiwa kwa kigezo cha dini, lakini alimshukuru Rais Jakaya Kikwete kwani hotuba yake ilileta mwelekeo mzuri wa kuelewa na kujiunga na sensa.

“Ipo baadhi ya misikiti ambayo waumini wao walikuwa wakiambiwa wasishiriki lakini wameshiriki,” alisema Rugimbana bila kuitaja.

Kadhalika, alisema zilikuwapo kaya 12 zilizoripotiwa katika maeneo ya Sinza, Mtambani na Mivumoni, ambazo hazikutaka kuhesabiwa, lakini polisi walipofika, kaya 10 walikubali kuhesabiwa huku mbili wakikosekana katika makazi yao. Imeandikwa na Shadrack Sagati na Lucy Lyatuu Dar na Sifa Lubasi, Dodoma.

Chadema ‘yakomalia’ kifo cha Morogoro


CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimesema hakina imani na Tume iliyoundwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) kuchunguza mauaji yanayodaiwa kufanywa na Polisi mkoani Morogoro wakati wa maandamano ya chama hicho.

Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa Chadema, John Mnyika alisema hayo jana Dar es Salaam wakati akitoa taarifa juu ya tukio la mauaji ya muuza magazeti wa eneo la Msamvu, Ally Zona (38).

Alisema kuna mgongano wa taarifa kuhusu tukio hilo kutoka kwa mashahidi na Polisi, akidai kuwa kifo hicho kina utata na hakiwezi kuchunguzwa na Polisi.

“Kiundwe chombo kingine huru cha uchunguzi au Rais Kikwete (Jakaya) aingilie kati iundwe Tume huru kuchunguza kifo hiki, kwani hii ya sasa haiwezi kuchunguzwa na polisi kwani wao ni watuhumiwa,” alisema Mnyika na kuongeza kuwa hata baadhi ya viongozi wa chama chake ni mashahidi.

Aidha, alisema chama hicho kwa kuheshimu sheria, kimeamua kusitisha operesheni ya vuguvugu ya mabadiliko iliyokuwa iendelee Iringa, na kuomba maelezo kutoka kwa Serikali na Polisi kuwa ni kwa nini vyama vingine vinaendeleza matukio ya kisiasa yenye halaiki ya wananchi huku Polisi wakiinyima Chadema ruhusa ya kufanya hivyo.

“Kwa mfano, Lindi Mjini kuna maandamano ya wafuasi wa CCM wanarudisha fomu kuwania nafasi za uchaguzi, huku polisi mikoani wakisema mikutano inayofanyika sasa inaingilia ratiba ya sensa,” alihoji Mnyika.

Alisema kutokana na tukio la Morogoro ipo haja ya sheria ya vifo vyenye utata ianze kutumika sasa ili kupata Tume huru ambayo itashughulikia mgogoro wa Morogoro na kuupatia suluhu stahiki.

Kuhusu kusaidia matibabu ya majeruhi wa tukio hilo, Mnyika alisema chama hicho kitahakikisha kinatoa matibabu yao na kuwezesha maziko ya marehemu huyo.

Hata hivyo, hakuzungumzia sababu ya kufanya maandamano juzi huku sensa ikiendelea na kuja kushituka baadaye na kusitisha operesheni yao.

Chadema ‘yakomalia’ kifo cha Morogoro


CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimesema hakina imani na Tume iliyoundwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) kuchunguza mauaji yanayodaiwa kufanywa na Polisi mkoani Morogoro wakati wa maandamano ya chama hicho.

Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa Chadema, John Mnyika alisema hayo jana Dar es Salaam wakati akitoa taarifa juu ya tukio la mauaji ya muuza magazeti wa eneo la Msamvu, Ally Zona (38).

Alisema kuna mgongano wa taarifa kuhusu tukio hilo kutoka kwa mashahidi na Polisi, akidai kuwa kifo hicho kina utata na hakiwezi kuchunguzwa na Polisi.

“Kiundwe chombo kingine huru cha uchunguzi au Rais Kikwete (Jakaya) aingilie kati iundwe Tume huru kuchunguza kifo hiki, kwani hii ya sasa haiwezi kuchunguzwa na polisi kwani wao ni watuhumiwa,” alisema Mnyika na kuongeza kuwa hata baadhi ya viongozi wa chama chake ni mashahidi.

Aidha, alisema chama hicho kwa kuheshimu sheria, kimeamua kusitisha operesheni ya vuguvugu ya mabadiliko iliyokuwa iendelee Iringa, na kuomba maelezo kutoka kwa Serikali na Polisi kuwa ni kwa nini vyama vingine vinaendeleza matukio ya kisiasa yenye halaiki ya wananchi huku Polisi wakiinyima Chadema ruhusa ya kufanya hivyo.

