Wednesday, August 29, 2012

IGP Mwema amwangukia Dk. Slaa

Polisi waunda tume kuchunguza mauaji yaliyotokea Moro
WAKATI serikali imeunda tume kuchunguza mauaji yaliyotokea juzi mjini Morogoro baada ya polisi kuwashambulia wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Said Mwema amemwomba Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa kusitisha maandamano na mikutano ya hadhara ya Movement For Change (M4C), kwa siku tano kupisha zoezi la sensa.

Dk. Slaa aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa, chama chake kimetafakari na kukubali kusitisha mikutano yake ambayo jana ilipaswa kufanyika mjini Iringa.

Alisema jana CHADEMA ilipanga kufanya mkutano wake wa kwanza mjini Iringa katika viwanja vya Mwembetogwa na tayari walishapata kibali cha polisi mkoani humo kufanya maandamano wakiwa ndani ya magari.

“Lakini ilipofika majira ya saa 3 usiku juzi, tulipata simu kutoka kwa mkuu wa polisi kwamba maandamano yetu yamesitishwa na kutengua mambo yote tuliyoafikiana nao.

“Asubuhi ya leo (jana), tulipigiwa simu na RPC na kutueleza kuwa wanataka kuonana na viongozi wa CHADEMA, huku wakiwa na hoja ya kutaka tuahirishe kufanya mikutano kutokana na sensa na hoja nyingine ni kwamba wananchi wa Iringa watakuwa wameathirika na kifo cha kijana aliyeuawa Morogoro,” alisema Dk. Slaa.

Alisema baada ya kutokubaliana na hoja zote za polisi, alipigiwa simu na IGP Mwema akimwomba Dk. Slaa kusitisha mikutano na maandamano kwa siku tano mkoani Iringa na kwamba vyama vyote vya siasa havitaruhusiwa kufanya mikutano ya hadhara katika kipindi hiki cha sensa.

“IGP nimeongea naye leo kwa dakika 40 akiniomba kwa kuniita…, ‘Dk. Slaa sijawahi kukuomba hata siku moja naomba nikuombe na usinikatalie kwamba ndani ya siku tano kuanzia leo, tumezuia vyama vya siasa kufanya mikutano ya hadhara kutokana na zoezi la sensa na wewe na chama chako tunawaomba msitishe mikutano yenu’,” alisema Dk. Slaa akimnukuu IGP Mwema.

Kwa mujibu wa Dk. Slaa, CHADEMA imekubaliana na ombi la IGP Mwema kusitisha mikutano yao ya hadhara, lakini wataendelea na ratiba ya mikutano ya ndani wakiwa mjini Iringa.

Alilitaka Jeshi la Polisi baada ya kumalizika kwa sensa, wasije na visingizio vingine vya kusimamisha mikutano yao kwani hawatakubali kusikia masharti mengine.

“Sisi CHADEMA tunawapa polisi nafasi ya mwisho na nchi hii inaongozwa na sheria. Nataka dunia nzima ifahamu na kujua kuwa kufanya maandamano ni haki ya kikatiba kwa kila mwananchi,” alisema.

Wakati polisi wakisitisha mikutano na maandamano, mapokezi ya msafara wa CHADEMA uliowasili mkoani Iringa jana, uliwashitua polisi ambao walikuwa na wakati mgumu kuweka doria na askari wenye silaha kila kona.

Katika hatua nyingine, CHADEMA imetangaza kushiriki mazishi ya marehemu Ally Nzona (38), aliyefariki dunia kwa kupigwa risasi kichwani na polisi mkoani Morogoro.

Alisema CHADEMA kitashiriki katika mazishi ya kijana huyo na kugharamia shughuli zote za mazishi bila kujali kama alikuwa mwanachama wa CHADEMA au la.

“Kama familia yake itaamua kusoma dua hapa Morogoro na kumzika hapa, tutashiriki kikamilifu, tumejadiliana na wanafamilia kuna mambo ya msingi tumekubaliana na walichoomba ni kusaidia kusafirisha mwili,” alisema Dk. Slaa.

Kamanda wa Polisi mkoani Morogoro, Faustine Shilogile alisema polisi wanaendelea na uchunguzi kwani hadi sasa haijulikani endapo kijana huyo alifariki dunia kwa kupigwa bomu, risasi au ajali.

Kifo cha kijana huyo kilitokea juzi katika eneo la Msamvu, Manispaa ya Morogoro ambapo wafuasi wa CHADEMA walikuwa wakiandamana kuwapokea viongozi wao wa kitaifa kwa ajili ya mkutano wa hadhara.

