Tuesday, July 31, 2012

Gazeti la Mwanahalisi lafungiwa

• Kubenea atoa kauli, wadau wa habari waja juu

SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imelifungia gazeti la Mwanahalisi kwa muda usiojulikana, kwa kile kilichoelezwa kuwa ni kutokana na mwenendo wake wa kuandika habari na makala za uchozezi.

Kwa mujibu wa serikali, sababu nyingine ya kufungiwa kwa gazeti hilo ni pamoja na kujenga uhasama na uzushi, likiwa na nia ya kusababisha wananchi wakose imani na vyombo vya dola, hali inayoweza kuhatarisha amani na mshikamano wa nchi.

Akisoma tamko la serikali lililotolewa na Msajili wa Magazeti jana jijini Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo (MAELEZO), Phabian Lugaikamu, alisema kuwa katika toleo la gazeti hilo namba 302, 303 na 304 ya mwaka 2012 na mengine yaliyotangulia yalichapisha habari na makala zenye kueneza na kujenga hofu kwa jamii.

“Mhariri wa gazeti la Mwanahalisi ameitwa na kuonywa mara nyingi lakini hataki kukiri kuwa maudhui ya makala zake hazina tija kwa jamii, pia hazifuati weledi na maadili ya taaluma ya uandishi wa habari,” alisema.

Aidha, alisema kuwa mhariri huyo mara zote katika utetezi wake amekuwa akinukuu kifungu cha 18 cha Katiba ya nchi kinachotoa uhuru wa kutoa maoni na kwa makusudi kutokunukuu kifungu cha 30 cha Katiba hiyo hiyo kinachoweka ukomo wa uhuru wa kutoa maoni.

“Serikali imeamua kulifungia gazeti hilo kutochapishwa kwa muda usiojulikana kwa mujibu wa sheria ya magazeti ya mwaka 1976, kifungu namba 25(i), adhabu hiyo itaanza tarehe 30 Julai, 2012 kwa mujibu wa tangazo la serikali namba 258 lililochapishwa katika gazeti la Serikali na kutolewa jijini Dar es Salaam Julai 27, 2012,” alisema.

Aidha, serikali imewataka wamiliki, wahariri na wanahabari kuzingatia sheria, uzalendo, weledi na maadili ya taaluma ya uandishi wa habari ili kutekeleza wajibu wa kuhabarisha, kuelimisha na kutoa burudani kwa wananchi.

Aidha, Lugaikamu alisema kuwa serikali haitasita kuchukua hatua dhidi ya vyombo vya habari ambavyo vitatoa taarifa za uchochezi ambazo zitahatarisha hali ya amani na utulivu.

Saed Kubenea atoa kauli


Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mwanahalisi Communications inayochapisha gazeti la Mwanahalisi na gazeti dada la michezo la Mseto, Saed Kubenea, alisema kuwa ni jambo la kusikitisha na kuhuzunisha kwani kisheria mashitaka ya uchozezi ni ya jinai, hivyo serikali kama ilikuwa na ushahidi ilitakiwa ilipeleke Mwanahalisi mahakamani.

Kubenea alisema hakuna haja ya kuogopa serikali, kwani kama ina hoja ni vema iende mahakamani ili aamuliwe mshindi nani, na kuachana na tabia ya kuendesha shughuli zake kwa kuvizia.

“Serikali ikae kimya iandikwe, kulifungia Mwanahalisi kwa habari iliyoandikwa itaonekana inakiri na inaogopa kusemwa ukweli,” alisema.

CUF yatoa tamko, Lissu awaka bungeni

Wakati akichangia mjadala wa bajeti ya Wizara ya afya mjini Dodoma jana, Mnadhimu Mkuu wa kambi rasmi ya upinzani Bungeni, Tundu Lissu, alitumia nafasi hiyo kuishambulia serikali na kutaka iachane na sheria kandamizi dhidi ya vyombo vya habari.

Naye Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Julius Mtatiro, alisema serikali isije kudhani kutumia mabavu kwa vyombo vya habari kutasaidia kuficha maovu yake na kutaka uhuru wa vyombo vya habari upewe kipaumbele.

Jukwaa la Wahariri waja juu

Baadhi ya wadau wa habari akiwamo Katibu Mkuu wa Jukwaa la Wahariri (TEF), Neville Meena, alisema kuwa kitendo cha kulifungia gazeti la Mwanahalisi hakikubaliki, huku akihoji aliyelifungia ni nani na kwa utaratibu upi, kwa kipi na waziri anatoa wapi maamuzi ya kulifungia.

Meena pia alisema mfumo mzima una matatizo kwani mtu mmoja hawezi kutoa maamuzi na mahali pekee penye haki ni mahakamani, kwani ndipo sehemu watu wanapopambana na kupatikana aliyesimama kwenye haki.

“Hakuna haki wala uhuru wa habari, tunataka haki itendeke kwa wanaoandikiwa na wanaoandika, tutajuaje kama makosa waliyofungiwa yana ukweli na unasema tunalifungia muda usiojulikana ndiyo nini? Ungefuatwa utaratibu wa mahakama,” alisema.

Meena pia alisema TEF wanatarajia kutoa tamko leo kuhusiana na jambo hilo.

Mhariri Tanzania Daima aguswa

Naye Mhariri Mtendaji wa gazeti hili, Absalom Kibanda, alisema taarifa za serikali kulifungia gazeti hilo zilivuja na jambo hilo haliingii akilini kwani taifa limekuwa likizungumzia uhuru wa kujieleza.

Kibanda pia alisema kuwa sheria zilizopo ni kandamizi na kulifungia gazeti hilo ni hatua nyingine ya kukandamiza na kutishia, ikiwamo kuwanyima wanahabari haki yao na maelfu ya wananchi kupata habari kupitia Mwanahalisi.

“Kwanini wasitoe maelezo kuhusu Mwanahalisi lilifanya nini kuhusiana na kile kilichokuwa kikiandikwa? Mimi naona hata serikali haikuzingatia weledi, ikiwamo kutoa ufafanuzi na kwa stahili hii nasema Mwanahalisi iliigusa serikali pabaya,” alisema Kibanda.

Pia aliitaka serikali kutoingilia uhuru wa habari, ikiwamo kutambua gharama za demokrasia, isiinyime mawazo na kutambua kuwa ukinzani wa mawazo ndipo kwenye maendeleo.

TAMWA nao wacharuka

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake, Ananilea Nkya, alieleza kupitia mtandao wa mabadiliko kuwa hatua hiyo ya serikali ya kulifungia gazeti la Mwanahalisi badala ya kwenda mahakamani ni ishara kwamba yaliyoandikwa na gazeti hilo ni ukweli mtupu.

“Labda niulize swali moja tu, hivi mfalme akiambiwa yuko uchi, kama hajawa uchi ni kwa nini aamue kumuua/kumwadhibu aliyemwambia yuko uchi kabla ya yeye mfalme kuthibitisha kuwa hajawa uchi?,” alihoji.



Source: Tanzania Daima.




Gazeti la Mwanahalisi lafungiwa

• Kubenea atoa kauli, wadau wa habari waja juu

SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imelifungia gazeti la Mwanahalisi kwa muda usiojulikana, kwa kile kilichoelezwa kuwa ni kutokana na mwenendo wake wa kuandika habari na makala za uchozezi.

Kwa mujibu wa serikali, sababu nyingine ya kufungiwa kwa gazeti hilo ni pamoja na kujenga uhasama na uzushi, likiwa na nia ya kusababisha wananchi wakose imani na vyombo vya dola, hali inayoweza kuhatarisha amani na mshikamano wa nchi.

Akisoma tamko la serikali lililotolewa na Msajili wa Magazeti jana jijini Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo (MAELEZO), Phabian Lugaikamu, alisema kuwa katika toleo la gazeti hilo namba 302, 303 na 304 ya mwaka 2012 na mengine yaliyotangulia yalichapisha habari na makala zenye kueneza na kujenga hofu kwa jamii.

“Mhariri wa gazeti la Mwanahalisi ameitwa na kuonywa mara nyingi lakini hataki kukiri kuwa maudhui ya makala zake hazina tija kwa jamii, pia hazifuati weledi na maadili ya taaluma ya uandishi wa habari,” alisema.

Aidha, alisema kuwa mhariri huyo mara zote katika utetezi wake amekuwa akinukuu kifungu cha 18 cha Katiba ya nchi kinachotoa uhuru wa kutoa maoni na kwa makusudi kutokunukuu kifungu cha 30 cha Katiba hiyo hiyo kinachoweka ukomo wa uhuru wa kutoa maoni.

“Serikali imeamua kulifungia gazeti hilo kutochapishwa kwa muda usiojulikana kwa mujibu wa sheria ya magazeti ya mwaka 1976, kifungu namba 25(i), adhabu hiyo itaanza tarehe 30 Julai, 2012 kwa mujibu wa tangazo la serikali namba 258 lililochapishwa katika gazeti la Serikali na kutolewa jijini Dar es Salaam Julai 27, 2012,” alisema.

Aidha, serikali imewataka wamiliki, wahariri na wanahabari kuzingatia sheria, uzalendo, weledi na maadili ya taaluma ya uandishi wa habari ili kutekeleza wajibu wa kuhabarisha, kuelimisha na kutoa burudani kwa wananchi.

Aidha, Lugaikamu alisema kuwa serikali haitasita kuchukua hatua dhidi ya vyombo vya habari ambavyo vitatoa taarifa za uchochezi ambazo zitahatarisha hali ya amani na utulivu.

Saed Kubenea atoa kauli


Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mwanahalisi Communications inayochapisha gazeti la Mwanahalisi na gazeti dada la michezo la Mseto, Saed Kubenea, alisema kuwa ni jambo la kusikitisha na kuhuzunisha kwani kisheria mashitaka ya uchozezi ni ya jinai, hivyo serikali kama ilikuwa na ushahidi ilitakiwa ilipeleke Mwanahalisi mahakamani.

Kubenea alisema hakuna haja ya kuogopa serikali, kwani kama ina hoja ni vema iende mahakamani ili aamuliwe mshindi nani, na kuachana na tabia ya kuendesha shughuli zake kwa kuvizia.

“Serikali ikae kimya iandikwe, kulifungia Mwanahalisi kwa habari iliyoandikwa itaonekana inakiri na inaogopa kusemwa ukweli,” alisema.

CUF yatoa tamko, Lissu awaka bungeni

Wakati akichangia mjadala wa bajeti ya Wizara ya afya mjini Dodoma jana, Mnadhimu Mkuu wa kambi rasmi ya upinzani Bungeni, Tundu Lissu, alitumia nafasi hiyo kuishambulia serikali na kutaka iachane na sheria kandamizi dhidi ya vyombo vya habari.

Naye Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Julius Mtatiro, alisema serikali isije kudhani kutumia mabavu kwa vyombo vya habari kutasaidia kuficha maovu yake na kutaka uhuru wa vyombo vya habari upewe kipaumbele.

Jukwaa la Wahariri waja juu

Baadhi ya wadau wa habari akiwamo Katibu Mkuu wa Jukwaa la Wahariri (TEF), Neville Meena, alisema kuwa kitendo cha kulifungia gazeti la Mwanahalisi hakikubaliki, huku akihoji aliyelifungia ni nani na kwa utaratibu upi, kwa kipi na waziri anatoa wapi maamuzi ya kulifungia.

Meena pia alisema mfumo mzima una matatizo kwani mtu mmoja hawezi kutoa maamuzi na mahali pekee penye haki ni mahakamani, kwani ndipo sehemu watu wanapopambana na kupatikana aliyesimama kwenye haki.

“Hakuna haki wala uhuru wa habari, tunataka haki itendeke kwa wanaoandikiwa na wanaoandika, tutajuaje kama makosa waliyofungiwa yana ukweli na unasema tunalifungia muda usiojulikana ndiyo nini? Ungefuatwa utaratibu wa mahakama,” alisema.

Meena pia alisema TEF wanatarajia kutoa tamko leo kuhusiana na jambo hilo.

Mhariri Tanzania Daima aguswa

Naye Mhariri Mtendaji wa gazeti hili, Absalom Kibanda, alisema taarifa za serikali kulifungia gazeti hilo zilivuja na jambo hilo haliingii akilini kwani taifa limekuwa likizungumzia uhuru wa kujieleza.

Kibanda pia alisema kuwa sheria zilizopo ni kandamizi na kulifungia gazeti hilo ni hatua nyingine ya kukandamiza na kutishia, ikiwamo kuwanyima wanahabari haki yao na maelfu ya wananchi kupata habari kupitia Mwanahalisi.

“Kwanini wasitoe maelezo kuhusu Mwanahalisi lilifanya nini kuhusiana na kile kilichokuwa kikiandikwa? Mimi naona hata serikali haikuzingatia weledi, ikiwamo kutoa ufafanuzi na kwa stahili hii nasema Mwanahalisi iliigusa serikali pabaya,” alisema Kibanda.

Pia aliitaka serikali kutoingilia uhuru wa habari, ikiwamo kutambua gharama za demokrasia, isiinyime mawazo na kutambua kuwa ukinzani wa mawazo ndipo kwenye maendeleo.

TAMWA nao wacharuka

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake, Ananilea Nkya, alieleza kupitia mtandao wa mabadiliko kuwa hatua hiyo ya serikali ya kulifungia gazeti la Mwanahalisi badala ya kwenda mahakamani ni ishara kwamba yaliyoandikwa na gazeti hilo ni ukweli mtupu.

“Labda niulize swali moja tu, hivi mfalme akiambiwa yuko uchi, kama hajawa uchi ni kwa nini aamue kumuua/kumwadhibu aliyemwambia yuko uchi kabla ya yeye mfalme kuthibitisha kuwa hajawa uchi?,” alihoji.



Source: Tanzania Daima.




Walimu waliogoma kutolipwa mishahara

Mgomo waanza, watikisa kila kona ya nchi
WAKATI walimu wakianza mgomo wa kutoingia madarasani jana, serikali imesema kuwa walimu watakaobainika kujihusisha na mgomo huo hawatalipwa mishahara.

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa, alisema hayo jana wakati akitoa tamko la serikali kuhusu mgomo huo kwa waandishi wa habari.

Kwa mujibu wa Dk. Kawambwa, licha ya mwajiri kutowalipa mshahara walimu wote waliogoma watachukuliwa hatua kali huku wale wanaowatisha wenzao na kuwashirikisha wanafunzi kwenye mgomo, watawajibishwa.

Serikali pia imevitaka vyombo vya habari kuacha kuchochea mgomo huo kwa aina ya habari inazopeleka kwa umma, huku akisema kwamba si kazi ya vyombo hivyo kulibomoa taifa.

“Kwa mujibu wa sheria namba sita ya Ajira na Mahusiano Kazini ya mwaka 2004 ambayo mchakato wake ni mfupi, kifungu cha 83(4)g cha sheria hiyo, mwajiri hatalazimika kulipa mshahara kwa mtumishi aliyeshiriki katika mgomo kwa kipindi chote cha mgomo huo.

“Sheria ipo wazi, tutafanya hivyo kwa kipindi chote watakachokuwa kwenye mgomo… lakini pia kesi ipo mahakamani tayari na kesho mchana itatolewa hukumu,” alisema Dk. Kawambwa na kuongeza kwamba Chama cha Walimu Tanzania (CWT) kimefuata taratibu zote za mgomo huo.