“Kwa mfano, Lindi Mjini kuna maandamano ya wafuasi wa CCM wanarudisha fomu kuwania nafasi za uchaguzi, huku polisi mikoani wakisema mikutano inayofanyika sasa inaingilia ratiba ya sensa,” alihoji Mnyika.

Alisema kutokana na tukio la Morogoro ipo haja ya sheria ya vifo vyenye utata ianze kutumika sasa ili kupata Tume huru ambayo itashughulikia mgogoro wa Morogoro na kuupatia suluhu stahiki.

Kuhusu kusaidia matibabu ya majeruhi wa tukio hilo, Mnyika alisema chama hicho kitahakikisha kinatoa matibabu yao na kuwezesha maziko ya marehemu huyo.

Hata hivyo, hakuzungumzia sababu ya kufanya maandamano juzi huku sensa ikiendelea na kuja kushituka baadaye na kusitisha operesheni yao.

Wednesday, August 29, 2012

Polisi waache matumizi mabaya ya silaha

KWAMBA askari polisi mjini Morogoro juzi walimuua kwa risasi kijana mmoja na kujeruhi wengine wawili wakati walipokuwa wakidhibiti maandamano ya wafuasi wa Chadema, ni taarifa ambazo zimetusikitisha sana na kutoa picha kwamba nchi yetu hakika bado ina safari ndefu kuelekea kwenye demokrasia ya kweli na utawala bora.

Tunasema nchi yetu bado ina safari ndefu kufikia vigezo vya demokrasia na utawala bora kutokana na matukio mengi makubwa tunayoshuhudia mara kwa mara katika sehemu kadhaa nchini. Aghalabu yamekuwapo matukio ya vifo na uvunjifu mkubwa wa haki za binadamu unaotokana na matumizi mabaya ya silaha na madaraka kwa upande wa Jeshi la Polisi. Mifano ya hali hiyo ya kusikitisha ni nyingi, lakini yatosha tu kusema hapa kwamba jeshi hilo kwa kiasi kikubwa limeshindwa kuelewa dhana ya ulinzi wa raia na haki ya mtu kuishi, ikiwa ndiyo dhima na dira kuu inayoliongoza jeshi hilo.

Yapo maeneo ambayo jeshi hilo limefanya vizuri na sisi tumekuwa msitari wa mbele kulimwagia sifa kila linapostahili kupongezwa. Lakini jeshi hilo limelaumiwa kwa mambo mengi ambayo hatuwezi kuyaorodhesha yote katika safu hii kutokana na ufinyu wa nafasi. Moja ya malalamiko makubwa ambayo yamekuwa yakielekezwa kwa jeshi hilo ni jinsi ambavyo limekuwa likivinyanyasa vyama vya upinzani na kuegemea kwa chama tawala. Miaka 20 tangu kuanzishwa kwa siasa za vyama vingi nchini, Jeshi la Polisi limekuwa halionekani kuvitendea haki vyama vya upinzani na limekuwa linavunja sheria ya mwaka 1992 ambayo ilianzisha vyama hivyo.

Kwa mfano, jeshi hilo limekataa kuelewa au kutambua kwamba sheria hiyo ya vyama vya siasa haitoi mamlaka kwa jeshi hilo kutoa vibali kwa vyama hivyo kufanya shughuli za siasa, yakiwamo maandamano, mikutano ya ndani na ya hadhara na shughuli nyingine zozote za kisiasa. Sheria inasema kuwa, ili shughuli hizo zifanyike kwa amani na utulivu, lazima vyama hivyo vilitaarifu rasmi Jeshi la Polisi ndani ya saa 48 kabla ya kufanyika kwa shughuli hizo ili jeshi hilo litoe ulinzi. Lakini katika hali ya kushangaza, jeshi hilo limejipachika mamlaka ya kuratibu shughuli za vyama hivyo kwa kutoa au kukataa kutoa vibali vya kufanyika kwa shughuli hizo.

Swali ambalo limekuwa likiulizwa na wananchi wengi ni kuhusu sababu za jeshi hilo kutoa vibali pasipo pingamizi kwa vikundi vinavyoandamana au kufanya mikutano ya hadhara kuipongeza Serikali na viongozi wake? Kama kweli ajenda ya jeshi hilo siyo ya siri na inaendeshwa kwa dhamira safi, inakuwaje halifanyi hivyo kwa vyama vya upinzani ambavyo vimesajiliwa kisheria au vikundi vya wanaharakati vinavyotetea haki za kijamii? Inakuwaje basi vyama vya upinzani na vya kiharakati vikataliwe kuendesha shughuli zake kwa kisingizio cha kutokuwapo polisi wa kutosha kulinda shughuli hizo, lakini polisi wa kusha, tena wenye magari yaliyosheheni silaha za kivita wanapatikana kuzuia shughuli hizo zisifanyike?