Wakati huo huo, serikali imeunda tume kuchunguza kifo cha kijana huyo.

Hatua hiyo ilitangazwa jana na Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk. Emmanuel Nchimbi wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na mazingira ya vurugu hizo.

Dk. Nchimbi alisema jopo la tume hiyo ambalo hakulitaja, litafanya uchunguzi kubaini chanzo cha mazingira ya kifo hicho.

“Polisi walikuta mtu mwenye majeraha mwilini ambaye baada ya kufikishwa hospitalini, alifariki dunia. Polisi Makao Makuu wameunda jopo kuchunguza ili kupata ukweli wa kile kilichosababisha kifo cha mtu huyo,” alisema Dk. Nchimbi.

Bila kutaja majina na idadi ya wajumbe waliomo kwenye jopo hilo na muda gani wataifanya kazi hiyo, Dk. Nchimbi alisema baada ya uchunguzi ndipo ukweli juu ya kile kilichosababisha kifo cha mtu huyo utajulikana.

Nzona alidaiwa kupigwa risasi kando ya meza ya magazeti.

Mbali ya kifo cha Nzona aliyeripotiwa kuwa ni mpiga debe katika mabasi ya Msamvu, Frank Mbalimba na Hashim Seif walijeruhiwa wakati polisi walipotumia nguvu kuwatawanya wafuasi wa CHADEMA.

Dk. Nchimbi alisema polisi walizuia maandamano hayo ili kupisha zoezi la sensa kwani yangeleta usumbufu.

Waziri huyo aliwataka viongozi wa vyama vya siasa kuheshimu sheria za nchi na kuongeza kuwa, kama mtu anahisi ameonewa afuate utaratibu kuwasilisha madai yake na sio kutumia nguvu.

IGP Mwema amwangukia Dk. Slaa

Polisi waunda tume kuchunguza mauaji yaliyotokea Moro
WAKATI serikali imeunda tume kuchunguza mauaji yaliyotokea juzi mjini Morogoro baada ya polisi kuwashambulia wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Said Mwema amemwomba Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa kusitisha maandamano na mikutano ya hadhara ya Movement For Change (M4C), kwa siku tano kupisha zoezi la sensa.

Dk. Slaa aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa, chama chake kimetafakari na kukubali kusitisha mikutano yake ambayo jana ilipaswa kufanyika mjini Iringa.

Alisema jana CHADEMA ilipanga kufanya mkutano wake wa kwanza mjini Iringa katika viwanja vya Mwembetogwa na tayari walishapata kibali cha polisi mkoani humo kufanya maandamano wakiwa ndani ya magari.

“Lakini ilipofika majira ya saa 3 usiku juzi, tulipata simu kutoka kwa mkuu wa polisi kwamba maandamano yetu yamesitishwa na kutengua mambo yote tuliyoafikiana nao.

“Asubuhi ya leo (jana), tulipigiwa simu na RPC na kutueleza kuwa wanataka kuonana na viongozi wa CHADEMA, huku wakiwa na hoja ya kutaka tuahirishe kufanya mikutano kutokana na sensa na hoja nyingine ni kwamba wananchi wa Iringa watakuwa wameathirika na kifo cha kijana aliyeuawa Morogoro,” alisema Dk. Slaa.

Alisema baada ya kutokubaliana na hoja zote za polisi, alipigiwa simu na IGP Mwema akimwomba Dk. Slaa kusitisha mikutano na maandamano kwa siku tano mkoani Iringa na kwamba vyama vyote vya siasa havitaruhusiwa kufanya mikutano ya hadhara katika kipindi hiki cha sensa.

“IGP nimeongea naye leo kwa dakika 40 akiniomba kwa kuniita…, ‘Dk. Slaa sijawahi kukuomba hata siku moja naomba nikuombe na usinikatalie kwamba ndani ya siku tano kuanzia leo, tumezuia vyama vya siasa kufanya mikutano ya hadhara kutokana na zoezi la sensa na wewe na chama chako tunawaomba msitishe mikutano yenu’,” alisema Dk. Slaa akimnukuu IGP Mwema.

Kwa mujibu wa Dk. Slaa, CHADEMA imekubaliana na ombi la IGP Mwema kusitisha mikutano yao ya hadhara, lakini wataendelea na ratiba ya mikutano ya ndani wakiwa mjini Iringa.

Alilitaka Jeshi la Polisi baada ya kumalizika kwa sensa, wasije na visingizio vingine vya kusimamisha mikutano yao kwani hawatakubali kusikia masharti mengine.