Awali waziri huyo alisema serikali inaithamini elimu na walimu pia, haina sababu ya kushindwa kutatua kero zao ikiwemo ya kuwaongezea mishahara kwa asilimia 100; posho ya kufundishia kwa asilimia 55 ya mshahara walimu wa sayansi na asilimua 50 walimu wa sanaa.

“Walimu wanadai pia posho ya mazingira magumu ya kazi kwa asilimia 30 ya mshahara wao,” tunayo nia ya kufanya hayo lakini uwezo wa serikali ni mdogo ndiyo maana Juni 30 mwaka huu tuliweza kulipa sh bilioni 56 madai yao kwenye malimbikizo ya likizo na madai mengine ya walimu.

Dk. Kawambwa aliyepata kuwa waziri kwenye wizara nne tofauti katika utawala wa Awamu ya Nne, alisema juhudi za usuluhishi wa mgogoro huo zimekwama baada ya Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) kushindwa kufanya hivyo, hali iliyoilazimu serikali kukimbilia Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi.

“Baada ya CMA kushindwa pale walimu walipokataa nyongeza ya asilimia 14 ya mishahara yao tofauti na watumishi wengine wa serikali, ikasema itatoa cheti cha kushindwa kuleta suluhu kwenye mgogoro ule (Certificate of Deadlock).

“Julai 26 serikali iliwasilisha ombi la kuzuia mgomo uliotangazwa na CWT nchi nzima, Julai 27 serikali na CWT tulitakiwa kupeleka maelezo yetu kwa maandishi ambapo serikali iliamriwa kupeleka maelezo yake leo (Julai 30) na wenzetu wapeleke maelezo yao kesho (Julai 31) kabla ya kuanza kwa mgomo huo,” alisema Dk. Kawambwa ambaye ni Mbunge wa Bagamoyo.

Bila kueleza iwapo mahakama hiyo ilitoa amri ya kuzuia mgomo ama la, waziri huyo aliwataka waandishi wa habari kusubiri uamuzi wa mahakama utakaotolewa leo mchana.

Hali ya mgomo nchini

Licha ya serikali kutangaza kuwa mgomo wa walimu ni batili, walimu wa mikoa mbalimbali nchini wameanza rasmi mgomo huo.

Jijini Dar es Salaam, mwitiko wa mgomo huo ulikuwa mkubwa wakati katika mikoa ya Mbeya na Arusha Polisi wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) walilazimika kupiga mabomu ya machozi kuwatawanya wanafunzi waliokuwa wakiandamana kupinga mgomo wa walimu wao.

Jijini Dar es Salaam, wanafunzi wa shule mbalimbali walikuwa nje wakicheza wakati walimu wao walijikusanya kwenye vikundi kujadili mgomo huo bila kuingia madarasani.

Miongoni mwa shule hizo ni Shule ya Msingi Nzasa na Charambe wilayani Temeke, ambapo katika Shule ya Nzasa walifika walimu wawili licha ya shule hiyo kuwa na walimu 63 na katika Shule ya Msingi Charambe mwalimu aliyefika ni mmoja kati ya walimu 48.

Shule nyingine ambazo walimu wake waliingia kwenye mgomo kuanzia jana ni Shule ya Msingi na Sekondari ya Makumbusho Wilaya ya Kinondoni, ambapo mkuu wa Shule ya Sekondari Makumbusho alikataa kuzungumzia hali hiyo na kutaka atafutwe ofisa elimu ili atolee maelezo mgomo huo.

Wakizungumza na gazeti hili jana, baadhi ya wanafunzi katika shule hizo walisema mgomo huo una waathiri kwani baadhi yao wapo katika maandalizi ya mitihani ya taifa.

Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili, umebaini kuwa baadhi ya shule kulikuwa na walimu wachache.

Hali ilikuwa tofauti kwenye shule za Msingi Mnazi Mmoja, Buruguni, Bunge na nyingine zilizopo katikati ya Jiji la Dar es Salaam, ambapo walimu walikuwa wakiendelea kufundisha.

“Hatuoni sababu ya sisi kugoma ikizingatiwa kuwa madai ya mgomo huu hatuyajui, pia hatujashirikishwa,” walisema baadhi ya walimu hao walipozungumza na gazeti hili.

Shule nyingine zilizoguswa na mgomo huo ni Shule ya Msingi Malamba Mawili Mbezi, ambapo mwalimu mkuu wa shule hiyo, Leah Sanga, alieleza kushangazwa na baadhi ya walimu wake kutofika kabisa eneo lao la kazi.

“Shule ina wanafunzi zaidi ya 3,000 lakini nimefika peke yangu, kutokana na hali hiyo imenilazimu nikae nao kwa maelewano hadi saa 5 asubuhi ndipo nilipowaruhusu kurudi nyumbani,” alisema Mwalimu Sanga.

Shule za msingi Mbagala Kuu, Bwawani na Kijichi walimu wake pia hawakuingia madarasani.

Kutoka Mbeya, Mwandishi Gordon Kalulunga, anaripoti kuwa mgomo wa walimu jana ulitikisa baadhi ya shule za mjini humo.

Kwa mujibu wa habari hizo, wanafunzi wa shule nyingi mjini hapa walionekana wakicheza muda wote wa masomo, huku walimu wao wakiwa nje wakibadilishana mawazo.

Katika baadhi ya mitaa ya katikati ya Jiji la Mbeya, FFU walilazimika kutumia nguvu kuwatawanya wanafunzi waliokuwa wakiandamana kupinga mgomo huo.

Kutoka mjini Arusha, inaripotiwa kuwa baadhi ya shule zimeingia katika mgomo huo kwa walimu wao kugoma kuingia darasani.

Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili katika mikoa ya Iringa, Mwanza, Shinyanga na mikoa mingine, walimu wengi walifika mashuleni na kusaini kitabu cha mahudhurio, lakini hakuna aliyeingia darasani kufundisha.



Walimu waliogoma kutolipwa mishahara

Mgomo waanza, watikisa kila kona ya nchi
WAKATI walimu wakianza mgomo wa kutoingia madarasani jana, serikali imesema kuwa walimu watakaobainika kujihusisha na mgomo huo hawatalipwa mishahara.

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa, alisema hayo jana wakati akitoa tamko la serikali kuhusu mgomo huo kwa waandishi wa habari.

Kwa mujibu wa Dk. Kawambwa, licha ya mwajiri kutowalipa mshahara walimu wote waliogoma watachukuliwa hatua kali huku wale wanaowatisha wenzao na kuwashirikisha wanafunzi kwenye mgomo, watawajibishwa.

Serikali pia imevitaka vyombo vya habari kuacha kuchochea mgomo huo kwa aina ya habari inazopeleka kwa umma, huku akisema kwamba si kazi ya vyombo hivyo kulibomoa taifa.

“Kwa mujibu wa sheria namba sita ya Ajira na Mahusiano Kazini ya mwaka 2004 ambayo mchakato wake ni mfupi, kifungu cha 83(4)g cha sheria hiyo, mwajiri hatalazimika kulipa mshahara kwa mtumishi aliyeshiriki katika mgomo kwa kipindi chote cha mgomo huo.

“Sheria ipo wazi, tutafanya hivyo kwa kipindi chote watakachokuwa kwenye mgomo… lakini pia kesi ipo mahakamani tayari na kesho mchana itatolewa hukumu,” alisema Dk. Kawambwa na kuongeza kwamba Chama cha Walimu Tanzania (CWT) kimefuata taratibu zote za mgomo huo.

Awali waziri huyo alisema serikali inaithamini elimu na walimu pia, haina sababu ya kushindwa kutatua kero zao ikiwemo ya kuwaongezea mishahara kwa asilimia 100; posho ya kufundishia kwa asilimia 55 ya mshahara walimu wa sayansi na asilimua 50 walimu wa sanaa.

“Walimu wanadai pia posho ya mazingira magumu ya kazi kwa asilimia 30 ya mshahara wao,” tunayo nia ya kufanya hayo lakini uwezo wa serikali ni mdogo ndiyo maana Juni 30 mwaka huu tuliweza kulipa sh bilioni 56 madai yao kwenye malimbikizo ya likizo na madai mengine ya walimu.

Dk. Kawambwa aliyepata kuwa waziri kwenye wizara nne tofauti katika utawala wa Awamu ya Nne, alisema juhudi za usuluhishi wa mgogoro huo zimekwama baada ya Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) kushindwa kufanya hivyo, hali iliyoilazimu serikali kukimbilia Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi.

“Baada ya CMA kushindwa pale walimu walipokataa nyongeza ya asilimia 14 ya mishahara yao tofauti na watumishi wengine wa serikali, ikasema itatoa cheti cha kushindwa kuleta suluhu kwenye mgogoro ule (Certificate of Deadlock).

“Julai 26 serikali iliwasilisha ombi la kuzuia mgomo uliotangazwa na CWT nchi nzima, Julai 27 serikali na CWT tulitakiwa kupeleka maelezo yetu kwa maandishi ambapo serikali iliamriwa kupeleka maelezo yake leo (Julai 30) na wenzetu wapeleke maelezo yao kesho (Julai 31) kabla ya kuanza kwa mgomo huo,” alisema Dk. Kawambwa ambaye ni Mbunge wa Bagamoyo.

Bila kueleza iwapo mahakama hiyo ilitoa amri ya kuzuia mgomo ama la, waziri huyo aliwataka waandishi wa habari kusubiri uamuzi wa mahakama utakaotolewa leo mchana.

Hali ya mgomo nchini

Licha ya serikali kutangaza kuwa mgomo wa walimu ni batili, walimu wa mikoa mbalimbali nchini wameanza rasmi mgomo huo.

Jijini Dar es Salaam, mwitiko wa mgomo huo ulikuwa mkubwa wakati katika mikoa ya Mbeya na Arusha Polisi wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) walilazimika kupiga mabomu ya machozi kuwatawanya wanafunzi waliokuwa wakiandamana kupinga mgomo wa walimu wao.

Jijini Dar es Salaam, wanafunzi wa shule mbalimbali walikuwa nje wakicheza wakati walimu wao walijikusanya kwenye vikundi kujadili mgomo huo bila kuingia madarasani.

Miongoni mwa shule hizo ni Shule ya Msingi Nzasa na Charambe wilayani Temeke, ambapo katika Shule ya Nzasa walifika walimu wawili licha ya shule hiyo kuwa na walimu 63 na katika Shule ya Msingi Charambe mwalimu aliyefika ni mmoja kati ya walimu 48.

Shule nyingine ambazo walimu wake waliingia kwenye mgomo kuanzia jana ni Shule ya Msingi na Sekondari ya Makumbusho Wilaya ya Kinondoni, ambapo mkuu wa Shule ya Sekondari Makumbusho alikataa kuzungumzia hali hiyo na kutaka atafutwe ofisa elimu ili atolee maelezo mgomo huo.

Wakizungumza na gazeti hili jana, baadhi ya wanafunzi katika shule hizo walisema mgomo huo una waathiri kwani baadhi yao wapo katika maandalizi ya mitihani ya taifa.

Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili, umebaini kuwa baadhi ya shule kulikuwa na walimu wachache.

Hali ilikuwa tofauti kwenye shule za Msingi Mnazi Mmoja, Buruguni, Bunge na nyingine zilizopo katikati ya Jiji la Dar es Salaam, ambapo walimu walikuwa wakiendelea kufundisha.

“Hatuoni sababu ya sisi kugoma ikizingatiwa kuwa madai ya mgomo huu hatuyajui, pia hatujashirikishwa,” walisema baadhi ya walimu hao walipozungumza na gazeti hili.

Shule nyingine zilizoguswa na mgomo huo ni Shule ya Msingi Malamba Mawili Mbezi, ambapo mwalimu mkuu wa shule hiyo, Leah Sanga, alieleza kushangazwa na baadhi ya walimu wake kutofika kabisa eneo lao la kazi.

“Shule ina wanafunzi zaidi ya 3,000 lakini nimefika peke yangu, kutokana na hali hiyo imenilazimu nikae nao kwa maelewano hadi saa 5 asubuhi ndipo nilipowaruhusu kurudi nyumbani,” alisema Mwalimu Sanga.

Shule za msingi Mbagala Kuu, Bwawani na Kijichi walimu wake pia hawakuingia madarasani.

Kutoka Mbeya, Mwandishi Gordon Kalulunga, anaripoti kuwa mgomo wa walimu jana ulitikisa baadhi ya shule za mjini humo.

Kwa mujibu wa habari hizo, wanafunzi wa shule nyingi mjini hapa walionekana wakicheza muda wote wa masomo, huku walimu wao wakiwa nje wakibadilishana mawazo.

Katika baadhi ya mitaa ya katikati ya Jiji la Mbeya, FFU walilazimika kutumia nguvu kuwatawanya wanafunzi waliokuwa wakiandamana kupinga mgomo huo.

Kutoka mjini Arusha, inaripotiwa kuwa baadhi ya shule zimeingia katika mgomo huo kwa walimu wao kugoma kuingia darasani.

Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili katika mikoa ya Iringa, Mwanza, Shinyanga na mikoa mingine, walimu wengi walifika mashuleni na kusaini kitabu cha mahudhurio, lakini hakuna aliyeingia darasani kufundisha.



CHADEMA: Zitto achunguzwe • Lissu ataja wabunge wala rushwa

KAMBI rasmi ya Upinzani Bungeni imetaka kuchunguzwa kwa madai ya Naibu Kiongozi wa wa kambi hiyo, Zitto Kabwe, kuhongwa.

Kambi hiyo pia imetaja majina ya wabunge sita wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), waliokuwa wajumbe wa Kamati ya Nishati na Madini iliyovunjwa na Spika wa Bunge, Anne Makinda, mwishoni mwa wiki, ikidai kuwa kwa namna moja ama nyingine walihusika na vitendo vya rushwa.

Wabunge hao wanatuhumiwa kupokea rushwa kutoka kwa kampuni za mafuta ili kuipigia debe menejimenti ya Shirika la Ugavi wa umeme nchini (TANESCO).

Akizungumza jana na waandishi wa habari mjini hapa, Mnadhimu Mkuu wa kambi hiyo, Tundu Lissu, alisema wamesikia tuhuma nyingi dhidi ya Zitto lakini hawajamhoji kiongozi huyo.

Alisema wanaviomba vyombo vinavyohusika vimchunguze Zitto ili ukweli ujulikane na hatua zinazostahili zichukuliwe kama atathibitika kuwa na makosa.

“Chama hatujakaa na Zitto kumsikiliza lakini tunataka achunguzwe, hatuna masilahi yoyote katika uchafu huu wa rushwa.

“Uchunguzi huu utatupa msingi wa kumchukulia hatua kama chama ikiwa itathibitika amehongwa,” alisema.

Alibainisha kuwa, mbunge wao huyo amekuwa akihusishwa na kumtumia ujumbe mfupi wa vitisho Katibu Mkuu wa Nishati na Madini, Eliakimu Maswi.

Alisema ni vema Zitto achunguzwe na apewe nafasi ya kujieleza kama itakavyokuwa kwa wengine kuliko kuendelea kusambaza maneno ya kufikirika.