Badala ya kulikemea jeshi hilo kwa kuvunja sheria na kukandamiza demokrasia, chama tawala na Serikali yake mara zote vimekuwa vikikaa kimya, huku vikichekelea pembeni na kuliacha jeshi hilo likitekeleza kile kinachodaiwa na vyama vya upinzani kwamba ni kutekeleza maagizo kutoka juu. Pengine ndiyo sababu kila mara jeshi hilo linaposababisha vifo vya raia kwa kisingizio cha kudhibiti maandamano ambayo hayana vibali vya polisi, Serikali hujitokeza na kulipongeza jeshi hilo kwa kusimamia sheria.

Hivyo ndivyo ilivyokuwa jana. Akizungumzia tukio la Morogoro ambapo juzi mji huo na viunga vyake viligeuka uwanja wa mapambano, ambapo polisi waliua mtu mmoja kwa risasi wakati wakidhibiti maandamano ya wafuasi wa Chadema, Waziri wa Mambo ya Ndani, Emmanuel Nchimbi alisema polisi walikuwa wanatekeleza wajibu wao, huku akiwataka viongozi wa vyama vya siasa kufuata sheria.

Polisi waache matumizi mabaya ya silaha

KWAMBA askari polisi mjini Morogoro juzi walimuua kwa risasi kijana mmoja na kujeruhi wengine wawili wakati walipokuwa wakidhibiti maandamano ya wafuasi wa Chadema, ni taarifa ambazo zimetusikitisha sana na kutoa picha kwamba nchi yetu hakika bado ina safari ndefu kuelekea kwenye demokrasia ya kweli na utawala bora.

Tunasema nchi yetu bado ina safari ndefu kufikia vigezo vya demokrasia na utawala bora kutokana na matukio mengi makubwa tunayoshuhudia mara kwa mara katika sehemu kadhaa nchini. Aghalabu yamekuwapo matukio ya vifo na uvunjifu mkubwa wa haki za binadamu unaotokana na matumizi mabaya ya silaha na madaraka kwa upande wa Jeshi la Polisi. Mifano ya hali hiyo ya kusikitisha ni nyingi, lakini yatosha tu kusema hapa kwamba jeshi hilo kwa kiasi kikubwa limeshindwa kuelewa dhana ya ulinzi wa raia na haki ya mtu kuishi, ikiwa ndiyo dhima na dira kuu inayoliongoza jeshi hilo.

Yapo maeneo ambayo jeshi hilo limefanya vizuri na sisi tumekuwa msitari wa mbele kulimwagia sifa kila linapostahili kupongezwa. Lakini jeshi hilo limelaumiwa kwa mambo mengi ambayo hatuwezi kuyaorodhesha yote katika safu hii kutokana na ufinyu wa nafasi. Moja ya malalamiko makubwa ambayo yamekuwa yakielekezwa kwa jeshi hilo ni jinsi ambavyo limekuwa likivinyanyasa vyama vya upinzani na kuegemea kwa chama tawala. Miaka 20 tangu kuanzishwa kwa siasa za vyama vingi nchini, Jeshi la Polisi limekuwa halionekani kuvitendea haki vyama vya upinzani na limekuwa linavunja sheria ya mwaka 1992 ambayo ilianzisha vyama hivyo.

Kwa mfano, jeshi hilo limekataa kuelewa au kutambua kwamba sheria hiyo ya vyama vya siasa haitoi mamlaka kwa jeshi hilo kutoa vibali kwa vyama hivyo kufanya shughuli za siasa, yakiwamo maandamano, mikutano ya ndani na ya hadhara na shughuli nyingine zozote za kisiasa. Sheria inasema kuwa, ili shughuli hizo zifanyike kwa amani na utulivu, lazima vyama hivyo vilitaarifu rasmi Jeshi la Polisi ndani ya saa 48 kabla ya kufanyika kwa shughuli hizo ili jeshi hilo litoe ulinzi. Lakini katika hali ya kushangaza, jeshi hilo limejipachika mamlaka ya kuratibu shughuli za vyama hivyo kwa kutoa au kukataa kutoa vibali vya kufanyika kwa shughuli hizo.

Swali ambalo limekuwa likiulizwa na wananchi wengi ni kuhusu sababu za jeshi hilo kutoa vibali pasipo pingamizi kwa vikundi vinavyoandamana au kufanya mikutano ya hadhara kuipongeza Serikali na viongozi wake? Kama kweli ajenda ya jeshi hilo siyo ya siri na inaendeshwa kwa dhamira safi, inakuwaje halifanyi hivyo kwa vyama vya upinzani ambavyo vimesajiliwa kisheria au vikundi vya wanaharakati vinavyotetea haki za kijamii? Inakuwaje basi vyama vya upinzani na vya kiharakati vikataliwe kuendesha shughuli zake kwa kisingizio cha kutokuwapo polisi wa kutosha kulinda shughuli hizo, lakini polisi wa kusha, tena wenye magari yaliyosheheni silaha za kivita wanapatikana kuzuia shughuli hizo zisifanyike?