“Sisi CHADEMA tunawapa polisi nafasi ya mwisho na nchi hii inaongozwa na sheria. Nataka dunia nzima ifahamu na kujua kuwa kufanya maandamano ni haki ya kikatiba kwa kila mwananchi,” alisema.

Wakati polisi wakisitisha mikutano na maandamano, mapokezi ya msafara wa CHADEMA uliowasili mkoani Iringa jana, uliwashitua polisi ambao walikuwa na wakati mgumu kuweka doria na askari wenye silaha kila kona.

Katika hatua nyingine, CHADEMA imetangaza kushiriki mazishi ya marehemu Ally Nzona (38), aliyefariki dunia kwa kupigwa risasi kichwani na polisi mkoani Morogoro.

Alisema CHADEMA kitashiriki katika mazishi ya kijana huyo na kugharamia shughuli zote za mazishi bila kujali kama alikuwa mwanachama wa CHADEMA au la.

“Kama familia yake itaamua kusoma dua hapa Morogoro na kumzika hapa, tutashiriki kikamilifu, tumejadiliana na wanafamilia kuna mambo ya msingi tumekubaliana na walichoomba ni kusaidia kusafirisha mwili,” alisema Dk. Slaa.

Kamanda wa Polisi mkoani Morogoro, Faustine Shilogile alisema polisi wanaendelea na uchunguzi kwani hadi sasa haijulikani endapo kijana huyo alifariki dunia kwa kupigwa bomu, risasi au ajali.

Kifo cha kijana huyo kilitokea juzi katika eneo la Msamvu, Manispaa ya Morogoro ambapo wafuasi wa CHADEMA walikuwa wakiandamana kuwapokea viongozi wao wa kitaifa kwa ajili ya mkutano wa hadhara.

Wakati huo huo, serikali imeunda tume kuchunguza kifo cha kijana huyo.

Hatua hiyo ilitangazwa jana na Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk. Emmanuel Nchimbi wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na mazingira ya vurugu hizo.

Dk. Nchimbi alisema jopo la tume hiyo ambalo hakulitaja, litafanya uchunguzi kubaini chanzo cha mazingira ya kifo hicho.

“Polisi walikuta mtu mwenye majeraha mwilini ambaye baada ya kufikishwa hospitalini, alifariki dunia. Polisi Makao Makuu wameunda jopo kuchunguza ili kupata ukweli wa kile kilichosababisha kifo cha mtu huyo,” alisema Dk. Nchimbi.

Bila kutaja majina na idadi ya wajumbe waliomo kwenye jopo hilo na muda gani wataifanya kazi hiyo, Dk. Nchimbi alisema baada ya uchunguzi ndipo ukweli juu ya kile kilichosababisha kifo cha mtu huyo utajulikana.

Nzona alidaiwa kupigwa risasi kando ya meza ya magazeti.

Mbali ya kifo cha Nzona aliyeripotiwa kuwa ni mpiga debe katika mabasi ya Msamvu, Frank Mbalimba na Hashim Seif walijeruhiwa wakati polisi walipotumia nguvu kuwatawanya wafuasi wa CHADEMA.

Dk. Nchimbi alisema polisi walizuia maandamano hayo ili kupisha zoezi la sensa kwani yangeleta usumbufu.

Waziri huyo aliwataka viongozi wa vyama vya siasa kuheshimu sheria za nchi na kuongeza kuwa, kama mtu anahisi ameonewa afuate utaratibu kuwasilisha madai yake na sio kutumia nguvu.

Vita CCM

• Sumaye, Lowassa, Chenge wakimbia kundi la kifo
WAKATI leo ndiyo siku ya mwisho kuchukua na kurejesha fomu za kuwania uongozi ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ngazi ya wilaya, mkoa na taifa, mpambano wa kuwania nafasi hizo umekuwa ni vita kali iliyojikita katika kulipizana visasi, chuki na kuibua makundi ya urais mwaka 2015.

Mnyukano mkali upo katika kuwania uongozi wa jumuiya za chama hicho ambazo ni Umoja wa Vijana (UVCCM), Wanawake (UWT) na Wazazi.

Nafasi zingine za wajumbe wa NEC ambazo zimekuwa na ushindani mkubwa ni kupitia kapu maalumu, maarufu kwa jina la ‘Kundi la Kifo’ ambalo safari hii lina viti 10 Bara na 10 Visiwani.

Ushindani uliopo katika kundi hilo, umesababisha baadhi ya vigogo ambao wamekuwa na kawaida kuwania NEC kupitia kundi hilo, kukimbia na safari hii wanaomba nafasi hizo kupitia wilaya zao.

