Monday, October 15, 2012

JK: Vurugu za kidini Mbagala zinaudhi

RAIS Jakaya Kikwete, amesema kuwa licha ya tukio la kijana wa Kikristo kukojolea kitabu kitakatifu cha Kuran kuudhi, lakini vurugu za kulipiza kisasi kwa kuchoma makanisa zinapaswa kuepukwa kwa vile si suluhu ya tatizo.

Akihutubia katika kilele cha kuzima Mwenge wa Uhuru, sherehe zilizokwenda sambamba na kumbukumbu za maadhimisho ya miaka 13 ya kifo cha Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere, mjini Shinyanga, Rais Kikwete alisema amechukizwa na hatua za watu kujichukulia sheria mkononi.

Kauli ya rais inakuja ikiwa ni siku tatu tangu vurugu kubwa kutokea eneo la Mbagala Kizuiani jijini Dar es Salaam na kusababisha makanisa saba na magari kadhaa kuharibiwa, baada ya mtoto Emmanuel Josephat (14) kudaiwa kukojolea kitabu hicho kitakatifu kinachotumiwa na Waislamu.

Rais Kikwete aliwaeleza wananchi kuwa ametembelea eneo hilo na kusisitiza kuwa kitendo hicho cha viongozi wa dini kuwahamasisha wafuasi wao kujichukulia sheria mkononi hakikuwa sahihi, kwa sababu kijana huyo alifanya tendo hilo bila kushurutishwa na kundi wala mtu yeyote.

Aliongeza kuwa iko haja ya wafuasi hao kujizuia na kutuliza hasira zao kwa kutafakari kwanza kwani hata kijana mwenyewe tayari alikuwa mikononi mwa Jeshi la Polisi.

“Kitendo cha kundi hilo la waumini wa Kiislamu kuingilia kazi za vyombo vya dola hakikuwa sahihi, kwa sababu kimesababisha mambo ya kusikitisha na yasiyokuwa na maelezo ya kujitosheleza ndani ya jamii.

“Niliwasihi kuwa pamoja na hasira walizokuwa nazo wawe na subira na kuvumiliana wakati viongozi wa dini zote mbili wanapojiandaa kukutana na kufikia muafaka,” aliongeza.

Rais Kikwete aliwataka wananchi wajiepushe na vitendo vya kuchochea vurugu na uvunjifu wa amani katika nchi, hivyo akawashauri wasichukue uamuzi wa hasira wakati wa tatizo kwa sababu kwa vyovyote vile ni lazima watadondokea kwenye makosa.

Alisema vijana 122 wanaodaiwa kutoka kundi la harakati za Kiislamu wakiwemo 36 vinara wakuu wa vurugu hizo, wanashikiliwa na polisi.

Katika hatua nyingine, Rais Kikwete aliwahamasisha Watanzania kuendelea kujitokeza kwa wingi kutoa maoni yao kwenye tume inayoratibu maoni bila kushawishiwa kwa ulaghai wa aina yoyote, kwamba hiyo ni haki na utashi wa kila mtu.

Akemea rushwa

Rais Kikwete katika hilo, aliwataka wananchi wote kuchukua jukumu la kupambana na vitendo vya rushwa pasipo kuwaachia kazi hiyo Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU).

Alisema vita hiyo ni ya kila mtu huku akiwapiga vijembe wale wanaolalamika uwepo wa vitendo hivyo pasipo kuchukuwa jukumu la kuwataja hadharani wahusika ili wachukuliwe hatua.

“Kama tunaendelea kulalamikia rushwa bila kuwataja wala rushwa haiwezi kutusaidia kuitokomeza. Rushwa ni hatari hasa inapoingia hata kwenye vyombo vya kusimamia sheria na kutoa haki,” alisema.

CCM watoa kauli

Wakati huo huo, Chama Cha Mapinduzi, kupitia kwa Katibu wa Halmashauri Kuu (NEC) Taifa, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, kimelaani vurugu za kidini zilizotokea Mbagala Kizuiani.

Alisema kuwa CCM kinalaani tukio la kukojelewa kwa kitabu kitakatifu cha Kuran na vile vile vitendo vya kuvamiwa na kuchomwa moto makanisa na uporaji wa mali, akisisitiza kuwa havifanani na mila na desturi za Watanzania.