Alibainisha wamejiridhisha pasipo shaka kuwa wabunge wao watatu waliokuwa wajumbe kwenye Kamati ya Nishati na Madini, John Mnyika (Ubungo), David Silinde (Mbozi Magharibi) na Mwanamrisho Taratibu Abama (Viti Maalumu), hawajahusika kwa lolote katika sakata hilo la rushwa.

“Kama kuna mtu ana ushahidi zaidi ya huu tulionao tunaomba atuletee ili hatua zaidi ziweze kuchukuliwa, lakini mpaka sasa wabunge wetu hawa watatu hawajashiriki kwa lolote katika kuomba rushwa,” alisema.

Kauli ya Lissu inashabihiana na aliyoitoa Zitto juzi ambapo alisema hajachukua hongo, ila kuna watu wana lengo la kuchafua jina lake.

Zitto alisema kuwa uchunguzi dhidi yake ndiyo njia pekee ya kuudhihirishia umma kuwa hahusiki na chochote kama baadhi ya watu wanaoeneza maneno ya kumchafua.

Awataja wala rushwa

Kuhusu majina ya wabunge wanaotuhumiwa kujihusisha na vitendo vya rushwa, Lissu alisema kuwa kwa mujibu wa kanuni za kudumu za Bunge na Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma ya mwaka 1995, wabunge hao walipaswa kutaja masilahi yao kibiashara kwenye shirika hilo.

“Sasa wabunge hawa hawajawahi kufanya hivyo na wameendelea kuwa wajumbe wa Kamati ya Nishati na Madini na wengine kufanya biashara na TANESCO,” alisema Lissu na kuwataja kuwa ni Munde Tambwe, Sara Msafiri, Mariam Kisangi wa Viti Maalumu, Yusuf Nassir (Korogwe Mjini) na Charles Mwijage Muleba Kaskazini.

Lissu alifafanua kuwa Tambwe na Msafiri wana tenda ya kuiuzia TANESCO matairi na kwamba hawajawahi kutangaza masilahi yao katika jambo hilo kwenye kamati zao.

“Mwijage ni mtaalamu mwelekezi wa Kampuni ya PUMA Energy iliyopewa tenda na Maswi kuiuzia mafuta TANESCO, hivyo kama mjumbe wa Kamati ya Nishati ana mgongano wa kimasilahi. Nassir na Kisangi hawa wanafanya biashara ya mafuta wanamiliki vituo vya mafuta na wana mgongano,” alisema.

Kuhusu Christopher ole Sendeka, Lissu alidai kuwa amekuwa akizipigia debe kampuni tatu zilizonyimwa tenda ya kuiuzia mafuta TANESCO akiwashawishi wajumbe wa kamati kuwa serikali ilikiuka kanuni kuipa tenda Kampuni ya PUMA Energy.

Mbunge mwingine aliyetajwa ni Vicky Kamata wa Viti Maalumu ambaye alidaiwa kuwa na mgongano wa kimasilahi na Maswi.

“Tunampongeza Spika kwa kuivunja Kamati ya Nishati na Madini lakini tunataka azivunje pia zile za LAAC, inayoongozwa na Augustine Mrema (TLP) na POAC ya Zitto, kwa kuwa baadhi ya wajumbe wake wamekuwa wakitajwa sana kujihusisha na vitendo vya rushwa.

Fukuto la kutajwa kwa majina ya wabunge wanaotuhumiwa kwa rushwa lilitawala mjadala wa Bunge jana, ambapo wabunge, Kangi Lugora (Mwibara), James Mbatia (Kuteuliwa), Ali Keisy (Nkasi), Joshua Nassari (Arumeru Mashariki na Salum Baruani (Lindi Mjini), waliomba mwongozo wa Spika wakidai wahusika wawekwe wazi.

Hata hivyo, katika mwongozo wake, Naibu Spika, Job Ndugai, alisema kuwa Kamati ya Maadili, Haki na Madaraka ya Bunge inaendelea na uchunguzi kama ilivyoagizwa na Spika ndipo hatua nyingine zitafuata.

“Wabunge, baadhi mtaitwa kusaidia kamati hiyo lakini si kwamba ukiitwa kuhojiwa na kamati inamaanisha umepokea rushwa, ni katika hatua za mwanzo tu kufikia ukweli wa kile kinachochunguzwa. Labda niwaeleze kuwa Spika amekubali kuiangalia kamati hii ili wale wajumbe wenye mgongano wa kimasilahi waondolewe,” alisema.

Alikataa kutaja majina ya watuhumiwa akisema kuwa Spika pamoja na yeye hawawajui wahusika ndiyo maana wanachunguza kuwabaini. Lakini aligusia kuwa Taasisi ya Kuzuia na kupambana na Rushwa (TAKUKURU), imeanza kuwahoji baadhi ya wabunge.

Ndugai pia alitolea ufafanuzi mwongozo ulioombwa na Mbunge wa Tabora Mjini, Ismail Rage (CCM), aliyetaka kujua ni kwanini kiongozi wa upinzani alitaja majina ya watuhumiwa wa rushwa kutoka CCM wakati kwenye chama chake cha CHADEMA kuna watuhumiwa pia.

“Mimi ningewashauri kuwa katika jambo hili tuwe na subira na tukitaka kulizungumza tutende haki kwa pande zote, maana hakuna chama chenye sera ya kura rushwa, tusilifanye kisiasa kwa kuoneana,” alisema Ndugai.

Watuhumiwa wajitetea

Tanzania Daima iliwasiliana na watuhumiwa kujua wana kauli gani dhidi ya tuhuma hizo ambapo Mwijage, Msafiri na Munde simu zao ziliita pasipo kupokewa wakati Ole Sendeka, Kisangi na Nassir walizikanusha.

Nassir alisema kuwa si kweli kuwa anafanya biashara ya mafuta bali aliwahi kufanya kazi katika Shirika la Maendeleo ya Petroli (TPDC) ambapo alipata ujuzi na hivyo kuwa na nia ya kutaka kuanza biashara ya gesi.

“Lissu ni mwanasheria lakini nashindwa kuelewa ni kwanini anafanya ‘generalization’ katika jambo hili, mimi sifanyi biashara ya mafuta na TANESCO wala serikali kupitia wizara husika, nampuuza kwa madai yake na nitamchukulia hatua,” alisema.

Kwa upande wake Kisangi alikiri kufanya biashara ya mafuta, akisema anamiliki vituo vya mafuta eneo la Mbagala Rangi Tatu, lakini akafafanua kuwa kila wakati alipochangia hoja ndani ya Bunge na kwenye Kamati ya Nishati na Madini alitangaza masilahi yake.

“Mimi niko vizuri sina wasiwasi, rejea kumbukumbu rasmi za Bunge utaona kuwa nimetangaza masilahi yangu, hivyo namshangaa huyu mwanasheria. Ina maana naye kuwa kwenye Kamati ya Sheria ni mgongano wa masilahi kwa vile ni mwanasheria?” alihoji.

Ole Sendeka naye alisema kuwa hakuwahi kuzipigia debe kampuni anazohusishwa nazo kwani alichokifanya kwenye kamati ni kuwaeleza wajumbe namna Maswi alivyovunja sheria ya manunuzi ya umma.

“Maswi ameichukua PUMA Energy kama mashati ya mitumba sokoni wala haikuwa kushindanishwa, sasa kama Lissu ambaye ni mwanasheria haoni hilo napata taabu,” alisema.

CHADEMA: Zitto achunguzwe • Lissu ataja wabunge wala rushwa

KAMBI rasmi ya Upinzani Bungeni imetaka kuchunguzwa kwa madai ya Naibu Kiongozi wa wa kambi hiyo, Zitto Kabwe, kuhongwa.

Kambi hiyo pia imetaja majina ya wabunge sita wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), waliokuwa wajumbe wa Kamati ya Nishati na Madini iliyovunjwa na Spika wa Bunge, Anne Makinda, mwishoni mwa wiki, ikidai kuwa kwa namna moja ama nyingine walihusika na vitendo vya rushwa.

Wabunge hao wanatuhumiwa kupokea rushwa kutoka kwa kampuni za mafuta ili kuipigia debe menejimenti ya Shirika la Ugavi wa umeme nchini (TANESCO).

Akizungumza jana na waandishi wa habari mjini hapa, Mnadhimu Mkuu wa kambi hiyo, Tundu Lissu, alisema wamesikia tuhuma nyingi dhidi ya Zitto lakini hawajamhoji kiongozi huyo.

Alisema wanaviomba vyombo vinavyohusika vimchunguze Zitto ili ukweli ujulikane na hatua zinazostahili zichukuliwe kama atathibitika kuwa na makosa.

“Chama hatujakaa na Zitto kumsikiliza lakini tunataka achunguzwe, hatuna masilahi yoyote katika uchafu huu wa rushwa.

“Uchunguzi huu utatupa msingi wa kumchukulia hatua kama chama ikiwa itathibitika amehongwa,” alisema.

Alibainisha kuwa, mbunge wao huyo amekuwa akihusishwa na kumtumia ujumbe mfupi wa vitisho Katibu Mkuu wa Nishati na Madini, Eliakimu Maswi.

Alisema ni vema Zitto achunguzwe na apewe nafasi ya kujieleza kama itakavyokuwa kwa wengine kuliko kuendelea kusambaza maneno ya kufikirika.

Alibainisha wamejiridhisha pasipo shaka kuwa wabunge wao watatu waliokuwa wajumbe kwenye Kamati ya Nishati na Madini, John Mnyika (Ubungo), David Silinde (Mbozi Magharibi) na Mwanamrisho Taratibu Abama (Viti Maalumu), hawajahusika kwa lolote katika sakata hilo la rushwa.

“Kama kuna mtu ana ushahidi zaidi ya huu tulionao tunaomba atuletee ili hatua zaidi ziweze kuchukuliwa, lakini mpaka sasa wabunge wetu hawa watatu hawajashiriki kwa lolote katika kuomba rushwa,” alisema.

Kauli ya Lissu inashabihiana na aliyoitoa Zitto juzi ambapo alisema hajachukua hongo, ila kuna watu wana lengo la kuchafua jina lake.

Zitto alisema kuwa uchunguzi dhidi yake ndiyo njia pekee ya kuudhihirishia umma kuwa hahusiki na chochote kama baadhi ya watu wanaoeneza maneno ya kumchafua.

Awataja wala rushwa

Kuhusu majina ya wabunge wanaotuhumiwa kujihusisha na vitendo vya rushwa, Lissu alisema kuwa kwa mujibu wa kanuni za kudumu za Bunge na Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma ya mwaka 1995, wabunge hao walipaswa kutaja masilahi yao kibiashara kwenye shirika hilo.

“Sasa wabunge hawa hawajawahi kufanya hivyo na wameendelea kuwa wajumbe wa Kamati ya Nishati na Madini na wengine kufanya biashara na TANESCO,” alisema Lissu na kuwataja kuwa ni Munde Tambwe, Sara Msafiri, Mariam Kisangi wa Viti Maalumu, Yusuf Nassir (Korogwe Mjini) na Charles Mwijage Muleba Kaskazini.

Lissu alifafanua kuwa Tambwe na Msafiri wana tenda ya kuiuzia TANESCO matairi na kwamba hawajawahi kutangaza masilahi yao katika jambo hilo kwenye kamati zao.

“Mwijage ni mtaalamu mwelekezi wa Kampuni ya PUMA Energy iliyopewa tenda na Maswi kuiuzia mafuta TANESCO, hivyo kama mjumbe wa Kamati ya Nishati ana mgongano wa kimasilahi. Nassir na Kisangi hawa wanafanya biashara ya mafuta wanamiliki vituo vya mafuta na wana mgongano,” alisema.

Kuhusu Christopher ole Sendeka, Lissu alidai kuwa amekuwa akizipigia debe kampuni tatu zilizonyimwa tenda ya kuiuzia mafuta TANESCO akiwashawishi wajumbe wa kamati kuwa serikali ilikiuka kanuni kuipa tenda Kampuni ya PUMA Energy.

Mbunge mwingine aliyetajwa ni Vicky Kamata wa Viti Maalumu ambaye alidaiwa kuwa na mgongano wa kimasilahi na Maswi.

“Tunampongeza Spika kwa kuivunja Kamati ya Nishati na Madini lakini tunataka azivunje pia zile za LAAC, inayoongozwa na Augustine Mrema (TLP) na POAC ya Zitto, kwa kuwa baadhi ya wajumbe wake wamekuwa wakitajwa sana kujihusisha na vitendo vya rushwa.

Fukuto la kutajwa kwa majina ya wabunge wanaotuhumiwa kwa rushwa lilitawala mjadala wa Bunge jana, ambapo wabunge, Kangi Lugora (Mwibara), James Mbatia (Kuteuliwa), Ali Keisy (Nkasi), Joshua Nassari (Arumeru Mashariki na Salum Baruani (Lindi Mjini), waliomba mwongozo wa Spika wakidai wahusika wawekwe wazi.

Hata hivyo, katika mwongozo wake, Naibu Spika, Job Ndugai, alisema kuwa Kamati ya Maadili, Haki na Madaraka ya Bunge inaendelea na uchunguzi kama ilivyoagizwa na Spika ndipo hatua nyingine zitafuata.

“Wabunge, baadhi mtaitwa kusaidia kamati hiyo lakini si kwamba ukiitwa kuhojiwa na kamati inamaanisha umepokea rushwa, ni katika hatua za mwanzo tu kufikia ukweli wa kile kinachochunguzwa. Labda niwaeleze kuwa Spika amekubali kuiangalia kamati hii ili wale wajumbe wenye mgongano wa kimasilahi waondolewe,” alisema.

Alikataa kutaja majina ya watuhumiwa akisema kuwa Spika pamoja na yeye hawawajui wahusika ndiyo maana wanachunguza kuwabaini. Lakini aligusia kuwa Taasisi ya Kuzuia na kupambana na Rushwa (TAKUKURU), imeanza kuwahoji baadhi ya wabunge.

Ndugai pia alitolea ufafanuzi mwongozo ulioombwa na Mbunge wa Tabora Mjini, Ismail Rage (CCM), aliyetaka kujua ni kwanini kiongozi wa upinzani alitaja majina ya watuhumiwa wa rushwa kutoka CCM wakati kwenye chama chake cha CHADEMA kuna watuhumiwa pia.

“Mimi ningewashauri kuwa katika jambo hili tuwe na subira na tukitaka kulizungumza tutende haki kwa pande zote, maana hakuna chama chenye sera ya kura rushwa, tusilifanye kisiasa kwa kuoneana,” alisema Ndugai.

Watuhumiwa wajitetea

Tanzania Daima iliwasiliana na watuhumiwa kujua wana kauli gani dhidi ya tuhuma hizo ambapo Mwijage, Msafiri na Munde simu zao ziliita pasipo kupokewa wakati Ole Sendeka, Kisangi na Nassir walizikanusha.

Nassir alisema kuwa si kweli kuwa anafanya biashara ya mafuta bali aliwahi kufanya kazi katika Shirika la Maendeleo ya Petroli (TPDC) ambapo alipata ujuzi na hivyo kuwa na nia ya kutaka kuanza biashara ya gesi.