Baadhi ya vigogo waliokimbia kundi la kifo na wanaotajwa kutaka kuwania urais mwaka 2015 ni pamoja na mawaziri wakuu wastaafu, Edward Lowassa na Fredrick Sumaye.

Sumaye ameachukua fomu ya NEC wiki iliyopita wilayani Hanang, akichuana vikali na Mbunge wa Hanang, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji na Uwezeshaji, Dk. Mary Nagu.

Uamuzi wa Nagu ambaye amepata kuwa meneja kampeni wa Sumaye katika mbio za urais mwaka 2005, umewashangaza wengi kwani wadadisi wa masuala ya siasa nje na ndani ya CCM, wanaamini kuwa mafanikio yake kisiasa, yametokana na waziri mkuu huyo mstaafu.

Wakati Sumaye akikimbilia Hanang, Lowassa naye amekimbilia wilayani kwake Monduli ambako amechukua fomu ya NEC.

Mwingine aliyekimbilia wilayani, ni Mwanasheria Mkuu mstaafu na Mbunge wa Bariadi Mashariki, Andrew Chenge.

Vigogo wengine waliokimbia kundi hilo ni Kapteni John Komba na Christopher Gachuma.

Duru za siasa ambazo gazeti hili imezipata, zinasema kuwa vigogo hao wameamua kukimbilia wilayani kukacha kundi la kifo baada ya CCM kufanya mabadiliko ya katiba ambapo kundi hilo litakuwa na viti kumi tu badala ya 20.

“Kundi la kifo safari hii lina viti kumi tu badala ya 20, na mara nyingi kumekuwa na kura za kiitifaki. Uwezekano wa kushindwa ni mkubwa mno, lakini pia ukipata kwa kura chache na kama una malengo ya kisiasa kwa 2015, haikupi nafasi nzuri. Ndiyo maana wazee wameona watokee kwenye wilaya zao,” alisema mmoja wa viongozi wa CCM.

Sababu nyingine inayotajwa vigogo hao kukimbia kundi la kifo, ni kutokana na ukweli kwamba endapo sekretarieti yote itaamua kugombea, nafasi sita kati ya kumi zinaweza kuchukuliwa nao, hivyo waombaji wengine wakalazimika kupigana vikumbo kuwania nafasi nne.

Mnyukano nafasi za mikoa

Mnyukano mkali upo katika nafasi za wenyeviti wa mikoa.

Mkoani Shinyanga, Mwenyekiti anayetetea kiti chake, Khamis Mgeja ameshikwa shati na hasimu wake kisiasa, Mbunge wa Kahama, James Lembeli.

Kabla hata ya zoezi la kuchukua fomu, mahasimu hawa walikuwa wakirushiana maneno, huku Mgeja akimfananisha Lembeli sawa na sisimizi ambaye hawezi kumyima usingizi.

Mkoani Dar es Salaam, Mwenyekiti wa sasa, John Guninita amekaliwa kooni na mjumbe wa Halmashauri Kuu Taifa, Ramadhani Madabida wakati Dodoma Adam Kimbisa anachuana na mkongwe William Kusila.

Aidha, kazi ipo mkoani Mwanza ambako Mbunge wa zamani wa Ilemela, Antony Diallo ameamua kuchukua fomu kumkabili mwenyekiti wa sasa, Clementi Mabina na mkoani Mara Makongoro Nyerere yuko jino kwa jino na Kisieri Chambili.

Wenyekiti Jumuiya ya Wazazi

Katika uchaguzi huo, unaotarajiwa kufanyika Novemba, Mbunge wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono amerejea tena kuwania nafasi ya mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Taifa.

Katika uchaguzi uliopita, Mkono aligombea kiti hicho, lakini jina lake lilienguliwa na NEC kwa sababu ambazo hadi sasa hazijajulikana.

Mkono anachuana na Mbunge wa Bukoba Vijijini, Joson Rweikiza, Matha Mlata na Salum Chicago.

Kwa upande wa UWT, Waziri Sofia Simba anaoneshana kazi na Mbunge wa Same Mashariki, Anna Kilango. Tayari wagombea hao wanaopewa nafasi kubwa, wameanza tambo za kisiasa.

Kazi ipo pia wilayani Nzega ambako Mbunge wa Nzega, Khamis Kingwangala na hasimu wake kisiasa, Hussein Bashe watachuana kuwania NEC kupitia wilaya hiyo.
source: Tanzania daima.