“Kitendo cha kukojolea kitabu kitakatifu cha Waislamu hakikubaliki, na kitendo cha kuvamia na kuchoma moto nyumba za ibada za Wakristo na kufanya vurugu pia hakikubaliki,” alisema Nape.




JK: Vurugu za kidini Mbagala zinaudhi

RAIS Jakaya Kikwete, amesema kuwa licha ya tukio la kijana wa Kikristo kukojolea kitabu kitakatifu cha Kuran kuudhi, lakini vurugu za kulipiza kisasi kwa kuchoma makanisa zinapaswa kuepukwa kwa vile si suluhu ya tatizo.

Akihutubia katika kilele cha kuzima Mwenge wa Uhuru, sherehe zilizokwenda sambamba na kumbukumbu za maadhimisho ya miaka 13 ya kifo cha Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere, mjini Shinyanga, Rais Kikwete alisema amechukizwa na hatua za watu kujichukulia sheria mkononi.

Kauli ya rais inakuja ikiwa ni siku tatu tangu vurugu kubwa kutokea eneo la Mbagala Kizuiani jijini Dar es Salaam na kusababisha makanisa saba na magari kadhaa kuharibiwa, baada ya mtoto Emmanuel Josephat (14) kudaiwa kukojolea kitabu hicho kitakatifu kinachotumiwa na Waislamu.

Rais Kikwete aliwaeleza wananchi kuwa ametembelea eneo hilo na kusisitiza kuwa kitendo hicho cha viongozi wa dini kuwahamasisha wafuasi wao kujichukulia sheria mkononi hakikuwa sahihi, kwa sababu kijana huyo alifanya tendo hilo bila kushurutishwa na kundi wala mtu yeyote.

Aliongeza kuwa iko haja ya wafuasi hao kujizuia na kutuliza hasira zao kwa kutafakari kwanza kwani hata kijana mwenyewe tayari alikuwa mikononi mwa Jeshi la Polisi.

“Kitendo cha kundi hilo la waumini wa Kiislamu kuingilia kazi za vyombo vya dola hakikuwa sahihi, kwa sababu kimesababisha mambo ya kusikitisha na yasiyokuwa na maelezo ya kujitosheleza ndani ya jamii.

“Niliwasihi kuwa pamoja na hasira walizokuwa nazo wawe na subira na kuvumiliana wakati viongozi wa dini zote mbili wanapojiandaa kukutana na kufikia muafaka,” aliongeza.

Rais Kikwete aliwataka wananchi wajiepushe na vitendo vya kuchochea vurugu na uvunjifu wa amani katika nchi, hivyo akawashauri wasichukue uamuzi wa hasira wakati wa tatizo kwa sababu kwa vyovyote vile ni lazima watadondokea kwenye makosa.

Alisema vijana 122 wanaodaiwa kutoka kundi la harakati za Kiislamu wakiwemo 36 vinara wakuu wa vurugu hizo, wanashikiliwa na polisi.

Katika hatua nyingine, Rais Kikwete aliwahamasisha Watanzania kuendelea kujitokeza kwa wingi kutoa maoni yao kwenye tume inayoratibu maoni bila kushawishiwa kwa ulaghai wa aina yoyote, kwamba hiyo ni haki na utashi wa kila mtu.

Akemea rushwa

Rais Kikwete katika hilo, aliwataka wananchi wote kuchukua jukumu la kupambana na vitendo vya rushwa pasipo kuwaachia kazi hiyo Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU).

Alisema vita hiyo ni ya kila mtu huku akiwapiga vijembe wale wanaolalamika uwepo wa vitendo hivyo pasipo kuchukuwa jukumu la kuwataja hadharani wahusika ili wachukuliwe hatua.

“Kama tunaendelea kulalamikia rushwa bila kuwataja wala rushwa haiwezi kutusaidia kuitokomeza. Rushwa ni hatari hasa inapoingia hata kwenye vyombo vya kusimamia sheria na kutoa haki,” alisema.

CCM watoa kauli

Wakati huo huo, Chama Cha Mapinduzi, kupitia kwa Katibu wa Halmashauri Kuu (NEC) Taifa, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, kimelaani vurugu za kidini zilizotokea Mbagala Kizuiani.