“Lissu ni mwanasheria lakini nashindwa kuelewa ni kwanini anafanya ‘generalization’ katika jambo hili, mimi sifanyi biashara ya mafuta na TANESCO wala serikali kupitia wizara husika, nampuuza kwa madai yake na nitamchukulia hatua,” alisema.

Kwa upande wake Kisangi alikiri kufanya biashara ya mafuta, akisema anamiliki vituo vya mafuta eneo la Mbagala Rangi Tatu, lakini akafafanua kuwa kila wakati alipochangia hoja ndani ya Bunge na kwenye Kamati ya Nishati na Madini alitangaza masilahi yake.

“Mimi niko vizuri sina wasiwasi, rejea kumbukumbu rasmi za Bunge utaona kuwa nimetangaza masilahi yangu, hivyo namshangaa huyu mwanasheria. Ina maana naye kuwa kwenye Kamati ya Sheria ni mgongano wa masilahi kwa vile ni mwanasheria?” alihoji.

Ole Sendeka naye alisema kuwa hakuwahi kuzipigia debe kampuni anazohusishwa nazo kwani alichokifanya kwenye kamati ni kuwaeleza wajumbe namna Maswi alivyovunja sheria ya manunuzi ya umma.

“Maswi ameichukua PUMA Energy kama mashati ya mitumba sokoni wala haikuwa kushindanishwa, sasa kama Lissu ambaye ni mwanasheria haoni hilo napata taabu,” alisema.

Monday, July 30, 2012

Dk. Ulimboka kuliteka Bunge

SAKATA la kutekwa, kuteswa na kuumizwa kwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari nchini, Dk. Steven Ulimboka, na mgogoro wa madaktari ni miongoni mwa mambo yanayotarajiwa kuliteka Bunge leo.
Suala hilo licha ya kuzuia kujadiliwa bungeni kwa madai kuwa kesi yake iko mahakamani, idadi kubwa ya wabunge imeonyesha kiu ya kulijadili.
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Husein Mwinyi, leo anatarajia kuwasilisha hotuba ya bajeti yake kwa mwaka wa fedha 2012/2013.
Dk. Mwinyi na Naibu wake Dk. Rashid Seif waliteuliwa na Rais Jakaya Kikwete kuongoza wizara hiyo miezi miwili iliyopita wakichukua nafasi za Dk. Haji Mponda na Dk. Lucy Nkya, walioondolewa kwa madai ya kushindwa kuwajibika ipasavyo.
Mponda na Nkya, walidaiwa kushindwa kushughulikia matatizo yanayoikabili sekta ya afya hivyo kuwafanya madaktari wafanye mgomo mwanzoni mwa mwaka huu.
Katika madai yao madaktari walikuwa wakitaka watendaji wakuu wa wizara hiyo waondolewe kwenye nafasi zao ndipo wazungumze na serikali.
Sharti hilo lilitekelezwa na serikali ambapo iliwaondoa madarakani Katibu Mkuu, Blandina Nyoni na Mganga Mkuu wa Serikali, Dk. Deo Mtasiwa, huku uchunguzi dhidi ya tuhuma zao ukiendelea mpaka sasa.
Waziri Mwinyi atakuwa na kibarua kizito kwa wabunge kwani mbali na kutakiwa kueleza hatua zilizochukuliwa kwa watuhumiwa hao, pia Bunge litapaswa kuelezwa hatua zilizofikiwa na serikali katika kutatua mgogoro wa madaktari hasa utekelezaji wa madai yao 10 yaliyosababisha wagome mara tatu na kuleta madhara kwa wagonjwa.
Sakata la Dk. Ulimboka lilitokea usiku wa Juni 28, siku mbili baada ya madaktari kuanza mgomo jambo lililowafanya baadhi ya watu kuvihusisha vyombo vya dola.
Hata hivyo viongozi mbalimbali akiwemo Rais Jakaya Kikwete walikana serikali kuhusika nalo.
Wabunge wang’ang’ania
Licha ya viongozi wa Bunge kudai suala hilo liko mahakamani na mtu mmoja ameshakamatwa, wabunge wengi wameonekana kupinga jambo hilo kwa madai kuna hila ya kuwazuia kulijadili.
Miongoni mwa wabunge wanaoonekana kuwa na kiu ya kutaka kulizungumzia suala la Dk. Ulimboka ni mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’, ambaye wiki iliyopita alisema sinema ya Dk. Ulimboka haijaeleweka katika jamii.
Kauli ya mbunge huyo ilikuwa kijembe kwa Jeshi la Polisi ambalo lilitangaza kumkamata mtuhumiwa wa tukio hilo na kumfikisha mahakamani.
Suala hilo huenda likazua malumbano makali bungeni hasa kutokana na hatua ya serikali kuwafutia leseni madaktari walioshiriki kwenye mgomo hivi karibuni.
Baadhi ya wabunge waliozungumza na gazeti hili mjini hapa jana, walisema kuwa wanataka serikali itoe ufafanuzi ni kwa nini imewafutia leseni madaktari wanafunzi kwa vitendo “interns” wakati ikielewa fika kuwa sekta hiyo inakabiliwa na uhaba mkubwa wa watumishi.
Ripoti ya mgomo yatakiwa
Mbunge Ubungo, John Mnyika (CHADEMA), amewataka wadau mbalimbali wa sekta ya afya nchini kuungana kutaka ripoti ya Kamati ya Bunge Huduma za Jamii iliyoshughukia suala la mgomo wa madaktari iwasilishwe bungeni na itumike kama hadidu rejea wakati wa kujadili suala zima la mgomo wa madaktari.
Mnyika alisema maelezo yaliyotolewa bungeni na Naibu Spika, Job Ndugai, kuwa taarifa hiyo iliwasilishwa bungeni hayakuwa ya kweli kwa kuwa wabunge hawajapewa nakala ya taarifa hiyo na kwamba bado inaendelea kufanywa siri.
Alisema tabia ya viongozi wa Bunge kuzuia mijadala mbali mbali kwa kigezo kuwa kesi ziko mahakamani ni kutowatendea wananchi haki.
“Kesho na keshokutwa Bunge litajadili Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, kwa mwaka wa fedha 2012/2013, kwa zaidi ya miezi mitatu Bunge limekuwa likizuiwa kutumia haki, uhuru na madaraka yake kwa mujibu wa ibara za 63 na 100 za Katiba ya nchi kuisimamia serikali kwa niaba ya wananchi kuhusu hali ya sekta ya afya nchini na migogoro kati ya serikali na madaktari.”
“Bunge linapaswa kutumia madaraka yake vema kujadili mustakabali wa maisha ya Watanzania ili iweze kujua chanzo cha mgogoro ulioendelea kati ya serikali na madaktari ili iweze kutoa ushauri wa namna ya kuzuia wakati mwingine isijirudie.”

Dk. Ulimboka kuliteka Bunge

SAKATA la kutekwa, kuteswa na kuumizwa kwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari nchini, Dk. Steven Ulimboka, na mgogoro wa madaktari ni miongoni mwa mambo yanayotarajiwa kuliteka Bunge leo.
Suala hilo licha ya kuzuia kujadiliwa bungeni kwa madai kuwa kesi yake iko mahakamani, idadi kubwa ya wabunge imeonyesha kiu ya kulijadili.
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Husein Mwinyi, leo anatarajia kuwasilisha hotuba ya bajeti yake kwa mwaka wa fedha 2012/2013.
Dk. Mwinyi na Naibu wake Dk. Rashid Seif waliteuliwa na Rais Jakaya Kikwete kuongoza wizara hiyo miezi miwili iliyopita wakichukua nafasi za Dk. Haji Mponda na Dk. Lucy Nkya, walioondolewa kwa madai ya kushindwa kuwajibika ipasavyo.
Mponda na Nkya, walidaiwa kushindwa kushughulikia matatizo yanayoikabili sekta ya afya hivyo kuwafanya madaktari wafanye mgomo mwanzoni mwa mwaka huu.
Katika madai yao madaktari walikuwa wakitaka watendaji wakuu wa wizara hiyo waondolewe kwenye nafasi zao ndipo wazungumze na serikali.
Sharti hilo lilitekelezwa na serikali ambapo iliwaondoa madarakani Katibu Mkuu, Blandina Nyoni na Mganga Mkuu wa Serikali, Dk. Deo Mtasiwa, huku uchunguzi dhidi ya tuhuma zao ukiendelea mpaka sasa.
Waziri Mwinyi atakuwa na kibarua kizito kwa wabunge kwani mbali na kutakiwa kueleza hatua zilizochukuliwa kwa watuhumiwa hao, pia Bunge litapaswa kuelezwa hatua zilizofikiwa na serikali katika kutatua mgogoro wa madaktari hasa utekelezaji wa madai yao 10 yaliyosababisha wagome mara tatu na kuleta madhara kwa wagonjwa.
Sakata la Dk. Ulimboka lilitokea usiku wa Juni 28, siku mbili baada ya madaktari kuanza mgomo jambo lililowafanya baadhi ya watu kuvihusisha vyombo vya dola.
Hata hivyo viongozi mbalimbali akiwemo Rais Jakaya Kikwete walikana serikali kuhusika nalo.
Wabunge wang’ang’ania
Licha ya viongozi wa Bunge kudai suala hilo liko mahakamani na mtu mmoja ameshakamatwa, wabunge wengi wameonekana kupinga jambo hilo kwa madai kuna hila ya kuwazuia kulijadili.
Miongoni mwa wabunge wanaoonekana kuwa na kiu ya kutaka kulizungumzia suala la Dk. Ulimboka ni mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’, ambaye wiki iliyopita alisema sinema ya Dk. Ulimboka haijaeleweka katika jamii.
Kauli ya mbunge huyo ilikuwa kijembe kwa Jeshi la Polisi ambalo lilitangaza kumkamata mtuhumiwa wa tukio hilo na kumfikisha mahakamani.
Suala hilo huenda likazua malumbano makali bungeni hasa kutokana na hatua ya serikali kuwafutia leseni madaktari walioshiriki kwenye mgomo hivi karibuni.
Baadhi ya wabunge waliozungumza na gazeti hili mjini hapa jana, walisema kuwa wanataka serikali itoe ufafanuzi ni kwa nini imewafutia leseni madaktari wanafunzi kwa vitendo “interns” wakati ikielewa fika kuwa sekta hiyo inakabiliwa na uhaba mkubwa wa watumishi.
Ripoti ya mgomo yatakiwa
Mbunge Ubungo, John Mnyika (CHADEMA), amewataka wadau mbalimbali wa sekta ya afya nchini kuungana kutaka ripoti ya Kamati ya Bunge Huduma za Jamii iliyoshughukia suala la mgomo wa madaktari iwasilishwe bungeni na itumike kama hadidu rejea wakati wa kujadili suala zima la mgomo wa madaktari.
Mnyika alisema maelezo yaliyotolewa bungeni na Naibu Spika, Job Ndugai, kuwa taarifa hiyo iliwasilishwa bungeni hayakuwa ya kweli kwa kuwa wabunge hawajapewa nakala ya taarifa hiyo na kwamba bado inaendelea kufanywa siri.
Alisema tabia ya viongozi wa Bunge kuzuia mijadala mbali mbali kwa kigezo kuwa kesi ziko mahakamani ni kutowatendea wananchi haki.
“Kesho na keshokutwa Bunge litajadili Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, kwa mwaka wa fedha 2012/2013, kwa zaidi ya miezi mitatu Bunge limekuwa likizuiwa kutumia haki, uhuru na madaraka yake kwa mujibu wa ibara za 63 na 100 za Katiba ya nchi kuisimamia serikali kwa niaba ya wananchi kuhusu hali ya sekta ya afya nchini na migogoro kati ya serikali na madaktari.”
“Bunge linapaswa kutumia madaraka yake vema kujadili mustakabali wa maisha ya Watanzania ili iweze kujua chanzo cha mgogoro ulioendelea kati ya serikali na madaktari ili iweze kutoa ushauri wa namna ya kuzuia wakati mwingine isijirudie.”

Rushwa Bungeni yatia doa taifa


KITENDO cha Bunge kukabiliwa na tuhuma za rushwa kutokana na baadhi ya wabunge kudaiwa kuhusika pamoja na kutetea ufisadi katika Shirika la Umeme (Tanesco), kimetajwa kuwa ni hatari kwa nchi na zinahitajika hatua za haraka kuwawajibisha wahusika.

Kutokana na tuhuma hizo za kuhongwa na kujiingiza katika vitendo vya rushwa kwa baadhi ya wabunge, watu wa kada tofauti wakiwemo wasomi waliozungumza na gazeti hili, baadhi yao wameshauri itungwe sheria ya kuwasimamisha ubunge watakaobainika kujihusisha na rushwa, kutetea uozo na mafisadi.

Aidha, viongozi wa chama wamesema hawatasita kuwachukulia hatua wanachama wao wabunge watakaobainika katika sakata hilo.

Hata hivyo, ipo Sheria ya Kinga na Madaraka ya Bunge ambapo wanaobainika kuhusika kupokea rushwa, wanaweza kuadhibiwa kwa kufukuzwa bungeni au kufungwa miaka mitatu jela.

Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Idara ya Sayansi ya Siasa na Utawala, Dk Benson Bana aliyesema yanayojitokeza bungeni kuhusu tuhuma za rushwa na kuhongwa, inadhihirisha wazi kuwa jamii ya watanzania ina mmomonyoko mkubwa wa maadili.

“Chombo kikubwa kama hiki kinatuhumiwa kuhusika na rushwa tena si mara moja, ni hatari kabisa kwa nchi yetu na si jambo zuri na inaonesha wazi kuwa baadhi ya wabunge hawana uadilifu,” alisema Dk Bana.

Alisema inafahamika wazi kuwa Bunge ni sehemu ya jamii hivyo kinachotendeka ndani ya chombo hicho kina akisi namna jamii ya kitanzania ilivyo, jambo ambalo linaibebesha sifa mbaya Tanzania.

Hata hivyo, alimpongeza Spika wa Bunge Anne Makinda kwa kuvunja Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini.

Alimpongeza pia Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila (NCCR-Mageuzi) kwa kujitoa katika kamati yake ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa baada ya baadhi ya wajumbe wake kutuhumiwa kujihusisha na vitendo vya rushwa.

“Ndio maana katika kulitafutia ufumbuzi jambo hili, nashauri iundwe Sheria itakayombana mbunge yeyote atakayethibitika kula rushwa au kutetea waziwazi uozo na kukumbatia ufisadi na ikiwezekana adhabu iwe kufukuzwa kabisa ubunge,” alisisitiza.

Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Itikadi na Uenezi ya CCM, Nape Nnauye, alisema chama hicho hakitosita kumchukulia hatua mbunge yeyote wa chama hicho atakayebainika kuhusika na rushwa au kuhongwa kutetea jambo lisilo na manufaa kwa Watanzania.

“Nimesikitika kuona tuhuma za baadhi ya wabunge wetu kuhongwa ili wafanye maamuzi ndivyo sivyo( bila kujali itikadi zao) zinaongezeka kila kukicha. Kama hawa wanaomudu kupata walau mahitaji muhimu ya binadamu kwa kipato chao halali wanahongwa, vipi watumishi ambao mshahara wao wa mwezi ni posho ya mbunge ya siku moja wafanyeje? Tunakwenda wapi?,” alihoji Nape.

