Thursday, August 29, 2013

MCH. MOSES KULOLA AFARIKI.


Nimesoma kwa masikitiko ktk chanzo kimoja cha habari kuwa mtumishi halisi wa Mungu baba Moses Kulola amefariki dunia kwa ugonjwa wam mapafu (mwenye taarifa zaidi atujuze). Mtumishi huyu wa ukweli (ukifananisha na hawa wanaoota ka uyoga siku hizi) alizaliwa 1928, aliilinda imani kwa uthabiti na ni mchango mkubwa sana kwa wokovu wa wengi Tanzania na nje ya mipaka.
Hakika mwendo ameumaliza, imani ameilinda na amevipiga vita vilivyo vizuri. Hakika mbingu imempokea shujaa huyu! Amina.