Alisema kuwa CCM kinalaani tukio la kukojelewa kwa kitabu kitakatifu cha Kuran na vile vile vitendo vya kuvamiwa na kuchomwa moto makanisa na uporaji wa mali, akisisitiza kuwa havifanani na mila na desturi za Watanzania.

“Kitendo cha kukojolea kitabu kitakatifu cha Waislamu hakikubaliki, na kitendo cha kuvamia na kuchoma moto nyumba za ibada za Wakristo na kufanya vurugu pia hakikubaliki,” alisema Nape.




Friday, October 5, 2012

Sumaye amtangazia vita Lowassa

Mwenyewe asema wananchi wa Monduli ndiyo msuli wake

SIKU chache baada ya Waziri Mkuu mstaafu, Fredereck Sumaye, kubwagwa kwenye kinyang’anyiro cha ujumbe wa Halmashauri Kuu (NEC) ya CCM kupitia wilaya ya Hanang’ mkoani Arusha mwanasiasa huyo sasa ametangaza vita na Waziri Mkuu mwenzake mstaafu, Edward Lowassa.

Sumaye ambaye hajatangaza rasmi kuwania kiti hicho, anatarajiwa kupasua jibu wakati wowote kuanzia leo kueleza kilichotokea; msimamo wake na kwamba yuko tayari kuwania urais mwaka 2015 endapo Lowassa atawania kiti hicho.

Sumaye aliangushwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji na Uwezeshaji, Dk. Mary Nagu, katika kuwania nafasi ya ujumbe wa NEC wilaya ya Hanang, matokeo ambayo anaamini yana mkono wa Lowassa.

Chanzo cha karibu na Sumaye, kilisema kuwa pamoja na Waziri Mkuu huyo mstaafu kushindwa na Dk. Nagu kwa zaidi ya kura 167, amepokea matokeo hayo kwa shingo upande kwa kile alichoeleza kuwa ushindi huo ni wa mafisadi.

“Hataki kuzungumza chochote leo ila atazungumza nanyi wakati wowote kuanzia leo, lakini anasema ikiwa Lowassa atawania urais, Sumaye ataingia katika mpambano huo kukabiliana naye kwa njia yoyote. Hataki kusema ataingia kwa CCM au chama gani au mgombea binafsi,” anaeleza mtu wa karibu na Sumaye.

Vyanzo vilivyo karibu na mwanasiasa huyo vimeeleza kuwa tayari Sumaye amefanya mazungumzo na baadhi ya wanasiasa wenye ushawishi wanaojipambanua kama wapiganaji wa ufisadi ili kuunganisha nguvu kwa ajili ya kukabiliana na kambi ya Lowassa.

Mbali ya kundi la Sumaye na wanasiasa wengine kuanza mkakati huo, wapo pia wanasiasa wengine wenye majina makubwa ndani ya chama, serikali na wastaafu wanaotajwa kuingia kwenye muungano huo.

Akijibu tuhuma hizo kwa kifupi, Lowassa alisema endapo Sumaye ataitisha mkutano na waandishi wa habari na kutoa tuhuma hizo, nitajibu.

Hata hivyo, baadhi ya wafuasi wa Sumaye na watendaji wa ndani ya serikali wamesema kuanguka kwa mwanasiasa huyo mkongwe katika uchaguzi wa wilaya kunamuweka vizuri zaidi kisiasa kutokana na mazingira tete ya kisiasa ndani ya CCM, chama ambacho kimechokwa na umma.

Waziri wa zamani wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora) na mbunge wa zamani wa jimbo la Makete, Dk. Hassy Kitine, alikaririwa juzi akisema kuwa kuangushwa kwa Sumaye katika nafasi ya NEC hakuwezi kumuathiri kisiasa kama atachukua uamuzi wa kuwania urais mwaka 2015 kupitia CCM.

Dk. Kitine alitoa kauli hiyo alipoombwa na gazeti moja kutoa maoni yake juu ya matokeo ya NEC wilayani Hanang’ kama yana athari kwa mustakabali wa kisiasa kwa kiongozi huyo.

“Katiba ya CCM haina kipengele kinachosema kama unataka kuwania urais ni lazima uwe mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM , kwa hiyo nasema kama kweli Sumaye anatafuta urais bado ana nafasi ya kuwania nafasi hiyo,” alikaririwa akisema Dk. Kitine.

Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, naye alimtia moyo Sumaye kwa kuweka bayana kuwa uchaguzi wa NEC ni wa ngazi ya wilaya tu kwa hiyo Sumaye anaweza kuwa anakubalika kitaifa kuliko katika wilaya anayotoka huku akitumia usemi kwamba ‘nabii hakubaliki kwao’.

Katika hatua nyingine, hali inaelezwa kuwa tete ndani ya CCM baada ya kuwapo kwa taarifa za ushangiliaji kutoka kwa wafuasi na viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambao wameona wanazidi kusafishiwa njia.

“CHADEMA wameshangilia sana kwa kuwa sasa jimbo hilo litachukuliwa kirahisi. Walikuwa wanamuogopa Sumaye na kumheshimu hivyo kwa sasa watu wake wote wanahamia CHADEMA.

“Wanasema mafisadi walihakikisha wanampa kila mjumbe kiwango cha chini kabisa cha shilingi 100,000 kumuangusha Sumaye. Uongozi wote wa CCM wa wilaya na hata baadhi kwenye mkoa walijipanga kumuangusha,” anasema.

Katika uchaguzi huo wa Hanang, hali ilianza kuwa tete toka hatua za awali, ambapo Dk. Nagu alitajwa kushinikiza kubadilishwa kwa muhtasari wa kikao cha wilaya kilichokata jina lake na hivyo kurudishwa tena.

Taarifa kutoka Hanang zinaeleza kwamba Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), ilifanya kazi katika mazingira ya aibu kutokana na kuonekana kufumbia macho vitendo vya rushwa iliyogawiwa waziwazi.

Hivi karibuni Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Dk. Edward Hoseah, alinukuliwa akisema kwamba taasisi yake inafuatilia kwa karibu uchaguzi huo ndani ya CCM ili kubaini watu wanaotumia rushwa, kauli ambayo imeelezwa kuwa ya kisiasa zaidi.

Dk. Hoseah alitoa kauli hiyo akijibu hoja mbalimbali za washiriki wa kongamano la kujadili utekelezaji wa awamu ya pili ya mpango wa kupambana na rushwa nchini na mapendekezo yanayopaswa kuzingatiwa katika utekelezaji wa mpango wa awamu ya tatu (2012 – 2016).

Uchaguzi huo ulifanyika siku chache baada ya CCM kupitisha majina ya walioomba nafasi hizo huku wanachama wengi wakienguliwa kutokana na kukosa sifa katika kikao kilichomalizika mjini Dodoma mapema wiki hii.

Katika hatua nyingine, Lowassa ametamba kuwa wananchi wa Monduli ndiyo msuli wake wa kisiasa.

Akizungumza baada ya ushindi wa NEC alioupata, Lowassa alisema ushindi huo mkubwa umedhihirisha kuwa ana misuli ya kisiasa kwa wananchi wake.

“Kuna mzee rafiki yangu aliniambia kuwa katika kazi za siasa angalia ‘grass roots’, watu wanakuwa ndiyo msuli wako kisiasa, na mimi watu wa Monduli ndiyo msuli wangu,” alisema Lowassa ambaye anatajwa kuwa mmoja wa watu watakaowania urais mwaka 2015.

“Wananchi wa Monduli mmenithibitishia hilo na nawashukuru sana kutoka kwenye sakafu ya moyo wangu, jibu la thibitisho hilo kwangu ni utumishi uliotukuka kwenu,” aliongeza.

Lowassa alipata asilimia 93 ya kura dhidi ya wapinzani wake, Dk. Sulesh Toure aliyetangaza kujitoa baada ya kuona upepo mbaya kwake na Nanai Konina.

Sumaye amtangazia vita Lowassa

Mwenyewe asema wananchi wa Monduli ndiyo msuli wake

SIKU chache baada ya Waziri Mkuu mstaafu, Fredereck Sumaye, kubwagwa kwenye kinyang’anyiro cha ujumbe wa Halmashauri Kuu (NEC) ya CCM kupitia wilaya ya Hanang’ mkoani Arusha mwanasiasa huyo sasa ametangaza vita na Waziri Mkuu mwenzake mstaafu, Edward Lowassa.

Sumaye ambaye hajatangaza rasmi kuwania kiti hicho, anatarajiwa kupasua jibu wakati wowote kuanzia leo kueleza kilichotokea; msimamo wake na kwamba yuko tayari kuwania urais mwaka 2015 endapo Lowassa atawania kiti hicho.