Naye Mhadhiri wa Sayansi ya Siasa wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT), Profesa Mwesiga Baregu, alitaka suala hilo la tuhuma za hongo na rushwa kwa wabunge lichukuliwe hatua zaidi kwa kuchunguzwa ili kubainika ukweli ulipo.

Akitoa maoni yake Waziri Kivuli wa Wizara ya Nishati na Madini, John Mnyika, alisema uamuzi wa Spika kuvunja kamati ya nishati ni sahihi lakini amechelewa.

Hata hivyo, Mnyika alisema uamuzi huo pekee hauwezi kurejesha heshima ya Bunge hilo wala kushughulikia uzembe na udhaifu ulioko ndani ya chombo hicho na kwenye serikali ikiwa hautaambatana na hatua nyingine za ziada na za haraka.

Aidha alitaka Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge imalize kazi yake kwa dharura ili majina ya wahusika yatajwe ndani ya Bunge na Bunge lijadili kupitisha maazimio ya hatua za ziada za kuchukuliwa na vyombo huru vya kiuchunguzi na hatimaye watakaothibitika kuvunja sheria wafikishwe mahakamani.

“Pamoja na hatua hizo, Kamati za vyama nazo zichukue hatua kwa wabunge wake watakaotajwa ili kudumisha misingi ya uadilifu na uwajibikaji kwa maslahi ya umma,” alisema Mnyika.

Pia Mnyika alisema uzembe mwingine na kashfa za wabunge zisingeendelea kutokea iwapo Bunge hilo lingeyafanyia kazi mapendekezo yanayotolewa ndani ya Bunge hilo, akitolea mfano mapendekezo ya sakata la Richmond na sakata la aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Jairo.

Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk Edward Hoseah alipoulizwa kuhusu namna ambavyo taasisi yake inafanyia kazi tuhuma hizo zilizoibuliwa bungeni, alimtaka mwandishi wa habari hizi aandike anavyotaka.

“Nyie waandishi mna matatizo kila siku kwenye vipindi vyetu tunatangaza kuwa tunapata taarifa kupitia maeneo mbalimbali, na kuzifanyia kazi, sasa unanipigia simu na kuniuliza hili ili nisemeje, unataka nikujibu nini?” alihoji.

Juzi bungeni Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo alibainisha kuwa wapo baadhi ya wabunge wamehongwa ili kumwajibisha yeye na Katibu Mkuu wake Eliakim Maswi na kuwafananisha wabunge hao kama Mobutu.

Pamoja na hayo, Profesa Muhongo alianika bungeni humo kuwa yupo mmoja wa wabunge ambaye ni mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini amekuwa akifanya biashara na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kwa kuliuzia matairi chini ya viwango.

Rushwa Bungeni yatia doa taifa


KITENDO cha Bunge kukabiliwa na tuhuma za rushwa kutokana na baadhi ya wabunge kudaiwa kuhusika pamoja na kutetea ufisadi katika Shirika la Umeme (Tanesco), kimetajwa kuwa ni hatari kwa nchi na zinahitajika hatua za haraka kuwawajibisha wahusika.

Kutokana na tuhuma hizo za kuhongwa na kujiingiza katika vitendo vya rushwa kwa baadhi ya wabunge, watu wa kada tofauti wakiwemo wasomi waliozungumza na gazeti hili, baadhi yao wameshauri itungwe sheria ya kuwasimamisha ubunge watakaobainika kujihusisha na rushwa, kutetea uozo na mafisadi.

Aidha, viongozi wa chama wamesema hawatasita kuwachukulia hatua wanachama wao wabunge watakaobainika katika sakata hilo.

Hata hivyo, ipo Sheria ya Kinga na Madaraka ya Bunge ambapo wanaobainika kuhusika kupokea rushwa, wanaweza kuadhibiwa kwa kufukuzwa bungeni au kufungwa miaka mitatu jela.

Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Idara ya Sayansi ya Siasa na Utawala, Dk Benson Bana aliyesema yanayojitokeza bungeni kuhusu tuhuma za rushwa na kuhongwa, inadhihirisha wazi kuwa jamii ya watanzania ina mmomonyoko mkubwa wa maadili.

“Chombo kikubwa kama hiki kinatuhumiwa kuhusika na rushwa tena si mara moja, ni hatari kabisa kwa nchi yetu na si jambo zuri na inaonesha wazi kuwa baadhi ya wabunge hawana uadilifu,” alisema Dk Bana.

Alisema inafahamika wazi kuwa Bunge ni sehemu ya jamii hivyo kinachotendeka ndani ya chombo hicho kina akisi namna jamii ya kitanzania ilivyo, jambo ambalo linaibebesha sifa mbaya Tanzania.

Hata hivyo, alimpongeza Spika wa Bunge Anne Makinda kwa kuvunja Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini.

Alimpongeza pia Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila (NCCR-Mageuzi) kwa kujitoa katika kamati yake ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa baada ya baadhi ya wajumbe wake kutuhumiwa kujihusisha na vitendo vya rushwa.

“Ndio maana katika kulitafutia ufumbuzi jambo hili, nashauri iundwe Sheria itakayombana mbunge yeyote atakayethibitika kula rushwa au kutetea waziwazi uozo na kukumbatia ufisadi na ikiwezekana adhabu iwe kufukuzwa kabisa ubunge,” alisisitiza.

Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Itikadi na Uenezi ya CCM, Nape Nnauye, alisema chama hicho hakitosita kumchukulia hatua mbunge yeyote wa chama hicho atakayebainika kuhusika na rushwa au kuhongwa kutetea jambo lisilo na manufaa kwa Watanzania.

“Nimesikitika kuona tuhuma za baadhi ya wabunge wetu kuhongwa ili wafanye maamuzi ndivyo sivyo( bila kujali itikadi zao) zinaongezeka kila kukicha. Kama hawa wanaomudu kupata walau mahitaji muhimu ya binadamu kwa kipato chao halali wanahongwa, vipi watumishi ambao mshahara wao wa mwezi ni posho ya mbunge ya siku moja wafanyeje? Tunakwenda wapi?,” alihoji Nape.

Naye Mhadhiri wa Sayansi ya Siasa wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT), Profesa Mwesiga Baregu, alitaka suala hilo la tuhuma za hongo na rushwa kwa wabunge lichukuliwe hatua zaidi kwa kuchunguzwa ili kubainika ukweli ulipo.

Akitoa maoni yake Waziri Kivuli wa Wizara ya Nishati na Madini, John Mnyika, alisema uamuzi wa Spika kuvunja kamati ya nishati ni sahihi lakini amechelewa.

Hata hivyo, Mnyika alisema uamuzi huo pekee hauwezi kurejesha heshima ya Bunge hilo wala kushughulikia uzembe na udhaifu ulioko ndani ya chombo hicho na kwenye serikali ikiwa hautaambatana na hatua nyingine za ziada na za haraka.

Aidha alitaka Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge imalize kazi yake kwa dharura ili majina ya wahusika yatajwe ndani ya Bunge na Bunge lijadili kupitisha maazimio ya hatua za ziada za kuchukuliwa na vyombo huru vya kiuchunguzi na hatimaye watakaothibitika kuvunja sheria wafikishwe mahakamani.

“Pamoja na hatua hizo, Kamati za vyama nazo zichukue hatua kwa wabunge wake watakaotajwa ili kudumisha misingi ya uadilifu na uwajibikaji kwa maslahi ya umma,” alisema Mnyika.

Pia Mnyika alisema uzembe mwingine na kashfa za wabunge zisingeendelea kutokea iwapo Bunge hilo lingeyafanyia kazi mapendekezo yanayotolewa ndani ya Bunge hilo, akitolea mfano mapendekezo ya sakata la Richmond na sakata la aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Jairo.

Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk Edward Hoseah alipoulizwa kuhusu namna ambavyo taasisi yake inafanyia kazi tuhuma hizo zilizoibuliwa bungeni, alimtaka mwandishi wa habari hizi aandike anavyotaka.

“Nyie waandishi mna matatizo kila siku kwenye vipindi vyetu tunatangaza kuwa tunapata taarifa kupitia maeneo mbalimbali, na kuzifanyia kazi, sasa unanipigia simu na kuniuliza hili ili nisemeje, unataka nikujibu nini?” alihoji.

Juzi bungeni Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo alibainisha kuwa wapo baadhi ya wabunge wamehongwa ili kumwajibisha yeye na Katibu Mkuu wake Eliakim Maswi na kuwafananisha wabunge hao kama Mobutu.

Pamoja na hayo, Profesa Muhongo alianika bungeni humo kuwa yupo mmoja wa wabunge ambaye ni mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini amekuwa akifanya biashara na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kwa kuliuzia matairi chini ya viwango.

NIDA yaongeza muda wa kujiandikisha Dar



MAMLAKA ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) imeongeza muda wa wiki moja wa kujaza fomu za kuomba vitambulisho vya uraia kwa wakazi wa Dar es Salaam na sasa zoezi hilo ambalo lilikuwa likamilike leo, litakamilika Jumatatu ijayo.

Taarifa iliyotolewa jana na NIDA iliwataka wananchi wote wa mkoa wa Dar es Salaam kujitokeza kujaza fomu hizo katika kipindi hicho kilichoongezwa kwani hawataongeza tena siku za uandikishaji.

Wakati NIDA ikiongeza muda huo, agizo la mamlaka hiyo ya kuwataka waandikishaji kuwagawia fomu wananchi ili wazijaze wenyewe limeendelea kukiukwa, hali ambayo imefanya vituo vingi vya uandikishaji viendelee kuwa na misururu mirefu ya watu.

Taarifa ya jana ya NIDA ilisisitiza tena suala hilo na kuwa waombaji wasiojua kusoma na kuandika watasaidiwa kujaza fomu na wananchi wanaojua kusoma na kuandika watapewa fomu ili wajaze wenyewe katika vituo vya usajili chini ya wasimamizi walioko katika kila kituo.

Kabla ya kutoa taarifa hiyo Mkurugenzi Mkuu wa NIDA, Jackson Mwaimu aliliambia gazeti hili jana kuwa mamlaka yake tayari imeshawataka waandikishaji hao kuwapa wananchi wenyewe wajaze fomu na akashangaa inakuwaje hawazingatii tamko hilo.

“Unajua tunashughulika na binadamu, sisi tumetoa maagizo lakini wao bado wanang’ang’ania kuwajazia fomu kwa kweli wamesababisha usumbufu mkubwa…yaani hawa watendaji wetu ni wagumu kuelewa,” alisema Mwaimu.

Gazeti hili pia lilibaini kuwa katika baadhi ya vituo watu wanaoenda kuandikishwa hawana taarifa juu ya tarehe walizozaliwa wazazi wao hali inayowalazimu wasimamizi wa vituo kuwajazia tarehe za bandia.

Lakini taarifa ya NIDA ya jana ilisisitiza kuwa ni marufuku kutoa taarifa ambazo sio sahihi ikiwemo ya uraia na watakaobainika watashitakiwa na wanaweza kutozwa faini au kuhukumiwa miaka mitatu jela ama vyote kwa pamoja.

Jana hali iliendelea kuwa ya sintofahamu katika vituo vingi. Katika kituo cha Kitunda waandikishaji walikuwa wanatumia utaratibu wa kukusanya nakala za nyaraka kama vyeti na vitambulisho na baadaye wanawaita mtu mmoja mmoja kuingia ndani ambako anaenda kuandikishwa kwa ofisa.

Utaratibu huo ulilalamikiwa na wananchi kuwa unachelewesha na kufanya eneo hilo kuwa na wananchi wengi ambao hawajajiandikisha.

Baadhi ya waandikishaji walipoulizwa na mwandishi kwa nini wasiwagawie wananchi fomu ili wajaze wenyewe walisema hawaruhusiwi kufanya hivyo.

Lakini walipobanwa kuwa tayari NIDA kupitia kwa mkurugenzi wake mkuu Mwaimu ameshatoa ruhusa wananchi wanaojua kusoma na kuandika wagawiwe fomu hizo, mmoja wa maofisa wanaoandikisha alisema eneo hilo lina watu wengi ambao hawajui kusoma wala kuandika.

“Huku kuna watu wengi hawajui kusoma wala kuandika ndio maana tunalazimika kuwaandikisha,” alisema ofisa huyo jambo ambalo wananchi wengi waliokuwa wamekusanyika katika eneo hilo walikanusha madai hayo ya kuwa hawajui kusoma wala kuandika.

Lakini baada ya mwandishi kushauri waandikishaji watumie busara wawaruhusu wananchi wajaze wenyewe fomu walikubali na kuwafanya wananchi wengi kwa kipindi kifupi kujiandikisha kwa wingi badala ya ilivyokuwa hapo awali.

“Unaona kumbe walikuwa wanakiuka utaratibu, walikuwa wanaweka mazingira ya rushwa,” alisema mwananchi mmoja baada ya kuona katika kipindi kifupi wananchi wanajiandikisha.

Katika kituo cha Masaki cha kujiandikisha, pamoja na kwamba kulikuwa hakuna foleni kubwa ya watu kama vituo vingine, ujazaji fomu hizo ulichukua muda kutokana na wahusika kuwajazia fomu watu wote hata wale wanaojua kusoma na kuandika.

Alipoulizwa mmoja wa waandikishaji kwanini hawapatii fomu wanaojua kusoma na kuandika na kujijazia wenyewe fomu hizo ili kuepuka makosa kama vile majina, alijibu kwa ukali kuwa, huo ndio utaratibu uliowekwa.

Katika kituo cha Msasani, mwananchi mmoja alidai fomu yake iliyopewa namba 90 aliichukua Ijumaa na hadi jana alikuwa hajafikiwa kuandikisha na akalalamika kuwa uandikishaji unaenda kwa kasi ndogo.

Katika kituo hicho pia kwa mujibu wa mwananchi huyo, waandikishaji hawaruhusu wananchi kupewa fomu na kuzijaza wenyewe hali ambayo imesababisha kasi ya uandikishwaji iwe ndogo.

Katika kituo cha Mogo kilichoko eneo la Majumbasita Ukonga kulikuwa na misururu mirefu huku watu wakiwa wamefika tangu saa kumi na moja alfajiri kutaka kujiandikisha huku baadhi wakiwalalamikia waandikishaji wasaidizi kwa kutowapa ushirikiano.

NIDA yaongeza muda wa kujiandikisha Dar



MAMLAKA ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) imeongeza muda wa wiki moja wa kujaza fomu za kuomba vitambulisho vya uraia kwa wakazi wa Dar es Salaam na sasa zoezi hilo ambalo lilikuwa likamilike leo, litakamilika Jumatatu ijayo.

Taarifa iliyotolewa jana na NIDA iliwataka wananchi wote wa mkoa wa Dar es Salaam kujitokeza kujaza fomu hizo katika kipindi hicho kilichoongezwa kwani hawataongeza tena siku za uandikishaji.

Wakati NIDA ikiongeza muda huo, agizo la mamlaka hiyo ya kuwataka waandikishaji kuwagawia fomu wananchi ili wazijaze wenyewe limeendelea kukiukwa, hali ambayo imefanya vituo vingi vya uandikishaji viendelee kuwa na misururu mirefu ya watu.