Badala ya kulikemea jeshi hilo kwa kuvunja sheria na kukandamiza demokrasia, chama tawala na Serikali yake mara zote vimekuwa vikikaa kimya, huku vikichekelea pembeni na kuliacha jeshi hilo likitekeleza kile kinachodaiwa na vyama vya upinzani kwamba ni kutekeleza maagizo kutoka juu. Pengine ndiyo sababu kila mara jeshi hilo linaposababisha vifo vya raia kwa kisingizio cha kudhibiti maandamano ambayo hayana vibali vya polisi, Serikali hujitokeza na kulipongeza jeshi hilo kwa kusimamia sheria.

Hivyo ndivyo ilivyokuwa jana. Akizungumzia tukio la Morogoro ambapo juzi mji huo na viunga vyake viligeuka uwanja wa mapambano, ambapo polisi waliua mtu mmoja kwa risasi wakati wakidhibiti maandamano ya wafuasi wa Chadema, Waziri wa Mambo ya Ndani, Emmanuel Nchimbi alisema polisi walikuwa wanatekeleza wajibu wao, huku akiwataka viongozi wa vyama vya siasa kufuata sheria.

Lowassa: Siungi mkono Kilimo Kwanza



Aliyewahi kuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa
ASEMA HATA CCM INAJUA MSIMAMO WAKE, WAZIRI KABAKA ASISITIZA KILIMO NI LAZIMA, PROFESA LIPUMBA, MBATIA WAMSHANGAA
Peter Edson
WAKATI Serikali ikielekeza nguvu nyingi kutekeleza mkakati wa kuendeleza sekta ya kilimo nchini uliopewa jina la Kilimo Kwanza, aliyewahi kuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa ameibuka na kusema haungi mkono mkakati huo.Alisema mkakati huo wa Kilimo Kwanza umekosa mashiko hivyo ili auunge mkono, kuna haja ya kubadili dhana yake na kuwa, elimu kabla ya kilimo kwanza.

“Ni vyema nikaeleweka hapa. Ninachomaanisha ni kuongeza elimu katika Kilimo Kwanza ili wananchi wawe na elimu kwanza ndipo waweze kuboresha kilimo,” alisema Lowassa.

Akizungumza katika Kipindi cha Dakika 45 kilichorushwa na Kituo cha Televisheni cha ITV juzi usiku, Lowassa alisema pamoja na Serikali kuwa na nia nzuri ya kumkomboa mwananchi kwa kuboresha mazingira ya kilimo, jambo hilo litakuwa si chochote kama hatapatiwa elimu itakayomwongoza kwenye mapinduzi hayo ya kijani.

“Mpango huu wa Kilimo Kwanza umekosa nguvu kwa sababu kuanzishwa kwake hakukuzingatia dhana ya ukombozi wa mwananchi wa kawaida. Tangu awali ndani ya chama (CCM) nilieleza kuwa sitaunga mkono hoja hiyo mpaka kuongezwe mashiko na kuwa Elimu Kabla ya Kilimo Kwanza,” alisema Lowasa na kuongeza:

“Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere alitoa uamuzi mgumu na wenye busara, ndiyo maana kilimo cha pamba, kahawa, mkonge na mazao mengine vikaanzishwa. Hivyo ipo haja ya kufanyika mchakato wa kuona mbali zaidi ili viongozi wetu waweze kutoa uamuzi sahihi katika hoja hii ya Kilimo Kwanza, kwani nguvu nyingi pasipo elimu inaweza kuligharimu taifa.”

Alisema kuwa ili mwananchi wa kawaida aweze kunufaika na Kilimo Kwanza, anahitaji kupatiwa elimu ya kutosha ya namna ya kuandaa mazingira ya kilimo na uelewa wa vifaa na pembejeo za kilimo ikiwemo mbolea na dawa.

Alisema pamoja na kuwa na mabwana shamba wachache, wananchi wamejikuta wakitumia mawazo yao kufanikisha miradi ya kilimo katika maeneo yao na matokeo yake wanapata mazao kidogo ambayo hayawakwamui kiuchumi.

Alitoa mfano wa nchi ya Indonesia akisema inaendesha uchumi wake kwa kilimo cha michikichi, ambayo mbegu zake zimetoka Tanzania... “Lakini Tanzania iliyotoa michikichi hiyo sasa ni moja ya wateja wa mafuta hayo yanayotoka Indonesia.”

Alishauri Serikali kuanzisha mashamba ya michikichi maeneo mbalimbali nchini kwa kuwa ardhi ipo ya kutosha hivyo kujitosheleza kwa mafuta hata ya kuuza nje.