Sumaye aliangushwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji na Uwezeshaji, Dk. Mary Nagu, katika kuwania nafasi ya ujumbe wa NEC wilaya ya Hanang, matokeo ambayo anaamini yana mkono wa Lowassa.

Chanzo cha karibu na Sumaye, kilisema kuwa pamoja na Waziri Mkuu huyo mstaafu kushindwa na Dk. Nagu kwa zaidi ya kura 167, amepokea matokeo hayo kwa shingo upande kwa kile alichoeleza kuwa ushindi huo ni wa mafisadi.

“Hataki kuzungumza chochote leo ila atazungumza nanyi wakati wowote kuanzia leo, lakini anasema ikiwa Lowassa atawania urais, Sumaye ataingia katika mpambano huo kukabiliana naye kwa njia yoyote. Hataki kusema ataingia kwa CCM au chama gani au mgombea binafsi,” anaeleza mtu wa karibu na Sumaye.

Vyanzo vilivyo karibu na mwanasiasa huyo vimeeleza kuwa tayari Sumaye amefanya mazungumzo na baadhi ya wanasiasa wenye ushawishi wanaojipambanua kama wapiganaji wa ufisadi ili kuunganisha nguvu kwa ajili ya kukabiliana na kambi ya Lowassa.

Mbali ya kundi la Sumaye na wanasiasa wengine kuanza mkakati huo, wapo pia wanasiasa wengine wenye majina makubwa ndani ya chama, serikali na wastaafu wanaotajwa kuingia kwenye muungano huo.

Akijibu tuhuma hizo kwa kifupi, Lowassa alisema endapo Sumaye ataitisha mkutano na waandishi wa habari na kutoa tuhuma hizo, nitajibu.

Hata hivyo, baadhi ya wafuasi wa Sumaye na watendaji wa ndani ya serikali wamesema kuanguka kwa mwanasiasa huyo mkongwe katika uchaguzi wa wilaya kunamuweka vizuri zaidi kisiasa kutokana na mazingira tete ya kisiasa ndani ya CCM, chama ambacho kimechokwa na umma.

Waziri wa zamani wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora) na mbunge wa zamani wa jimbo la Makete, Dk. Hassy Kitine, alikaririwa juzi akisema kuwa kuangushwa kwa Sumaye katika nafasi ya NEC hakuwezi kumuathiri kisiasa kama atachukua uamuzi wa kuwania urais mwaka 2015 kupitia CCM.

Dk. Kitine alitoa kauli hiyo alipoombwa na gazeti moja kutoa maoni yake juu ya matokeo ya NEC wilayani Hanang’ kama yana athari kwa mustakabali wa kisiasa kwa kiongozi huyo.

“Katiba ya CCM haina kipengele kinachosema kama unataka kuwania urais ni lazima uwe mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM , kwa hiyo nasema kama kweli Sumaye anatafuta urais bado ana nafasi ya kuwania nafasi hiyo,” alikaririwa akisema Dk. Kitine.

Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, naye alimtia moyo Sumaye kwa kuweka bayana kuwa uchaguzi wa NEC ni wa ngazi ya wilaya tu kwa hiyo Sumaye anaweza kuwa anakubalika kitaifa kuliko katika wilaya anayotoka huku akitumia usemi kwamba ‘nabii hakubaliki kwao’.

Katika hatua nyingine, hali inaelezwa kuwa tete ndani ya CCM baada ya kuwapo kwa taarifa za ushangiliaji kutoka kwa wafuasi na viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambao wameona wanazidi kusafishiwa njia.

“CHADEMA wameshangilia sana kwa kuwa sasa jimbo hilo litachukuliwa kirahisi. Walikuwa wanamuogopa Sumaye na kumheshimu hivyo kwa sasa watu wake wote wanahamia CHADEMA.

“Wanasema mafisadi walihakikisha wanampa kila mjumbe kiwango cha chini kabisa cha shilingi 100,000 kumuangusha Sumaye. Uongozi wote wa CCM wa wilaya na hata baadhi kwenye mkoa walijipanga kumuangusha,” anasema.

Katika uchaguzi huo wa Hanang, hali ilianza kuwa tete toka hatua za awali, ambapo Dk. Nagu alitajwa kushinikiza kubadilishwa kwa muhtasari wa kikao cha wilaya kilichokata jina lake na hivyo kurudishwa tena.