Taarifa ya jana ya NIDA ilisisitiza tena suala hilo na kuwa waombaji wasiojua kusoma na kuandika watasaidiwa kujaza fomu na wananchi wanaojua kusoma na kuandika watapewa fomu ili wajaze wenyewe katika vituo vya usajili chini ya wasimamizi walioko katika kila kituo.

Kabla ya kutoa taarifa hiyo Mkurugenzi Mkuu wa NIDA, Jackson Mwaimu aliliambia gazeti hili jana kuwa mamlaka yake tayari imeshawataka waandikishaji hao kuwapa wananchi wenyewe wajaze fomu na akashangaa inakuwaje hawazingatii tamko hilo.

“Unajua tunashughulika na binadamu, sisi tumetoa maagizo lakini wao bado wanang’ang’ania kuwajazia fomu kwa kweli wamesababisha usumbufu mkubwa…yaani hawa watendaji wetu ni wagumu kuelewa,” alisema Mwaimu.

Gazeti hili pia lilibaini kuwa katika baadhi ya vituo watu wanaoenda kuandikishwa hawana taarifa juu ya tarehe walizozaliwa wazazi wao hali inayowalazimu wasimamizi wa vituo kuwajazia tarehe za bandia.

Lakini taarifa ya NIDA ya jana ilisisitiza kuwa ni marufuku kutoa taarifa ambazo sio sahihi ikiwemo ya uraia na watakaobainika watashitakiwa na wanaweza kutozwa faini au kuhukumiwa miaka mitatu jela ama vyote kwa pamoja.

Jana hali iliendelea kuwa ya sintofahamu katika vituo vingi. Katika kituo cha Kitunda waandikishaji walikuwa wanatumia utaratibu wa kukusanya nakala za nyaraka kama vyeti na vitambulisho na baadaye wanawaita mtu mmoja mmoja kuingia ndani ambako anaenda kuandikishwa kwa ofisa.

Utaratibu huo ulilalamikiwa na wananchi kuwa unachelewesha na kufanya eneo hilo kuwa na wananchi wengi ambao hawajajiandikisha.

Baadhi ya waandikishaji walipoulizwa na mwandishi kwa nini wasiwagawie wananchi fomu ili wajaze wenyewe walisema hawaruhusiwi kufanya hivyo.

Lakini walipobanwa kuwa tayari NIDA kupitia kwa mkurugenzi wake mkuu Mwaimu ameshatoa ruhusa wananchi wanaojua kusoma na kuandika wagawiwe fomu hizo, mmoja wa maofisa wanaoandikisha alisema eneo hilo lina watu wengi ambao hawajui kusoma wala kuandika.

“Huku kuna watu wengi hawajui kusoma wala kuandika ndio maana tunalazimika kuwaandikisha,” alisema ofisa huyo jambo ambalo wananchi wengi waliokuwa wamekusanyika katika eneo hilo walikanusha madai hayo ya kuwa hawajui kusoma wala kuandika.

Lakini baada ya mwandishi kushauri waandikishaji watumie busara wawaruhusu wananchi wajaze wenyewe fomu walikubali na kuwafanya wananchi wengi kwa kipindi kifupi kujiandikisha kwa wingi badala ya ilivyokuwa hapo awali.

“Unaona kumbe walikuwa wanakiuka utaratibu, walikuwa wanaweka mazingira ya rushwa,” alisema mwananchi mmoja baada ya kuona katika kipindi kifupi wananchi wanajiandikisha.

Katika kituo cha Masaki cha kujiandikisha, pamoja na kwamba kulikuwa hakuna foleni kubwa ya watu kama vituo vingine, ujazaji fomu hizo ulichukua muda kutokana na wahusika kuwajazia fomu watu wote hata wale wanaojua kusoma na kuandika.

Alipoulizwa mmoja wa waandikishaji kwanini hawapatii fomu wanaojua kusoma na kuandika na kujijazia wenyewe fomu hizo ili kuepuka makosa kama vile majina, alijibu kwa ukali kuwa, huo ndio utaratibu uliowekwa.

Katika kituo cha Msasani, mwananchi mmoja alidai fomu yake iliyopewa namba 90 aliichukua Ijumaa na hadi jana alikuwa hajafikiwa kuandikisha na akalalamika kuwa uandikishaji unaenda kwa kasi ndogo.

Katika kituo hicho pia kwa mujibu wa mwananchi huyo, waandikishaji hawaruhusu wananchi kupewa fomu na kuzijaza wenyewe hali ambayo imesababisha kasi ya uandikishwaji iwe ndogo.

Katika kituo cha Mogo kilichoko eneo la Majumbasita Ukonga kulikuwa na misururu mirefu huku watu wakiwa wamefika tangu saa kumi na moja alfajiri kutaka kujiandikisha huku baadhi wakiwalalamikia waandikishaji wasaidizi kwa kutowapa ushirikiano.

Waziri aibua madudu mengine Tanesco



UOZO zaidi wa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Umeme (Tanesco) aliyesimamishwa, William Mhando umeibuliwa jana na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo.

Akizungumza jana wakati wa kujibu hoja za wabunge kuhusu makadirio ya bajeti ya wizara hiyo, Profesa Muhongo alisema uozo wa Mhando, si tu kuipa kampuni ya mkewe zabuni ya ugavi wa vifaa vya ofisi vya Tanesco kwa gharama ya Sh milioni 884, bali alifanya madudu zaidi.

Alisema Mtendaji huyo wakati akiisimamia Tanesco, shirika hilo lilikuwa likinunua nguzo kutoka Iringa na kuzisafirisha kwenda Mombasa nchi jirani ya Kenya na kisha kuzirudisha nchini na kutoa maelezo kuwa zimenunuliwa kutoka Afrika Kusini.

Profesa Muhongo aliyekuwa akizungumza kwa kujiamini huku akiwaambia wabunge kuwa anao ushahidi wa kutosha, alisema Tanesco pia chini ya Mhando, iliagiza vipuri nje ya nchi na kulipa pauni za Uingereza 50,000, sawa na zaidi ya Sh milioni 120, lakini wakapokea kasha la misumari badala ya vipuri.

Alisema kutokana na utendaji usio wa uwajibikaji wa Mhando, waliona kuwa umuhimu wa kuchukua hatua za haraka ambapo Bodi ya Tanesco, iliitisha kikao cha dharura na kumsimamisha kazi.

Tuhuma zingine za Mhando zinazochunguzwa kwa mujibu wa Profesa Muhongo ni pamoja na kukumbatia wafanyabiashara na kushindwa kutenganisha maslahi binafsi na ya umma.

Mbali na hayo, Profesa Muhongo ambaye alisema hata Bodi ya Tanesco nayo itavunjwa kutokana na uozo ulioko huko, alisema pia waligundua kuwa baadhi ya wabunge ambao ni wajumbe wa Kamati ya Nishati na Madini, walikuwa wanafanya biashara na Tanesco.

Kwa mujibu wa Profesa Muhongo, mmoja wa wajumbe wa kamati hiyo (hakumtaja, ingawa jina tunalo) aliingia mkataba wa kuiuzia Tanesco matairi ya magari.

Alisema hata baada ya kupata mkataba, mbunge huyo ambaye hakumtaja jina, aliiuzia Tanesco matairi ya kiwango cha chini na akapandisha bei ya kuuzia ikawa kubwa kuliko iliyokuweko katika mkataba.

“Nawaomba wabunge waache kufanya biashara na Tanesco ili waisimamie kwa uhuru, vinginevyo watajiweka katika mazingira magumu ya kimaslahi,” alisema.

Kuhusu kuundwa tume ya uchunguzi, Profesa Muhongo alisema hakuna haja ya tume au kamati maalumu kwa kuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), amepewa kazi hiyo.

Akina Mobutu bungeni Kuhusu mpango uliosukwa na baadhi ya wabunge wanaodaiwa kuhongwa ili kumwajibisha yeye na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi, Profesa Muhongo alianza kwa kuwagawa wabunge katika makundi ya viongozi wa zamani wa Afrika.

“Hapa kuna makundi mawili, moja la watoto wa Mwalimu Julius Nyerere, Edward Sokoine na Rashidi Kawawa na kundi la Mobutu Seseko, Sani Abacha na Bokasa,” alisema Muhongo.

Kwa mujibu wa Profesa Muhongo, wabunge waliokuwa wakitetea Tanesco na Mhando ambao kawafananisha na akina Mobutu, walikuwa wakitetea upuuzi na kuhoji wanatetea vipi shirika ambalo tangu lianzishwe mwaka 1930 hadi leo asilimia 20 tu ya Watanzania ndio wana umeme.

Alisema yeye na Maswi, walijiandaa na hoja ya kuwajibishwa kwa kukiuka sheria kama ingefikishwa bungeni na wabunge hao na kuna barua moja kutoka kwa Mfilisi wa Kampuni ya IPTL, Mamlaka ya Ufilisi, Vizazi na Vifo (RITA) ambayo ndiyo ingewaokoa.

“Pamoja na kwamba mimi si mwanasheria, kwa kusoma soma magazeti na vitabu nilifanikiwa kuwa mwanasheria pori, tulikuwa na barua moja ilikuwa kama nondo ya mwisho ya kujitetea mimi na Maswi kama suala hilo lingefikishwa bungeni,” alisema.

Alisema barua hiyo iliweka wazi kuwa mnunuzi wa mafuta ya IPTL, ni Wizara na kufafanua kuwa hawakuingilia utaratibu wa Tanesco wa zabuni, wala kuikataza isinunue mafuta kutoka katika kampuni ilizoona zinafaa.

Alifafanua kuwa Tanesco haikuwa na fedha za kununua mafuta na yeye na Maswi kwa kutoa fedha za wizara walikuwa huru kuchagua mahali pa kununua ambako ni Kampuni ya Puma Energy ambayo Serikali ina hisa asilimia 50 na ilikuwa inauza kwa bei nafuu.

Mbali na kuuza kwa bei nafuu, alibainisha kuwa hata moja ya kampuni ambazo zilishinda zabuni ya Tanesco, kuiuzia IPTL mafuta kwa Sh 1,800 kwa lita, ilikuwa inanunua mafuta hayo Puma Energy na kuuzia IPTL kwa bei ya juu.

Aliwashukuru wabunge kwa kumpa ushirikiano na kuongeza kuwa anataka baada ya muda Serikali iwe inachukua gawiwo kutoka Tanesco na kuacha kutafuta fedha za bajeti kila siku katika bia. Wizi Tanesco Profesa Muhongo alisema Tanesco kuna wizi mkubwa wa umeme kupitia mita za Luku zisizosajiliwa na shirika hilo.

Aliwataja wateja watano wakubwa waliokamatwa na kufikishwa Polisi kwa wizi wa umeme kuwa ni pamoja na shule za St. Mary’s International School zinazodaiwa kuiba umeme wa Sh milioni 10.5.

Mtandao wa shule za St. Mary’s unamilikiwa na Mchungaji Dk Gertrude Rwakatare ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalumu.

Wengine ni Benki ya Access iliyopo Matumbi Tabata Sh milioni 13.5, duka la Shree lililoko mtaa wa Aggrey, Kariakoo Sh milioni 8 na Hoteli ya Akubu ya Kariakoo pia Sh milioni 25.3.

Waziri aibua madudu mengine Tanesco



UOZO zaidi wa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Umeme (Tanesco) aliyesimamishwa, William Mhando umeibuliwa jana na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo.

Akizungumza jana wakati wa kujibu hoja za wabunge kuhusu makadirio ya bajeti ya wizara hiyo, Profesa Muhongo alisema uozo wa Mhando, si tu kuipa kampuni ya mkewe zabuni ya ugavi wa vifaa vya ofisi vya Tanesco kwa gharama ya Sh milioni 884, bali alifanya madudu zaidi.

Alisema Mtendaji huyo wakati akiisimamia Tanesco, shirika hilo lilikuwa likinunua nguzo kutoka Iringa na kuzisafirisha kwenda Mombasa nchi jirani ya Kenya na kisha kuzirudisha nchini na kutoa maelezo kuwa zimenunuliwa kutoka Afrika Kusini.

Profesa Muhongo aliyekuwa akizungumza kwa kujiamini huku akiwaambia wabunge kuwa anao ushahidi wa kutosha, alisema Tanesco pia chini ya Mhando, iliagiza vipuri nje ya nchi na kulipa pauni za Uingereza 50,000, sawa na zaidi ya Sh milioni 120, lakini wakapokea kasha la misumari badala ya vipuri.

Alisema kutokana na utendaji usio wa uwajibikaji wa Mhando, waliona kuwa umuhimu wa kuchukua hatua za haraka ambapo Bodi ya Tanesco, iliitisha kikao cha dharura na kumsimamisha kazi.

Tuhuma zingine za Mhando zinazochunguzwa kwa mujibu wa Profesa Muhongo ni pamoja na kukumbatia wafanyabiashara na kushindwa kutenganisha maslahi binafsi na ya umma.

Mbali na hayo, Profesa Muhongo ambaye alisema hata Bodi ya Tanesco nayo itavunjwa kutokana na uozo ulioko huko, alisema pia waligundua kuwa baadhi ya wabunge ambao ni wajumbe wa Kamati ya Nishati na Madini, walikuwa wanafanya biashara na Tanesco.

Kwa mujibu wa Profesa Muhongo, mmoja wa wajumbe wa kamati hiyo (hakumtaja, ingawa jina tunalo) aliingia mkataba wa kuiuzia Tanesco matairi ya magari.

Alisema hata baada ya kupata mkataba, mbunge huyo ambaye hakumtaja jina, aliiuzia Tanesco matairi ya kiwango cha chini na akapandisha bei ya kuuzia ikawa kubwa kuliko iliyokuweko katika mkataba.

“Nawaomba wabunge waache kufanya biashara na Tanesco ili waisimamie kwa uhuru, vinginevyo watajiweka katika mazingira magumu ya kimaslahi,” alisema.

Kuhusu kuundwa tume ya uchunguzi, Profesa Muhongo alisema hakuna haja ya tume au kamati maalumu kwa kuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), amepewa kazi hiyo.

Akina Mobutu bungeni Kuhusu mpango uliosukwa na baadhi ya wabunge wanaodaiwa kuhongwa ili kumwajibisha yeye na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi, Profesa Muhongo alianza kwa kuwagawa wabunge katika makundi ya viongozi wa zamani wa Afrika.

“Hapa kuna makundi mawili, moja la watoto wa Mwalimu Julius Nyerere, Edward Sokoine na Rashidi Kawawa na kundi la Mobutu Seseko, Sani Abacha na Bokasa,” alisema Muhongo.

Kwa mujibu wa Profesa Muhongo, wabunge waliokuwa wakitetea Tanesco na Mhando ambao kawafananisha na akina Mobutu, walikuwa wakitetea upuuzi na kuhoji wanatetea vipi shirika ambalo tangu lianzishwe mwaka 1930 hadi leo asilimia 20 tu ya Watanzania ndio wana umeme.

Alisema yeye na Maswi, walijiandaa na hoja ya kuwajibishwa kwa kukiuka sheria kama ingefikishwa bungeni na wabunge hao na kuna barua moja kutoka kwa Mfilisi wa Kampuni ya IPTL, Mamlaka ya Ufilisi, Vizazi na Vifo (RITA) ambayo ndiyo ingewaokoa.