“Ningelikuwa na uwezo wa kutoa uamuzi, vijana wetu wa JKT (Jeshi la Kujenga Taifa), ningewapa kazi ya kuanzisha mashamba ya michikichi nchi nzima kwani nchi yetu imejaliwa kuwa na ardhi kubwa na yenye rutuba, mapori yapo mengi,” alisema Lowassa.

Alisema wananchi wanaweza kupewa matrekta na pembejeo mbalimbali za kilimo, lakini bila kupewa elimu elekezi ya namna ya kuzitumia pembejeo hizo kuzalisha mazao bora, itakuwa kazi bure kwa kuwa ongezeko la mazao litakuwa dogo kama ilivyo kwa kilimo cha jembe la mkono.

Alitoa wito kwa Serikali kutumia fursa zilizopo za miradi ya kilimo kuwaelimisha Watanzania ili baadaye waweze kupewa au kukopeshwa zana za kilimo, akieleza kuwa nguvu kazi na elimu, ndivyo vitakavyomkomboa mwananchi katika umaskini wa kipato.

Kabaka: Kilimo lazima
Alipotakiwa kuzungumzia kauli hiyo, Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudencia Kabaka alisema kilimo ni lazima na Lowassa lazima akubaliane na mpango wa Serikali wa kutekeleza Kilimo Kwanza.

“Lowassa lazima akubaliane na msimamo wa Serikali wa kutekeleza Kilimo Kwanza. Kilimo ni lazima,” alisema Kabaka na kuongeza kuwa sekta hiyo ndiyo inayotoa ajira kwa watu wengi kuliko nyingine.

Alisema Tanzania ina wahitimu zaidi ya 800,000 wa elimu ya juu wa fani mbalimbali ambao moja ya ajira ambazo wanapaswa kujiunga nazo ni kilimo na hakuna ambaye anaweza kutafuta elimu akiwa na njaa... “Serikali itaendelea kusimamia Kilimo Kwanza na tunamtaka Lowassa atuunge mkono.”

Waziri huyo alisema Serikali haipuuzi elimu, lakini ukweli unabaki kuwa sekta ya kilimo ilisahaulika kitambo hivyo kupitia Kilimo Kwanza ukiacha ajira za wakulima wa kawaida, pia maofisa ugani wa kada mbalimbali wanaajiriwa.

“Hata huko kijijini huwezi kusema unampelekea elimu mtu ambaye ana njaa. Huwezi kueleweka, lakini tunajua watu wakishiba wataweza kufanya mambo mengine hivyo kauli yake kuwa kwanza ingetolewa elimu haina tija,” alisema.

Profesa Lipumba, Mbatia wamshangaa
Kauli hiyo ya Lowassa imeonekana kumkera mchumi maarufu nchini na Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba na Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, James Mbatia. Kwa nyakati tofauti jana, viongozi hao wa vyama vya upinzani walihoji mamlaka ya kimaadili aliyonayo Lowassa ya kusema hayo.

Profesa Ibrahim Lipumba alimponda akisema anachofanya kada huyo wa CCM ni kujipapatua kisiasa kwani Kilimo Kwanza ni muhimu kwa maendeleo ya Taifa.

Profesa Lipumba alisema kauli hiyo ya Lowassa inaonyesha kana kwamba hafahamu vizuri mkakati huo wa Kilimo Kwanza hivyo ni bora akachukua muda kujifunza kabla ya kutoa kauli hizo.

Profesa Lipumba alisema katika kutekeleza Kilimo Kwanza, elimu pia hutolewa hivyo haiwezekani kusema kuwa itolewe kwanza elimu kabla ya kutekeleza mpango huo, kwa kuwa vyote vinakwenda pamoja.
“Huwezi kusema kuwa eti utoe elimu kwanza kisha ndiyo uanze utekelezaji. Hivi vyote vinatakiwa kwenda pamoja labda kasoro zilizopo ni kuwa Kilimo Kwanza kimewalenga wakulima wakubwa wakitarajiwa wawainue wadogo jambo ambalo haliwezekani,” alisema.

Alisema utekelezaji wa Sera ya Kilimo ni jambo jema kutokana na ukweli kuwa katika kipindi cha zaidi ya miaka 10 iliyopita, wakulima wamesahaulika na kufanya ukuaji wa kilimo kuwa asilimia nne, kiwango ambacho ni cha chini kwa mahitaji ya ongezeko la watu ambalo ni wastani wa asilimia moja kwa mwaka.
“Kilimo ni muhimu katika ukuaji wa uchumi wa taifa lolote duniani na kitendo
cha kuwategemea wakulima wakubwa ni kasoro ambayo inapaswa kufanyiwa kazi katika utekelezaji wa mpango huu wa Kilimo Kwanza,” alisema Profesa Lipumba.