Taarifa kutoka Hanang zinaeleza kwamba Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), ilifanya kazi katika mazingira ya aibu kutokana na kuonekana kufumbia macho vitendo vya rushwa iliyogawiwa waziwazi.

Hivi karibuni Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Dk. Edward Hoseah, alinukuliwa akisema kwamba taasisi yake inafuatilia kwa karibu uchaguzi huo ndani ya CCM ili kubaini watu wanaotumia rushwa, kauli ambayo imeelezwa kuwa ya kisiasa zaidi.

Dk. Hoseah alitoa kauli hiyo akijibu hoja mbalimbali za washiriki wa kongamano la kujadili utekelezaji wa awamu ya pili ya mpango wa kupambana na rushwa nchini na mapendekezo yanayopaswa kuzingatiwa katika utekelezaji wa mpango wa awamu ya tatu (2012 – 2016).

Uchaguzi huo ulifanyika siku chache baada ya CCM kupitisha majina ya walioomba nafasi hizo huku wanachama wengi wakienguliwa kutokana na kukosa sifa katika kikao kilichomalizika mjini Dodoma mapema wiki hii.

Katika hatua nyingine, Lowassa ametamba kuwa wananchi wa Monduli ndiyo msuli wake wa kisiasa.

Akizungumza baada ya ushindi wa NEC alioupata, Lowassa alisema ushindi huo mkubwa umedhihirisha kuwa ana misuli ya kisiasa kwa wananchi wake.

“Kuna mzee rafiki yangu aliniambia kuwa katika kazi za siasa angalia ‘grass roots’, watu wanakuwa ndiyo msuli wako kisiasa, na mimi watu wa Monduli ndiyo msuli wangu,” alisema Lowassa ambaye anatajwa kuwa mmoja wa watu watakaowania urais mwaka 2015.

“Wananchi wa Monduli mmenithibitishia hilo na nawashukuru sana kutoka kwenye sakafu ya moyo wangu, jibu la thibitisho hilo kwangu ni utumishi uliotukuka kwenu,” aliongeza.

Lowassa alipata asilimia 93 ya kura dhidi ya wapinzani wake, Dk. Sulesh Toure aliyetangaza kujitoa baada ya kuona upepo mbaya kwake na Nanai Konina.

Mjane wa Mwangosi alilia rambirambi za Slaa

Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa

UTAMADUNI mpya wa siasa za misibani, unaoendana na mauaji yaliyotokana na ukaidi wa wanasiasa kwa Jeshi la Polisi, umeanza kuiumbua Chadema ambayo imejikuta ikishindwa kutimiza ahadi ndogo ndogo za kutoa rambirambi inazoahidi kwa wafiwa.

Juzi, mjane wa mwandishi wa habari wa kituo cha televisheni cha Channel Ten, Daudi Mwangosi, Aneti, alijikuta akiomba wanahabari wasaidie kufuatilia rambirambi iliyoahidiwa na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa kutokana na kiongozi huyo, kukata mawasiliano baada ya msiba.

“Nina mawasiliano na Profesa Mark Mwandosya ambaye pia aliahidi kumsomesha mtoto mmoja, yeye aliniambia nitakapokuwa tayari nimjulishe ili atume fedha kwenye akaunti ya shule, lakini sina mawasiliano na Dk Slaa,” alisema Aneti.

Mwangosi aliuawa Septemba 2 mwaka huu, kwa kupigwa na kitu kinachodaiwa kuwa ni bomu katika Kijiji cha Nyololo, wilayani Mufindi mkoani Iringa.

Aliuawa wakati Polisi ikizuia wafuasi na viongozi wa Chadema kufanya mikutano ya hadhara ambayo ilipigwa marufuku ili kuruhusu shughuli ya Sensa ya Watu na Makazi, kufanyika bila kuingiliwa.

Baada ya mauaji hayo, wakati wa maziko ya mwandishi huyo, Dk Slaa aliahidi kubeba jukumu la kusomesha mtoto wa kwanza wa Mwangosi aitwaye Nehemiah, ambaye yuko kidato cha nne katika Sekondari ya Malangali, Mufindi, Iringa.