“Pamoja na kwamba mimi si mwanasheria, kwa kusoma soma magazeti na vitabu nilifanikiwa kuwa mwanasheria pori, tulikuwa na barua moja ilikuwa kama nondo ya mwisho ya kujitetea mimi na Maswi kama suala hilo lingefikishwa bungeni,” alisema.

Alisema barua hiyo iliweka wazi kuwa mnunuzi wa mafuta ya IPTL, ni Wizara na kufafanua kuwa hawakuingilia utaratibu wa Tanesco wa zabuni, wala kuikataza isinunue mafuta kutoka katika kampuni ilizoona zinafaa.

Alifafanua kuwa Tanesco haikuwa na fedha za kununua mafuta na yeye na Maswi kwa kutoa fedha za wizara walikuwa huru kuchagua mahali pa kununua ambako ni Kampuni ya Puma Energy ambayo Serikali ina hisa asilimia 50 na ilikuwa inauza kwa bei nafuu.

Mbali na kuuza kwa bei nafuu, alibainisha kuwa hata moja ya kampuni ambazo zilishinda zabuni ya Tanesco, kuiuzia IPTL mafuta kwa Sh 1,800 kwa lita, ilikuwa inanunua mafuta hayo Puma Energy na kuuzia IPTL kwa bei ya juu.

Aliwashukuru wabunge kwa kumpa ushirikiano na kuongeza kuwa anataka baada ya muda Serikali iwe inachukua gawiwo kutoka Tanesco na kuacha kutafuta fedha za bajeti kila siku katika bia. Wizi Tanesco Profesa Muhongo alisema Tanesco kuna wizi mkubwa wa umeme kupitia mita za Luku zisizosajiliwa na shirika hilo.

Aliwataja wateja watano wakubwa waliokamatwa na kufikishwa Polisi kwa wizi wa umeme kuwa ni pamoja na shule za St. Mary’s International School zinazodaiwa kuiba umeme wa Sh milioni 10.5.

Mtandao wa shule za St. Mary’s unamilikiwa na Mchungaji Dk Gertrude Rwakatare ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalumu.

Wengine ni Benki ya Access iliyopo Matumbi Tabata Sh milioni 13.5, duka la Shree lililoko mtaa wa Aggrey, Kariakoo Sh milioni 8 na Hoteli ya Akubu ya Kariakoo pia Sh milioni 25.3.

Saturday, July 28, 2012

Kuunganishiwa umeme sasa kuanzia Sh180,000



Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo, akiwakilisha makadirio na matumizi ya Wizara yake kwa mwaka wa fedha 2012/2013 Bungeni, Dodoma jana.

NI KWA WALE WASIOHITAJI NGUZO, WA NGUZO MBILI KUTOZWA SH 800,000, WAZIRI MUHONGO, ASEMA MGAWO SAFARI HII HAUKUBALIKI
Boniface Meena, Dodoma
 
SERIKALI imetangaza kushusha gharama za kuunganisha umeme kwa wananchi wanaohitaji huduma hiyo kwa viwango ambavyo ni kati ya asilimia 60 na 77 kwa wakazi wa vijijini na kati ya asilimia 29 na 65 kwa wananchi waishio sehemu za mijini.

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo aliliambia Bunge jana kuwa gharama za kuunganishiwa umeme kwa wateja walioko kwenye umbali usiozidi meta 30 (single phase) ambao hawahitaji nguzo sasa zitakuwa Sh177,000 kwa wateja wa vijijini na mijini itakuwa Sh320,960 badala ya Sh455,108 ambazo zilikuwa zikilipwa awali bila kujali mteja aliko.

Akiwasilisha hotuba ya makadirio ya matumizi ya wizara yake ya 2012/2013 bungeni Dodoma jana, waziri huyo alisema punguzo hilo ni sawa na asilimia 61.11 kwa wateja waishio vijijini na asilimia 29.48 kwa wateja waishio mijini.

Profesa Muhongo alisema pia Serikali imeshusha gharama za uunganishaji wa umeme kwa wateja watakaojengewa njia moja (single phase) na kuwekewa nguzo moja katika maeneo ya vijijini ambao sasa watalipa Sh337,740 na mijini Sh515,618 badala ya Sh1,351,884 zilizokuwa zikilipwa awali.
“Punguzo hilo la pili ni sawa na asilimia 75.02 kwa wateja wa vijijini na asilimia 61.86 kwa wateja waishio mijini,” alisema Profesa Muhongo.

Alisema kwa wateja watakaojengewa njia moja na kuwekewa nguzo mbili katika maeneo ya vijijini watalipa Sh454,654 na mijini watalipa Sh696,670 badala ya Sh2.001 milioni zilizokuwa zikilipwa awali.

“Punguzo hili ni sawa na asilimia 77.28 kwa wateja waishio vijijini na asilimia 65.19 kwa wateja waishio mijini,” alisema Profesa Muhongo na kuongeza. “Viwango hivyo vya gharama vitaanza kutumika Januari mwakani bila kisingizio.”

Chimbuko la Punguzo
Hatua ya kushushwa kwa gharama za kuunganishiwa umeme zimekuja zaidi ya mwaka mmoja tangu Rais Jakaya Kikwete alipolilekeza Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), kupunguza gharama hizo ili kupata wateja wengi zaidi.

Machi 18 mwaka jana, Rais Kikwete aliitaka Tanesco, kupunguza gharama za kuunganisha umeme kwa wananchi ili wengi wapate huduma hiyo sambamba na kuongeza wateja wanaotumia umeme kwa asilimia 30 ifikapo mwaka 2015.

Akizungumza na wafanyakazi wa Wizara ya Nishati na Madini, Rais Kikwete alisema gharama hiyo ikipunguza, itaiwezesha Tanesco kupata wateja wengi ikilinganishwa na sasa.
Kauli ya Rais ilitokana na maelezo ya Mkurugenzi wa Shirika hilo, William Mhando (ambaye sasa amesimamishwa kazi) kuwa Tanesco ilikuwa ikifanya mazungumzo na Benki za Akiba na Azania ili zitoe mikopo kwa wateja kwa ajili ya kuunganishiwa umeme.

Kadhalika Mei 16 mwaka huu, akizungumza na Balozi wa Marekani nchini, Alfonso Lenhardt Profesa Muhongo alisema: “Kipaumbele cha wizara kwa sasa ni kupata umeme wa uhakika wa bei nafuu na unaotabirika. Ni muhimu kuongeza watumiaji wa umeme kwa kuwa kwa sasa kwa takwimu za Tanesco ni asilimia 18.4 tu ya Watanzania wanaopata huduma hii.”

Wizi Tanesco Profesa Muhongo aliwataka wezi wa umeme kujisalimisha kabla hawajakamatwa kwani hata wakijificha watakamatwa tu. Alisema upotevu wa umeme unafanywa na baadhi ya wananchi wanaoshirikiana na wafanyakazi wa Tanesco kwa kushirikiana na vishoka. “Kuna rushwa iliyokithiri Tanesco, kuna wezi wanaowaunganishia watu umeme na kuliibia shirika, wakae chonjo kwani watakamatwa tu,” alisema Profesa Muhongo. kuhusu wizara hiyo, alisema mambo mengi yatafanyika kwa uwazi na haoni sababu za kila jambo kuwa ni siri. “Mnakaribishwa wizarani kila mtakapoona mambo yanakwenda ndivyo sivyo, hatutakuwa na mambo ya kuficha tutakuwa wawazi,” alisema Profesa Muhongo.

Mgawo wa Umeme
Kuhusu suala la mgawo wa umeme, alisema hautakuwepo tena na haukubaliki kamwe.
“Waheshimiwa wabunge, suala la mgawo haliwezekani na halikubaliki,” alisema Profesa Muhongo. Alisema katika mwaka 2011/12, wizara iliendelea kuchukua hatua mbalimbali ili kuboresha upatikanaji wa nishati ya umeme nchini. Profesa Muhongo alisema hadi Juni, 2012 uwezo wa mitambo ya kufua umeme (installed capacity) ulikua megawati 1,375.74 (gesi asilia ikiwa ni asilimia 40, maji asilimia 41 na mafuta asilimia 19).

“Uwezo huo ni ongezeko la megawati 367 sawa na asilimia 36 ikilinganishwa na uwezo wa megawati 1,013.74 uliokuwepo Juni, 2011. Mahitaji ya juu ya umeme kwa mwaka 2011/12 yalifikia wastani wa MW 820.35 ikilinganishwa na MW 730 kwa mwaka 2010/11,” alisema.

Alisema Julai, 2011 wakati wa Bajeti ya wizara hiyo ilipowasilishwa, nchi ilikuwa katika mgawo wa umeme... “Mgawo huo ulitokana na upungufu wa umeme wa takriban megawati 300 uliosababishwa na upungufu wa maji katika mabwawa kwenye vituo vya kufua umeme. Kutokana na hali hiyo, Serikali ililazimika kuandaa mpango wa dharura wa kuondoa mgawo wa umeme nchini ulioridhiwa na bunge.” Alisema katika mpango huo, megawati 572 zilipangwa kuzalishwa na kuingizwa kwenye gridi ya taifa. Alisema hadi kufikia Juni, mwaka huu uwezo wa ufuaji wa umeme kutokana na mpango huo wa dharura ulifikia megawati 422.

“Mitambo hiyo inajumuisha Symbion megawati 137, Aggreko megawati 100, IPTL megawati 100 na mtambo wa gesi asili wa Ubungo megawati 150," alisema. Alisema kutofikiwa kwa kiwango kilichokusudiwa, kunatokana na kukosekana kwa mitambo ya megawati 150 ya Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) iliyokadiriwa kugharimu Dola za Marekani 162 milioni sawa na Sh256.20 bilioni. Alisema hadi kufikia mwishoni mwa Juni, mwaka huu lengo la kuondoa mgawo wa umeme lilifikiwa kwa asilimia 100.

“Kwa sasa hakuna mgawo wa umeme kwa kuwa upungufu ulikuwepo ulikuwa ni kati ya megawati 260 na megawati 300 ikilinganishwa na uwezo wa megawati 422 ulioongezeka,” alisema. Kamati ya Bunge
Kwa upande wake, Mwenyekiti Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, Suleiman Zedi alisema pamoja na kamati yake kuishauri Serikali njia bora za kupunguza tatizo la umeme, bado hali ya upatikanaji wa umeme siyo ya kuridhisha.

“Sababu hizo ni pamoja na mabadiliko ya tabia nchi yanayosababisha ukosefu wa mvua za kutosha na hivyo kuathiri mitambo ambayo inatumia maji,” alisema Zedi. Alisema katika mwaka wa fedha 2011/12, uzalishaji wa mitambo ya maji ulikuwa asilimia 45 ya umeme wote uliozalishwa nchini ikilinganishwa na uwezo wake wa asilimia 51.

“Kamati ina hofu kuwa ifikapo miezi ya kiangazi ya Agosti mpaka Oktoba hatutaweza kuzalisha sehemu kubwa ya umeme utokanao na maji na hivyo kutegemea umeme unaozalishwa kwa gesi na mafuta tu,” alisema Zedi. Alisema kuwa kamati hiyo inaamini kuwa vyanzo vya umeme nchini vikitumiwa ipasavyo, upungufu wa umeme nchini utakuwa historia.

Kuunganishiwa umeme sasa kuanzia Sh180,000



Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo, akiwakilisha makadirio na matumizi ya Wizara yake kwa mwaka wa fedha 2012/2013 Bungeni, Dodoma jana.

NI KWA WALE WASIOHITAJI NGUZO, WA NGUZO MBILI KUTOZWA SH 800,000, WAZIRI MUHONGO, ASEMA MGAWO SAFARI HII HAUKUBALIKI
Boniface Meena, Dodoma
 
SERIKALI imetangaza kushusha gharama za kuunganisha umeme kwa wananchi wanaohitaji huduma hiyo kwa viwango ambavyo ni kati ya asilimia 60 na 77 kwa wakazi wa vijijini na kati ya asilimia 29 na 65 kwa wananchi waishio sehemu za mijini.

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo aliliambia Bunge jana kuwa gharama za kuunganishiwa umeme kwa wateja walioko kwenye umbali usiozidi meta 30 (single phase) ambao hawahitaji nguzo sasa zitakuwa Sh177,000 kwa wateja wa vijijini na mijini itakuwa Sh320,960 badala ya Sh455,108 ambazo zilikuwa zikilipwa awali bila kujali mteja aliko.

Akiwasilisha hotuba ya makadirio ya matumizi ya wizara yake ya 2012/2013 bungeni Dodoma jana, waziri huyo alisema punguzo hilo ni sawa na asilimia 61.11 kwa wateja waishio vijijini na asilimia 29.48 kwa wateja waishio mijini.

Profesa Muhongo alisema pia Serikali imeshusha gharama za uunganishaji wa umeme kwa wateja watakaojengewa njia moja (single phase) na kuwekewa nguzo moja katika maeneo ya vijijini ambao sasa watalipa Sh337,740 na mijini Sh515,618 badala ya Sh1,351,884 zilizokuwa zikilipwa awali.
“Punguzo hilo la pili ni sawa na asilimia 75.02 kwa wateja wa vijijini na asilimia 61.86 kwa wateja waishio mijini,” alisema Profesa Muhongo.

Alisema kwa wateja watakaojengewa njia moja na kuwekewa nguzo mbili katika maeneo ya vijijini watalipa Sh454,654 na mijini watalipa Sh696,670 badala ya Sh2.001 milioni zilizokuwa zikilipwa awali.

“Punguzo hili ni sawa na asilimia 77.28 kwa wateja waishio vijijini na asilimia 65.19 kwa wateja waishio mijini,” alisema Profesa Muhongo na kuongeza. “Viwango hivyo vya gharama vitaanza kutumika Januari mwakani bila kisingizio.”

Chimbuko la Punguzo
Hatua ya kushushwa kwa gharama za kuunganishiwa umeme zimekuja zaidi ya mwaka mmoja tangu Rais Jakaya Kikwete alipolilekeza Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), kupunguza gharama hizo ili kupata wateja wengi zaidi.

Machi 18 mwaka jana, Rais Kikwete aliitaka Tanesco, kupunguza gharama za kuunganisha umeme kwa wananchi ili wengi wapate huduma hiyo sambamba na kuongeza wateja wanaotumia umeme kwa asilimia 30 ifikapo mwaka 2015.

Akizungumza na wafanyakazi wa Wizara ya Nishati na Madini, Rais Kikwete alisema gharama hiyo ikipunguza, itaiwezesha Tanesco kupata wateja wengi ikilinganishwa na sasa.
Kauli ya Rais ilitokana na maelezo ya Mkurugenzi wa Shirika hilo, William Mhando (ambaye sasa amesimamishwa kazi) kuwa Tanesco ilikuwa ikifanya mazungumzo na Benki za Akiba na Azania ili zitoe mikopo kwa wateja kwa ajili ya kuunganishiwa umeme.