Mbatia alisema anamshangaa Lowassa kupingana na uamuzi wa chama chake kwa kuwa mkakati wa Kilimo Kwanza ulipitishwa na chama chake... “Lowassa ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, hivyo Kilimo Kwanza ni uamuzi wa CCM. Anapingaje wakati hata alipojiuzulu alisema anafanya hivyo kulinda masilahi ya chama, leo anapinga mipango ya chama hichohicho?”

Alisema kama anaona haendani na mambo yanayofanywa na CCM ni vyema ajiondoe na kujiunga na chama kingine au kuanzisha chake ili awe na fursa nzuri ya kupinga kazi za chama tawala.

Ajira

Lowassa pia alizungumzia suala la ajira akisema viwanda vikifufuliwa vitanufaisha Watanzania wengi kwa kupata ajira na hivyo kuondoa dhana ya kuwepo kwa wahitimu wengi wa vyuo vikuu wasiokuwa na ajira.
“Unapotangaza kazi ya watu 20, barua za maombi ya kazi zinakuja 2,000, tusisubiri maandamano, tutatue tatizo hili sasa,” alisema Lowassa na kuongeza:

“Hili suala linahitaji ufumbuzi wa haraka ingawa tumechelewa. Nilimshangaa sana yule waziri niliposema kuna shida ya ajira, akasema hakuna tatizo hilo.”

Tangu mwaka jana, Lowassa amenukuliwa na vyombo vya habari mara kadhaa akisema ukosefu wa ajira kwa vijana ni tatizo kubwa nchini, akilifananisha na bomu linalosubiri kulipuka ikiwa halitatafutiwa ufumbuzi.
Hata hivyo, Machi 21 mwaka huu, Kabaka katika mkutano na wanahabari alipinga kauli hiyo ya Lowassa akisema:
“Hali halisi ya ukuaji wa uchumi nchini ni nzuri lakini, haiwezi kuonekana kama wananchi wake ni maskini na hawana ajira. Hata hivyo, Serikali imekuwa ikichukua hatua mbalimbali kushughulikia suala hilo ikiwamo la kuhimiza uwekezaji nchini,” alisema Kabaka na kuongeza:

“Kitendo cha wanasiasa kuendelea kusema tatizo la ajira kwa vijana ni bomu linalosubiri kulipuka, siyo kweli na kudai Serikali haijafanya kitu wanakuwa hawaitendei haki. Tatizo limepungua kutoka asilimia 12.9 mwaka 2000/01 hadi asilimia 11.7, mwaka 2006.

Mbio za urais 2015
Alipotakiwa kueleza iwapo ana mpango wa kuwania urais mwaka 2015, Lowassa alisema suala hilo halipaswi kuzungumzwa sasa kwani linaweza kufungua uwanja wa malumbano.

“Waingereza wana msemo mmoja unaosema, ‘tutavuka daraja tutakapolifikia.’ 2015 bado ni mbali ukisema chochote sasa utafungua uwanja wa malumbano, tusubiri 2015 bado ni mbali,” alisema Lowassa.

Lowassa: Siungi mkono Kilimo Kwanza



Aliyewahi kuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa
ASEMA HATA CCM INAJUA MSIMAMO WAKE, WAZIRI KABAKA ASISITIZA KILIMO NI LAZIMA, PROFESA LIPUMBA, MBATIA WAMSHANGAA
Peter Edson
WAKATI Serikali ikielekeza nguvu nyingi kutekeleza mkakati wa kuendeleza sekta ya kilimo nchini uliopewa jina la Kilimo Kwanza, aliyewahi kuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa ameibuka na kusema haungi mkono mkakati huo.Alisema mkakati huo wa Kilimo Kwanza umekosa mashiko hivyo ili auunge mkono, kuna haja ya kubadili dhana yake na kuwa, elimu kabla ya kilimo kwanza.

“Ni vyema nikaeleweka hapa. Ninachomaanisha ni kuongeza elimu katika Kilimo Kwanza ili wananchi wawe na elimu kwanza ndipo waweze kuboresha kilimo,” alisema Lowassa.

Akizungumza katika Kipindi cha Dakika 45 kilichorushwa na Kituo cha Televisheni cha ITV juzi usiku, Lowassa alisema pamoja na Serikali kuwa na nia nzuri ya kumkomboa mwananchi kwa kuboresha mazingira ya kilimo, jambo hilo litakuwa si chochote kama hatapatiwa elimu itakayomwongoza kwenye mapinduzi hayo ya kijani.