“Mtoto huyu alifika na kutaka kujua sababu za kifo cha baba yake, kwa uchungu huku machozi yakimtoka, nimewasiliana na mdau wangu na kuahidi kubeba jukumu la kumsomesha na pia naahidi kufuatilia ahadi hiyo kwa kipindi chote cha masomo yake,” alinukuliwa Dk Slaa akiahidi.

Hata hivyo ahadi hiyo, mbali na ukweli kuwa haijatekelezwa, lakini pia hata mawasiliano kati yake na mjane wa Mwangosi hayapo mpaka mjane huyo kuamua kuomba waandishi wamfuatilie.

Mwingine aliyeahidi kusaidia familia hiyo ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais asiye na Wizara Maalumu, Profesa Mwandosya, ambaye aliiwakilisha Serikali na katika salamu zake za rambimbambi msibani, alisema atabeba jukumu la kusomesha watoto wengine wa marehemu huyo.

Aliahidi pia kufuatilia ahadi za watu wengine katika kuisaidia familia ya Mwangosi kwa kuwa ni ndugu yake na jirani. “Nitahakikisha familia hii inaishi maisha kama ambavyo angelikuwapo baba yao kwa kuhakikisha kila mtoto wa familia hiyo anasoma kwa kila hatua kwa kuzingatia kuwa hao ni sehemu ya familia yangu,” alisema Mwandosya, ambaye pia ni Mbunge wa Rungwe Mashariki (CCM).

Alipopigiwa Dk Slaa simu kujua mipango yake ya kutekeleza ahadi hiyo, simu yake ilikuwa inaita mara zote bila kupokewa.

Rambirambi zingine Wakati huo huo, wafanyakazi wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) mkoani Iringa, wametoa rambirambi zao kwa mjane huyo. Mhasibu Mkuu wa Tanroads Iringa, Alex Mgeta alikabidhi Sh 265,000 juzi katika nyumba yao iliyopo Kihesa Bwawani mjini hapa.

“Nashukuru sana lakini pia nawaomba kwa kupitia michango ambayo nimeambiwa inaendelea kukusanywa mnisaidie nimalizie nyumba hii,” alisema Aneti.

Aneti alisema nyumba hiyo yenye vyumba vinne vya kulala haijakamilika na ikikamilika, atapangisha baadhi ili kiasi cha fedha atakachopata kitumike kuendesha familia yake.

Septemba 30 katika harambee iliyofanyika Iringa kwa mujibu wa blogu ya Mjengwa, Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Kabwe Zitto alijitolea kumchangia mjane huyo kwa kumlipia ada ya uanachama wa Bima ya Afya kila mwezi kwa miaka mitatu mfululizo.

Alikaririwa akisema: "Nimeona nami niunge mkono harambee hii. Pamoja na michango ya fedha iliyotolewa kumsaidia mjane kuanzisha mradi wa kujikimu, naona ni muhimu akawa na uhakika wa huduma ya afya yake na watoto wake wanne.

Hivyo, mchango wangu utakuwa ni kwenye eneo hilo la Bima ya Afya kwa miaka mitatu.

"Baadhi ya watu wengine maarufu waliojitokeza kumchangia mjane kupitia mtandao wa kijamii wa Mjengwablog.com ni pamoja na Shy-Rose Bhanji, Ananilea Nkya, John Bukuku na Mobhare Matinyi aliyepata kuwa Mhariri wa Majira.

Mjane wa Mwangosi alilia rambirambi za Slaa

Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa

UTAMADUNI mpya wa siasa za misibani, unaoendana na mauaji yaliyotokana na ukaidi wa wanasiasa kwa Jeshi la Polisi, umeanza kuiumbua Chadema ambayo imejikuta ikishindwa kutimiza ahadi ndogo ndogo za kutoa rambirambi inazoahidi kwa wafiwa.

Juzi, mjane wa mwandishi wa habari wa kituo cha televisheni cha Channel Ten, Daudi Mwangosi, Aneti, alijikuta akiomba wanahabari wasaidie kufuatilia rambirambi iliyoahidiwa na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa kutokana na kiongozi huyo, kukata mawasiliano baada ya msiba.

“Nina mawasiliano na Profesa Mark Mwandosya ambaye pia aliahidi kumsomesha mtoto mmoja, yeye aliniambia nitakapokuwa tayari nimjulishe ili atume fedha kwenye akaunti ya shule, lakini sina mawasiliano na Dk Slaa,” alisema Aneti.

