Friday, September 13, 2013

UGONJWA WA KUOTA NYWELE MWILI MZIMA WAWATESA

 
Ndugu hawa watatu kati ya sita waliozaliwa katika familia moja wameathirika na ugonjwa uitwao kitaalamu werewolf syndrom au kwa jina lingine hypertrichosis. Ugonjwa huu huweza kumfanya mgonjwa kuweza kuota nywele karibu kila sehemu ya mwili wake hasa sehemu za usoni. ni mara chache sana kumpata gonjwa anayeumwa ugonjwa huu kwani wataalamu wanasema kua hutokea kwa mtu mmoja katika watu bilioni moja.

Ndugu hawa wote wanatokea nchini india, wa kwanza anaitwa Savita (miaka 23), wa pili Monisha (miaka 18) na wa mwisho ni Savitri (miaka 18) ambao wote hawa katika maisha yao wamelazimika kutumia dawa ambazo huweza kuwasaidia kupunguza uwezo wa nywele zao kukua kwa kasi.
 
Mama mzazi wa watoto hao anasema chanzo cha ugonjwa huo ni kutoka kwa baba yao, akielezea historia ya maisha yake alisema kua aliolewa kwa kulazimishwa. Na alikuja kujua kua mumewe ni mwathirika wa ugonjwa huo siku ya ndoa yao. Katika kuongezea zaidi amesema kutokana na umaskini walionao wameshindwa kulipia kiasi cha fedha kwa ajili ya watoto wake hao kufanyawa upasuaji, kwani gharama ya upasuaji kwa mgonjwa mmoja ni zaidi ya $7,000 za kimarekani. Mama huyo aliimalizia kwa kuomba msaada ili watoto wake waweze pata msaada wa kufanyiwa upasuaji ili nao siku moja waweze pona na kuolewa.