“Mpango huu wa Kilimo Kwanza umekosa nguvu kwa sababu kuanzishwa kwake hakukuzingatia dhana ya ukombozi wa mwananchi wa kawaida. Tangu awali ndani ya chama (CCM) nilieleza kuwa sitaunga mkono hoja hiyo mpaka kuongezwe mashiko na kuwa Elimu Kabla ya Kilimo Kwanza,” alisema Lowasa na kuongeza:

“Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere alitoa uamuzi mgumu na wenye busara, ndiyo maana kilimo cha pamba, kahawa, mkonge na mazao mengine vikaanzishwa. Hivyo ipo haja ya kufanyika mchakato wa kuona mbali zaidi ili viongozi wetu waweze kutoa uamuzi sahihi katika hoja hii ya Kilimo Kwanza, kwani nguvu nyingi pasipo elimu inaweza kuligharimu taifa.”

Alisema kuwa ili mwananchi wa kawaida aweze kunufaika na Kilimo Kwanza, anahitaji kupatiwa elimu ya kutosha ya namna ya kuandaa mazingira ya kilimo na uelewa wa vifaa na pembejeo za kilimo ikiwemo mbolea na dawa.

Alisema pamoja na kuwa na mabwana shamba wachache, wananchi wamejikuta wakitumia mawazo yao kufanikisha miradi ya kilimo katika maeneo yao na matokeo yake wanapata mazao kidogo ambayo hayawakwamui kiuchumi.

Alitoa mfano wa nchi ya Indonesia akisema inaendesha uchumi wake kwa kilimo cha michikichi, ambayo mbegu zake zimetoka Tanzania... “Lakini Tanzania iliyotoa michikichi hiyo sasa ni moja ya wateja wa mafuta hayo yanayotoka Indonesia.”

Alishauri Serikali kuanzisha mashamba ya michikichi maeneo mbalimbali nchini kwa kuwa ardhi ipo ya kutosha hivyo kujitosheleza kwa mafuta hata ya kuuza nje.

“Ningelikuwa na uwezo wa kutoa uamuzi, vijana wetu wa JKT (Jeshi la Kujenga Taifa), ningewapa kazi ya kuanzisha mashamba ya michikichi nchi nzima kwani nchi yetu imejaliwa kuwa na ardhi kubwa na yenye rutuba, mapori yapo mengi,” alisema Lowassa.

Alisema wananchi wanaweza kupewa matrekta na pembejeo mbalimbali za kilimo, lakini bila kupewa elimu elekezi ya namna ya kuzitumia pembejeo hizo kuzalisha mazao bora, itakuwa kazi bure kwa kuwa ongezeko la mazao litakuwa dogo kama ilivyo kwa kilimo cha jembe la mkono.

Alitoa wito kwa Serikali kutumia fursa zilizopo za miradi ya kilimo kuwaelimisha Watanzania ili baadaye waweze kupewa au kukopeshwa zana za kilimo, akieleza kuwa nguvu kazi na elimu, ndivyo vitakavyomkomboa mwananchi katika umaskini wa kipato.

Kabaka: Kilimo lazima
Alipotakiwa kuzungumzia kauli hiyo, Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudencia Kabaka alisema kilimo ni lazima na Lowassa lazima akubaliane na mpango wa Serikali wa kutekeleza Kilimo Kwanza.

“Lowassa lazima akubaliane na msimamo wa Serikali wa kutekeleza Kilimo Kwanza. Kilimo ni lazima,” alisema Kabaka na kuongeza kuwa sekta hiyo ndiyo inayotoa ajira kwa watu wengi kuliko nyingine.

Alisema Tanzania ina wahitimu zaidi ya 800,000 wa elimu ya juu wa fani mbalimbali ambao moja ya ajira ambazo wanapaswa kujiunga nazo ni kilimo na hakuna ambaye anaweza kutafuta elimu akiwa na njaa... “Serikali itaendelea kusimamia Kilimo Kwanza na tunamtaka Lowassa atuunge mkono.”

Waziri huyo alisema Serikali haipuuzi elimu, lakini ukweli unabaki kuwa sekta ya kilimo ilisahaulika kitambo hivyo kupitia Kilimo Kwanza ukiacha ajira za wakulima wa kawaida, pia maofisa ugani wa kada mbalimbali wanaajiriwa.

“Hata huko kijijini huwezi kusema unampelekea elimu mtu ambaye ana njaa. Huwezi kueleweka, lakini tunajua watu wakishiba wataweza kufanya mambo mengine hivyo kauli yake kuwa kwanza ingetolewa elimu haina tija,” alisema.

Profesa Lipumba, Mbatia wamshangaa
Kauli hiyo ya Lowassa imeonekana kumkera mchumi maarufu nchini na Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba na Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, James Mbatia. Kwa nyakati tofauti jana, viongozi hao wa vyama vya upinzani walihoji mamlaka ya kimaadili aliyonayo Lowassa ya kusema hayo.