Kadhalika Mei 16 mwaka huu, akizungumza na Balozi wa Marekani nchini, Alfonso Lenhardt Profesa Muhongo alisema: “Kipaumbele cha wizara kwa sasa ni kupata umeme wa uhakika wa bei nafuu na unaotabirika. Ni muhimu kuongeza watumiaji wa umeme kwa kuwa kwa sasa kwa takwimu za Tanesco ni asilimia 18.4 tu ya Watanzania wanaopata huduma hii.”

Wizi Tanesco Profesa Muhongo aliwataka wezi wa umeme kujisalimisha kabla hawajakamatwa kwani hata wakijificha watakamatwa tu. Alisema upotevu wa umeme unafanywa na baadhi ya wananchi wanaoshirikiana na wafanyakazi wa Tanesco kwa kushirikiana na vishoka. “Kuna rushwa iliyokithiri Tanesco, kuna wezi wanaowaunganishia watu umeme na kuliibia shirika, wakae chonjo kwani watakamatwa tu,” alisema Profesa Muhongo. kuhusu wizara hiyo, alisema mambo mengi yatafanyika kwa uwazi na haoni sababu za kila jambo kuwa ni siri. “Mnakaribishwa wizarani kila mtakapoona mambo yanakwenda ndivyo sivyo, hatutakuwa na mambo ya kuficha tutakuwa wawazi,” alisema Profesa Muhongo.

Mgawo wa Umeme
Kuhusu suala la mgawo wa umeme, alisema hautakuwepo tena na haukubaliki kamwe.
“Waheshimiwa wabunge, suala la mgawo haliwezekani na halikubaliki,” alisema Profesa Muhongo. Alisema katika mwaka 2011/12, wizara iliendelea kuchukua hatua mbalimbali ili kuboresha upatikanaji wa nishati ya umeme nchini. Profesa Muhongo alisema hadi Juni, 2012 uwezo wa mitambo ya kufua umeme (installed capacity) ulikua megawati 1,375.74 (gesi asilia ikiwa ni asilimia 40, maji asilimia 41 na mafuta asilimia 19).

“Uwezo huo ni ongezeko la megawati 367 sawa na asilimia 36 ikilinganishwa na uwezo wa megawati 1,013.74 uliokuwepo Juni, 2011. Mahitaji ya juu ya umeme kwa mwaka 2011/12 yalifikia wastani wa MW 820.35 ikilinganishwa na MW 730 kwa mwaka 2010/11,” alisema.

Alisema Julai, 2011 wakati wa Bajeti ya wizara hiyo ilipowasilishwa, nchi ilikuwa katika mgawo wa umeme... “Mgawo huo ulitokana na upungufu wa umeme wa takriban megawati 300 uliosababishwa na upungufu wa maji katika mabwawa kwenye vituo vya kufua umeme. Kutokana na hali hiyo, Serikali ililazimika kuandaa mpango wa dharura wa kuondoa mgawo wa umeme nchini ulioridhiwa na bunge.” Alisema katika mpango huo, megawati 572 zilipangwa kuzalishwa na kuingizwa kwenye gridi ya taifa. Alisema hadi kufikia Juni, mwaka huu uwezo wa ufuaji wa umeme kutokana na mpango huo wa dharura ulifikia megawati 422.

“Mitambo hiyo inajumuisha Symbion megawati 137, Aggreko megawati 100, IPTL megawati 100 na mtambo wa gesi asili wa Ubungo megawati 150," alisema. Alisema kutofikiwa kwa kiwango kilichokusudiwa, kunatokana na kukosekana kwa mitambo ya megawati 150 ya Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) iliyokadiriwa kugharimu Dola za Marekani 162 milioni sawa na Sh256.20 bilioni. Alisema hadi kufikia mwishoni mwa Juni, mwaka huu lengo la kuondoa mgawo wa umeme lilifikiwa kwa asilimia 100.

“Kwa sasa hakuna mgawo wa umeme kwa kuwa upungufu ulikuwepo ulikuwa ni kati ya megawati 260 na megawati 300 ikilinganishwa na uwezo wa megawati 422 ulioongezeka,” alisema. Kamati ya Bunge
Kwa upande wake, Mwenyekiti Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, Suleiman Zedi alisema pamoja na kamati yake kuishauri Serikali njia bora za kupunguza tatizo la umeme, bado hali ya upatikanaji wa umeme siyo ya kuridhisha.

“Sababu hizo ni pamoja na mabadiliko ya tabia nchi yanayosababisha ukosefu wa mvua za kutosha na hivyo kuathiri mitambo ambayo inatumia maji,” alisema Zedi. Alisema katika mwaka wa fedha 2011/12, uzalishaji wa mitambo ya maji ulikuwa asilimia 45 ya umeme wote uliozalishwa nchini ikilinganishwa na uwezo wake wa asilimia 51.

“Kamati ina hofu kuwa ifikapo miezi ya kiangazi ya Agosti mpaka Oktoba hatutaweza kuzalisha sehemu kubwa ya umeme utokanao na maji na hivyo kutegemea umeme unaozalishwa kwa gesi na mafuta tu,” alisema Zedi. Alisema kuwa kamati hiyo inaamini kuwa vyanzo vya umeme nchini vikitumiwa ipasavyo, upungufu wa umeme nchini utakuwa historia.

Akutwa na uniti 29,365.5 za sh milioni 8

MKAZI wa Kariakoo Mtaa Agrey jijini Dar es Salaam, Ahamad Selemani anashikiliwa na Polisi baada mita yake ya Luku kukutwa na uniti za umeme 29,365.5, zenye thamani ya sh milioni nane.

Meneja wa Shirika la Ugavi wa Umeme Tanzania (TANESCO), Kanda ya Ilala, Athanasius Nangali, alisema jana kuwa mteja huyo ambaye jina analotumia kwenye mita yake ya Luku ni Mallick Bhachool, hajawahi kununua umeme tangu alipounganishiwa mita hiyo mwaka 2010.

Mtuhumiwa huyo anashikiliwa na Polisi na anatarajiwa kufikishwa mahakamani wakati wowote.

Kwa mujibu wa Nangali, tukio lingine kama hilo limetokea katika eneo la Kariakoo Mtaa wa Magila ambapo Meneja wa Hoteli ya Akubu Paradise, Inocent Masawe alikamatwa akiwa na uniti 1100 za umeme kwenye mita yake ya Luku, zenye thamani ya sh milioni 4.

Alisema mteja huyo amekuwa akifanya ujanja wa kununua umeme kidogo kwa ajili ya matumuzi ya hoteli yake, lakini umeme uliomo kwenye mita ni mwingi kuliko kiasi anachonunulia.

“Hawa tutakula nao sahani moja hadi watuambie wanakonunua umeme na hatimaye tutakamata mtambo unaozalisha uniti hizo bandia,” alisema.

Nangali alisema TANESCO itahakikisha inawatia mbaroni wauzaji wa uniti hizo kinyume cha sheria.

“Hawa kuna sehemu wananunua umeme lakini hatujafahamu ni wapi hivyo kukamatwa kwao ni dalili kubwa ya kubaini wanakonunua maana katika hali ya kawaida haiwezekani mtu awe na uniti hizi zote,” alifafanua Nangali.

Alitoa wito kwa Watanzania kutoa taarifa za wanaoihujumu TANESCO na kutangaza zawadi ya sh 50,000 kwa kila nyumba itakayokamatwa.

Alipoulizwa kuhusu ongezeko la faini na idadi ya watu waliofikishwa mahakamani, Nangali alisema idadi hiyo itajulikana mara baada ya kufanya majumuisho mwishoni mwa mwezi huu japo inakadiriwa kuwa zaidi ya watu 100 sasa wameshakamatwa na kulipishwa faini tangu kuanza kwa operesheni hiyo.

Wiki tatu zilizopita aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo, William Mhando, alitangaza kukamatwa kwa watu watatu mkoani Dodoma na wawili jijini Dar es Salaam waliokuwa wakitumia umeme ambao haujafahamika unakopatikana.

Akutwa na uniti 29,365.5 za sh milioni 8

MKAZI wa Kariakoo Mtaa Agrey jijini Dar es Salaam, Ahamad Selemani anashikiliwa na Polisi baada mita yake ya Luku kukutwa na uniti za umeme 29,365.5, zenye thamani ya sh milioni nane.

Meneja wa Shirika la Ugavi wa Umeme Tanzania (TANESCO), Kanda ya Ilala, Athanasius Nangali, alisema jana kuwa mteja huyo ambaye jina analotumia kwenye mita yake ya Luku ni Mallick Bhachool, hajawahi kununua umeme tangu alipounganishiwa mita hiyo mwaka 2010.

Mtuhumiwa huyo anashikiliwa na Polisi na anatarajiwa kufikishwa mahakamani wakati wowote.

Kwa mujibu wa Nangali, tukio lingine kama hilo limetokea katika eneo la Kariakoo Mtaa wa Magila ambapo Meneja wa Hoteli ya Akubu Paradise, Inocent Masawe alikamatwa akiwa na uniti 1100 za umeme kwenye mita yake ya Luku, zenye thamani ya sh milioni 4.

Alisema mteja huyo amekuwa akifanya ujanja wa kununua umeme kidogo kwa ajili ya matumuzi ya hoteli yake, lakini umeme uliomo kwenye mita ni mwingi kuliko kiasi anachonunulia.

“Hawa tutakula nao sahani moja hadi watuambie wanakonunua umeme na hatimaye tutakamata mtambo unaozalisha uniti hizo bandia,” alisema.

Nangali alisema TANESCO itahakikisha inawatia mbaroni wauzaji wa uniti hizo kinyume cha sheria.

“Hawa kuna sehemu wananunua umeme lakini hatujafahamu ni wapi hivyo kukamatwa kwao ni dalili kubwa ya kubaini wanakonunua maana katika hali ya kawaida haiwezekani mtu awe na uniti hizi zote,” alifafanua Nangali.

Alitoa wito kwa Watanzania kutoa taarifa za wanaoihujumu TANESCO na kutangaza zawadi ya sh 50,000 kwa kila nyumba itakayokamatwa.

Alipoulizwa kuhusu ongezeko la faini na idadi ya watu waliofikishwa mahakamani, Nangali alisema idadi hiyo itajulikana mara baada ya kufanya majumuisho mwishoni mwa mwezi huu japo inakadiriwa kuwa zaidi ya watu 100 sasa wameshakamatwa na kulipishwa faini tangu kuanza kwa operesheni hiyo.

Wiki tatu zilizopita aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo, William Mhando, alitangaza kukamatwa kwa watu watatu mkoani Dodoma na wawili jijini Dar es Salaam waliokuwa wakitumia umeme ambao haujafahamika unakopatikana.

Serikali, walimu vitani • Ikulu yang’aka, yatoa tamko zito

SERIKALI na Chama cha Walimu Nchini (CWT) wameendelea kuvutana juu ya mgomo wa walimu unaotarajiwa kuuanza rasmi kesho kutwa nchi nzima.

Wakati Wizara ya Elimu na Mafunzo ikishindwa kutoa majibu ya kuridhisha juu ya hatma ya madai ya walimu hususan ongezeko la mishahara na malimbikizo ya stahiki zao, CWT imeipa serikali saa 48 ili kuipa nafasi ya kutimiza madai hayo vinginevyo wataanza mgomo.

Akizungumza na Tanzania Daima jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa CWT Ezekiel Oluoch alisema kuwa asilimia 95 ya walimu nchini wameunga mkono mgomo huo.

“Mgomo huo utawahusisha walimu wote walioko wilayani na mikoani, tunatarajia kuuanza rasmi Julai 30 asubuhi, kwa pamoja tutashikamana imara hadi serikali itekeleze madai yetu,” alisema Oluoch.

Naye Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo, Philipo Mulugo, aliwataka walimu hao kusitisha mgomo huo na badala yake wakutane na wizara kwa ajili ya majadilino na kuyatafutia ufumbuzi.

“Endapo dhamira yao itakuwa pale pale, watafakari madhara ya mgomo kwa sababu kuna taratibu zake na watakuwa wamekiuka, ukichukulia kwamba watakuwa hawajawatendea haki wanafunzi hivyo kwa pamoja washirikiane kufikisha hoja zao wizarani.

Hata hivyo alikwepa kuzungumzia suala la ongezeko la mshahara kwa walimu akidai kuwa si hao wanaokabiliana nalo tu, bali hata wafanyakazi wa sekta nyingine kama kilimo, afya, na wanakabiliwa na changamoto hiyo.

Vile vile alilitaka baraza lililotumika kuandaa mgomo huo litumie busara ya kukutana na serikali kwa maana hawatatenda haki kuingia katika mgomo wakati serikali haijashirikishwa.

“Hatuwezi kutoa tamko la moja kwa moja kuhusiana na ongezeko la mshahara la walimu ila ushauri wangu walimu waingie darasani kufundisha na kuipa serikali nafasi ya kutatua tatizo hilo,” alisema Mulugo.

Wakati walimu wakijiandaa kuanza mgomo Jumatatu ijayo, Ikulu ya Rais Jakaya Kikwete imetoa taarifa kupinga mgomo huo kwa madai kuwa ni batili kwani kuna kesi mahakamani.

Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu na kusainiwa na Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi, Peniel Lyimo, mgomo huu siyo halali kwa sababu shauri hili bado liko mahakamani.

“Kwa sasa, shauri hili liko Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi na leo hii siku ya Ijumaa Julia 27, 2012 majira ya saa sita mchana pande zote mbili zilifika mahakamani na mahakama ikaamuru kwamba pande zote zikamilishe maelezo yao ifikapo siku ya Jumanne Julia 31, 2012 saa sita mchana ili kuiwezesha mahakama kuendelea kusikiliza shauri hilo na hatimaye kutoa uamuzi. Kwa hiyo mgomo huo sio halali kwa vile shauri hilo bado liko mahakamani,” alisema Lyimo.

Lyimo alisema kwa msingi huo, hatua ya CWT kutoa notisi ya kuanza kwa mgomo kabla ya kukamilika kwa shauri hili ni kukiuka taratibu halali za kimahakama ambazo kila mmoja anawajibika kuziheshimu.

“Serikali inapenda kuwafahamisha walimu wote kuwa kujihusisha na mgomo huu ni kwenda kinyume cha sheria, kanuni na taratibu za kazi. Hivyo, walimu wanapaswa kupima madhara ya mgomo huu usiokuwa halali na serikali inawataka walimu kupuuza mgomo huo na kutokujihusisha nao. Walimu wote wanatakiwa waendelee na kazi kama kawaida,” ilisema taarifa hiyo.

Kwa mujibu wa Lyimo, serikali imepokea notisi ya saa arobaini na nane (48) ya kusudio la walimu kuanza kugoma Julai 30 mwaka huu, lakini kabla ya notisi hiyo, serikali imekuwa ikifanya jitihada kubwa za kujadiliana na viongozi wa CWT kuhusu jinsi ya kuboresha maslahi ya walimu kwa nia ya kumaliza suala hili kwa maelewano.

Juzi chama hicho kilitangaza mgomo rasmi huku kikikamilisha taratibu za mgomo kwa kupiga kura kuunga au kukataa mgomo huo ambapo asilimia 95 ya walimu walipiga kura kuunga mkono.

Hatua hiyo imekuja baada ya serikali na CWT kushindwa kufikia makubaliano katika siku 30 walizoipa kuanzia Juni 25 mwaka huu.