Mwangosi aliuawa Septemba 2 mwaka huu, kwa kupigwa na kitu kinachodaiwa kuwa ni bomu katika Kijiji cha Nyololo, wilayani Mufindi mkoani Iringa.

Aliuawa wakati Polisi ikizuia wafuasi na viongozi wa Chadema kufanya mikutano ya hadhara ambayo ilipigwa marufuku ili kuruhusu shughuli ya Sensa ya Watu na Makazi, kufanyika bila kuingiliwa.

Baada ya mauaji hayo, wakati wa maziko ya mwandishi huyo, Dk Slaa aliahidi kubeba jukumu la kusomesha mtoto wa kwanza wa Mwangosi aitwaye Nehemiah, ambaye yuko kidato cha nne katika Sekondari ya Malangali, Mufindi, Iringa.

“Mtoto huyu alifika na kutaka kujua sababu za kifo cha baba yake, kwa uchungu huku machozi yakimtoka, nimewasiliana na mdau wangu na kuahidi kubeba jukumu la kumsomesha na pia naahidi kufuatilia ahadi hiyo kwa kipindi chote cha masomo yake,” alinukuliwa Dk Slaa akiahidi.

Hata hivyo ahadi hiyo, mbali na ukweli kuwa haijatekelezwa, lakini pia hata mawasiliano kati yake na mjane wa Mwangosi hayapo mpaka mjane huyo kuamua kuomba waandishi wamfuatilie.

Mwingine aliyeahidi kusaidia familia hiyo ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais asiye na Wizara Maalumu, Profesa Mwandosya, ambaye aliiwakilisha Serikali na katika salamu zake za rambimbambi msibani, alisema atabeba jukumu la kusomesha watoto wengine wa marehemu huyo.

Aliahidi pia kufuatilia ahadi za watu wengine katika kuisaidia familia ya Mwangosi kwa kuwa ni ndugu yake na jirani. “Nitahakikisha familia hii inaishi maisha kama ambavyo angelikuwapo baba yao kwa kuhakikisha kila mtoto wa familia hiyo anasoma kwa kila hatua kwa kuzingatia kuwa hao ni sehemu ya familia yangu,” alisema Mwandosya, ambaye pia ni Mbunge wa Rungwe Mashariki (CCM).

Alipopigiwa Dk Slaa simu kujua mipango yake ya kutekeleza ahadi hiyo, simu yake ilikuwa inaita mara zote bila kupokewa.

Rambirambi zingine Wakati huo huo, wafanyakazi wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) mkoani Iringa, wametoa rambirambi zao kwa mjane huyo. Mhasibu Mkuu wa Tanroads Iringa, Alex Mgeta alikabidhi Sh 265,000 juzi katika nyumba yao iliyopo Kihesa Bwawani mjini hapa.

“Nashukuru sana lakini pia nawaomba kwa kupitia michango ambayo nimeambiwa inaendelea kukusanywa mnisaidie nimalizie nyumba hii,” alisema Aneti.

Aneti alisema nyumba hiyo yenye vyumba vinne vya kulala haijakamilika na ikikamilika, atapangisha baadhi ili kiasi cha fedha atakachopata kitumike kuendesha familia yake.

Septemba 30 katika harambee iliyofanyika Iringa kwa mujibu wa blogu ya Mjengwa, Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Kabwe Zitto alijitolea kumchangia mjane huyo kwa kumlipia ada ya uanachama wa Bima ya Afya kila mwezi kwa miaka mitatu mfululizo.

Alikaririwa akisema: "Nimeona nami niunge mkono harambee hii. Pamoja na michango ya fedha iliyotolewa kumsaidia mjane kuanzisha mradi wa kujikimu, naona ni muhimu akawa na uhakika wa huduma ya afya yake na watoto wake wanne.

Hivyo, mchango wangu utakuwa ni kwenye eneo hilo la Bima ya Afya kwa miaka mitatu.

"Baadhi ya watu wengine maarufu waliojitokeza kumchangia mjane kupitia mtandao wa kijamii wa Mjengwablog.com ni pamoja na Shy-Rose Bhanji, Ananilea Nkya, John Bukuku na Mobhare Matinyi aliyepata kuwa Mhariri wa Majira.