Profesa Ibrahim Lipumba alimponda akisema anachofanya kada huyo wa CCM ni kujipapatua kisiasa kwani Kilimo Kwanza ni muhimu kwa maendeleo ya Taifa.

Profesa Lipumba alisema kauli hiyo ya Lowassa inaonyesha kana kwamba hafahamu vizuri mkakati huo wa Kilimo Kwanza hivyo ni bora akachukua muda kujifunza kabla ya kutoa kauli hizo.

Profesa Lipumba alisema katika kutekeleza Kilimo Kwanza, elimu pia hutolewa hivyo haiwezekani kusema kuwa itolewe kwanza elimu kabla ya kutekeleza mpango huo, kwa kuwa vyote vinakwenda pamoja.
“Huwezi kusema kuwa eti utoe elimu kwanza kisha ndiyo uanze utekelezaji. Hivi vyote vinatakiwa kwenda pamoja labda kasoro zilizopo ni kuwa Kilimo Kwanza kimewalenga wakulima wakubwa wakitarajiwa wawainue wadogo jambo ambalo haliwezekani,” alisema.

Alisema utekelezaji wa Sera ya Kilimo ni jambo jema kutokana na ukweli kuwa katika kipindi cha zaidi ya miaka 10 iliyopita, wakulima wamesahaulika na kufanya ukuaji wa kilimo kuwa asilimia nne, kiwango ambacho ni cha chini kwa mahitaji ya ongezeko la watu ambalo ni wastani wa asilimia moja kwa mwaka.
“Kilimo ni muhimu katika ukuaji wa uchumi wa taifa lolote duniani na kitendo
cha kuwategemea wakulima wakubwa ni kasoro ambayo inapaswa kufanyiwa kazi katika utekelezaji wa mpango huu wa Kilimo Kwanza,” alisema Profesa Lipumba.

Mbatia alisema anamshangaa Lowassa kupingana na uamuzi wa chama chake kwa kuwa mkakati wa Kilimo Kwanza ulipitishwa na chama chake... “Lowassa ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, hivyo Kilimo Kwanza ni uamuzi wa CCM. Anapingaje wakati hata alipojiuzulu alisema anafanya hivyo kulinda masilahi ya chama, leo anapinga mipango ya chama hichohicho?”

Alisema kama anaona haendani na mambo yanayofanywa na CCM ni vyema ajiondoe na kujiunga na chama kingine au kuanzisha chake ili awe na fursa nzuri ya kupinga kazi za chama tawala.

Ajira

Lowassa pia alizungumzia suala la ajira akisema viwanda vikifufuliwa vitanufaisha Watanzania wengi kwa kupata ajira na hivyo kuondoa dhana ya kuwepo kwa wahitimu wengi wa vyuo vikuu wasiokuwa na ajira.
“Unapotangaza kazi ya watu 20, barua za maombi ya kazi zinakuja 2,000, tusisubiri maandamano, tutatue tatizo hili sasa,” alisema Lowassa na kuongeza:

“Hili suala linahitaji ufumbuzi wa haraka ingawa tumechelewa. Nilimshangaa sana yule waziri niliposema kuna shida ya ajira, akasema hakuna tatizo hilo.”

Tangu mwaka jana, Lowassa amenukuliwa na vyombo vya habari mara kadhaa akisema ukosefu wa ajira kwa vijana ni tatizo kubwa nchini, akilifananisha na bomu linalosubiri kulipuka ikiwa halitatafutiwa ufumbuzi.
Hata hivyo, Machi 21 mwaka huu, Kabaka katika mkutano na wanahabari alipinga kauli hiyo ya Lowassa akisema:
“Hali halisi ya ukuaji wa uchumi nchini ni nzuri lakini, haiwezi kuonekana kama wananchi wake ni maskini na hawana ajira. Hata hivyo, Serikali imekuwa ikichukua hatua mbalimbali kushughulikia suala hilo ikiwamo la kuhimiza uwekezaji nchini,” alisema Kabaka na kuongeza:

“Kitendo cha wanasiasa kuendelea kusema tatizo la ajira kwa vijana ni bomu linalosubiri kulipuka, siyo kweli na kudai Serikali haijafanya kitu wanakuwa hawaitendei haki. Tatizo limepungua kutoka asilimia 12.9 mwaka 2000/01 hadi asilimia 11.7, mwaka 2006.

Mbio za urais 2015
Alipotakiwa kueleza iwapo ana mpango wa kuwania urais mwaka 2015, Lowassa alisema suala hilo halipaswi kuzungumzwa sasa kwani linaweza kufungua uwanja wa malumbano.

“Waingereza wana msemo mmoja unaosema, ‘tutavuka daraja tutakapolifikia.’ 2015 bado ni mbali ukisema chochote sasa utafungua uwanja wa malumbano, tusubiri 2015 bado ni mbali,” alisema Lowassa.